Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Kila ninapotembelea hifadhi ya SERENGETI kupitia vijiji vya ISSENYE, MOTUKERI, NATTA, MAKUNDUSI, IKOMA, BURUNGA vikiwa katika lindi la umasikini na ufukara, machozi huwa yananilengalenga!

Mkuu kweli ukienda Singida, Tabora hata Ngorongoro utasikitika Watu walivyopigwa na maisha.
Hivi Watu wa Mtwara Wakibana gesi isito kwenda Dar tusiwalaumu kwani Wanaona Wenzao wa Ngorongoro, Serengeti Kahama, Mwadui, Kiwira walivyoachwa "SOLEMBA" NA KUBAKIA WAKITAZAMA MANDHARI SAFI ZA MASAKI, MBEZI BEACH, OYSTERBAY NA AKIBA ZA WAKUBWA HUKO UGHAIBUNI ZINAVYOTUTUMUKA.
 
vyote hivo tunavyo cha ajabu wananchi wanao zuguka hifadhi hizi wapo nyuma kweli kimaendeleo hawana zahanati,shule zipo mbali na huduma za maji ni shida tupu. umefika wakati wa ku-pay back to the community kwa kufanya coorperate-community conservation ili nao wawe na sense of ownership.
 
mchawi ni ccm mkiendelea kuikumbatia watakaoendelea kuneemeka ni akinana RIz moko. huyu mama anayetembea na ndege ya serikali kwa ajili ya NGO yake binafsi ya WAMA.
 
Mleta uzi asante kwa kuwa na upeo wa kutuwekea katika janvi leetu tujadili. Kama unavyojiuliza "Sijui kwa nini Tanzania ni Maskini". Nina imani kila Mtanzania mzalendo anajiuliza swali hili la muhimu.Mimi ni mdau wa utalii na niko humo kwenye utalii katika sekta binafsi.Tuna kila sababu ya kujivunia kutokana na mbuga zetu na jinsi TANAPA wanavyojitahidi kuzitunza ukilinganisha na majirani zetu.Watalii wanaoingia Serengeti wanaongezeka mwaka hadi mwaka.Ukitoa utalii wa picha (photographic safaris), kuna uwindaji katika maeneo tengefu kama Selous na kwingineko.Gharama za kuingia katika hifadhi kwa wageni ni kati ya $ 35 na $ 50 kwa kichwa kwa siku kutegemeana na hifadhi, kuna wanaokwenda safari za kupiga kambi (camping safaris) hizi zina gharama za nyongeza.

Mdau Nasikia hata mkomazi kwa Sasa inakuja juu maana iko pembezoni mwa barabara ya Same to Dar hivo ni rahisi kufikika ila ngoma inakuja kwenye makusanyo hayataeleweka wala kusaidia Wakaazi wa Same Waliotunza pori hilo toka Enzi na Enzi.
 
mchawi ni ccm mkiendelea kuikumbatia watakaoendelea kuneemeka ni akinana RIz moko. huyu mama anayetembea na ndege ya serikali kwa ajili ya NGO yake binafsi ya WAMA.

Mkuu mchawi siyo ccm, bali ni wale waTanzania wanaoipa kura na wale wanaosaidia kuiba kura ili waonekane wameshinda na hivyo kuendelea kubaki madarakani. wapiga kura ndiyo wachawi wakubwa!:frusty:
:frusty::frusty::frusty:
 
Ni masikini kwasababu mapato yote tunategemea kodi. Watalii wakija walipe ili waone hayo maajabu, the real value is in accomodation, food, transport and shopping ya vitu vyetu.
Hawa watalii wakija wanaishia kwenye mahoteli ambayo sio ya watanzania, tours sio za watanzania, magari maduka ambayo sio ya watanzania. In the end we only benefit 10% of the whole package.

We should look at the whole tourism industry with a wide view. Animals have drawn them to us, we should exploit every posible way to make them spend cash here also see how we can maximize our profit and profit sio lazima government upate kodi. As long as they bring money into the local economy we expect multiplier effect.

We dnt need to have a million visitors to benefit, what is needed is to make sure they spend a lot directly into the local economy while they are here. This doesn't mean you hike prices but rather diversify our product at affordable rates. Make their visit worth while, this way we will reap billions of dollars and get rid of this bad omen called poverty.
 
