Zakumi,
Sasa namwelewa Mwanakijiji alipozungumzia swala la UMASKINI kwa sababu tunaviumiza vichwa vyetu ktk kutafuta tafsiri na mazungumzo badala ya kuweka nguvu hizi ktk utekelezaji maana hakuna tafsiri ya UMASKINI ktk UCHUMI zaidi ya matokeo ya uwezo mdogo ktk kupata maendeleo. Ni hali halisi ulonayo regardless of what You have in store na ndio maana nikasema kamauna njaa wakati chakula kipo ndani ya friji huwezi kusema huna njaa ati nimeshiba wakati tumbo lako ni empty.
Labda ktk mfano huo huo naweza kusema kwamba Ulimbukeni wetu ulotokana na kutawaliwa ndio uliotuponza kiasi kwamba chakula kipo ghalani toka mahindi, mchele, mtama na mawele isipokuwa tunataka chakula cha Mlimani City na Shoppers ambacho kiko tayari chenye hadhi ya kimataifa na kieleezo za Utajiri.. bila kujua thamani kubwa ya mahindi na mawele tuloyaacha maghalani ambayo wazungu wanakuja tena kwetu kuyataka kutokana na wao kuthamini Organic.
Hapa nikiwa na maana kwamba tuna all economic resources ambazo zinaweza kabisa kutuondoa ktk umaskini (njaa) lakini sii chakula tunachokitaka na tunatumia nguvu kubwa ktk Imported good ili kujibadirisha sisi tuonekane sawa ama kama wazungu. Sisi tunashindwa kukubali reality, na kama nisemavyo kila siku WATU na MAZINGIRA ndio focus kubwa ya neno maendeleo. Maendeleo sio watu pekee bali mazingira yao pia na wlaa huwezi kuita utajiri in aconomic term ikiwa mazingira ni mabaya. Hivyo policies zote zinapowekwa hutazama kuboresha vitu hivi vyote na sii kimojawapo.
Huyo Mmasai sisi tutamwita tajiri kwa sababu tunazithaminisha hizo ng'ombe zake 500 ktk bei za soko na kutoa namba zinayomweka Mmasai ktk utajiri au laa, lakini maadam mazingira yake yapo ktk hali mbaya utajiri wake unabakia tumbo tupu kwa sababu kuwepo kwa ng'ombe hawa na kuthaminishwa kwake bila kubadirisha maisha na mazingira yake utajiri huu ni mtupu. Na ndio maana huyo mmasai hana habari kwamba yeye ni tajiri japokuwa ana ng'ombe 500 sawa na sisi wenye dhahabu ambazo hazibadilishi maisha wala mazingira yetu. Huyu Masai sii Fukara bali ni Maskini kwa sababu umaskini unakusanya hali na mali za watu na mazingira kiuchumi..
Navyofikiria mimi, tukiondoa leo neno maendeleo basi bila shaka hata neno maskini litapotea japokuwa fukara na tajiri yatabakia kwa sababu inawahusu WATU tu na sio mazingira waliyopo. Na ktk umaskini ndio unakuta vitu kama elimu vinachangia sana kutambua mahusiano ya watu na mazingira ktk uboreshaji wake. Na neno uchumi linatokana na elimu ya kuelewa, kutambua na kupima production, distribution, and consumption of goods and services. Maadam jamii zetu zinakua na mahitaji yetu yanazidi kupanda wakati uwezo wa kutosheleza mahitaji haya unazidi kupungua ndipo neno maskini linapochukua nafasi na hivyo kusema Umaskini ni matokeo ya kushindwa kukidhi mahitaji yetu.
Kuna jambo moja hunikera sana mimi japokuwa halikubaliwi na Watanzania wengi..nalo ni matumizi ya Lugha ya kiswahili. Tumejenga utamaduni wa kuiga hadi lugha ili kuwahudumia watanzania wasiojua kiingereza, hivyo kweli tunatumia lugha kama means of communication baina ya wananchi au na kina nani?. Sasa matokeo yake mashirika yote nchini utakuta ma CEOs, board mebers na executive officers ni wageni ambao wataajiri Watanzania wanaozungumza lugha yao hao ma TX ili ku serve Watanzania ambao hawajui kiingereza. Hii kweli hatufanyi kinyume?
Kwa nini nafasi zote za juu ktk ashirika yatu zichukuliwe na wageni ambao hawawezi kuwasiliana na wananchi ila kwa kumtumia Mtanzania anaye ajiriwa kama mkarimani baina ya mgeni na Watanzania halafu hata huyo Mtanzania anapoichukua kazi ile hafahamu kwamba yeye anatumiwa kama mkarimani ila naye anakuwa mzungu ktk mawasiliano kuwataka walio chini yake na wananchi wazungumze kiingereza..
Inakuwaje Wachina wanapoingia nchini inawachukua onlt miezi sita au mwaka wanazungumza kiswahili na sio kiingereza kuwasiliana na wananchi lakini MKenya atakuja tanzania na kupewa wadhifa na nafasi kubwa kwa sababu anazungumza kiingereza, pengine hana elimu kuliko Mchina au Mtanzania..Na mwisho nawaacha na swali jingine, kwa nini nchi zote zinazotumia lugha ya kigeni ambayo sii yao ndio wako nyuma ktk maendeleo?. Hakuna Mhindi wala Mchina asiyejua kusoma na kuandika Kichina hadi maofisini mwao vitu vimeandikwa Kichina au kihindi lakini sisi hata matangazo yetu yameandikwa kiingereza ilihali ni asilimia chini ya 20 ndio wanazungumza kiingereza. Hapa mlengwa wa matangazo hayo ni nani > Unamtangazia nani?