Kwa jinsi hali ilivyo inabidi tuwarithishe watoto wetu wimbo wa :Tanzania Nakupenda kwa moyo: maana tembo wanaisha madini nayo yako hatihati tusikubali lazima vitu tulivyovikuta viwe endelevu.
 
JK alishasema nae hajui kwanini Nchi ni maskini. Nchi yenye kila kitu kizuri tatizo Uongozi mbovu.

Ahadi za Mwana Tanu kapuni.
 
nyumbu ni naturally kuzaa kwa wakati mmoja hii huwasaidia kujihami na maadui kwani watoto huwa wengi na kwa muda mfupi almost wote wanakuwa kama wanalingana kwa mwonekano.pia cha ajabu zaidi kwangu ni uwezo wao wa ku delay kuzaa mpaka muda wa wiki tatu incase mazingira si salama.motto wao ni "do what i do, ask me later" hasa wanapovuka mto.
 
Salaam wana JF!

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali za Benki ya Dunia, Shirika la Fedha la Kimataifa na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa, Tanzania ni moja kati ya mataifa masikini sana duniani.

Umasikini huo upo licha ya maliasili lukuki zilizotapakaa kwenye kila kona ya nchi:

a. Maziwa makubwa yenye samaki na viumbemaji vya kutosha - Mwanza, Kagera, Mara, Kigoma, Ruvuma n.k.

b. Mito mikubwa yenye samaki wa kutosha - Kagera, Mara, Ruvuma, Iringa, Mtwara, Tanga, Kilimanjaro, Rukwa n.k.

c. Misitu mikubwa yenye rasilimali mbao, wanyamapori, madawa ya asili, matunda, nyuki n.k. - Manyara, Tanga, Lindi, Kigoma, Kilimanjaro, Tabora, Rukwa, Iringa n.k.

d. Wanyamapori wa kila aina - Mara, Arusha, Kigoma, Iringa, Tanga, Manyara, Pwani, Kilimanjaro, Rukwa, Zanzibar n.k.

e. Bahari ya Hindi yenye viumbebahari wa kila aina - Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Lindi na Zanzibar.

f. Madini ya kila aina - Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Mwanza, Shinyanga, Tabora, Mara, Kagera n.k.

g. Na sasa ina gesi - Mtwara

Pamoja na rasilimali watu, takribani milioni 45.

Sasa swali kwa wanachama, wapenzi, washabiki na wanazi wa CCM, kwa nini Tanzania bado ni masikini sana?

Ni swali jepesi sana, lakini lenye kuhitaji majibu ya uhakika na kina.

Cc: Ritz chama zomba Jichola3 ZeMarcopolo Nduka [MENTION=95413]thatha Atongwele
 
Last edited by a moderator:
Jibu la swali lako liko kwenye hiyo sifa h.

Uvivu wa watu na porojo za wanasiasa?!? Kwa ndiyo sababu ya umasikini wetu?

Kama ndivyo, kwa nini CCM bado inaendelea kuongoza taifa la watu wavivu na wapenda porojo?
Kwa miaka takribani 52 sasa, chama kinaongoza taifa la watu wavivu? Huoni kuwa ni dalili za chama kushindwa katika sera na mikakati yake? Kwani ilipaswa iwe na mikakati ya kuwafanya watu wafanye kazi!!

Kwa maana hiyo, taifa la watu wavivu na wapenda porojo ndilo utoa viongozi wavivu na wapenda porojo. Hivyo taifa la rais mvivu na mpenda porojo, waziri mkuu na mawaziri pia!!
Hii inamaanisha pia serikali ya wavivu na wapenda porojo.

Sasa na wewe chifu unawatetea wavivu na wapenda porojo?
 
Jibu lako ni RUSHWA. Watanzania ni wapenda rushwa. Kila mmoja anataka kujichumia zake. Na hili tatizo liko kwa wote sio CCM bali kwa watanzania wote.
 
Uvivu wa watu na porojo za wanasiasa?!? Kwa ndiyo sababu ya umasikini wetu?

Kama ndivyo, kwa nini CCM bado inaendelea kuongoza taifa la watu wavivu na wapenda porojo?
Kwa miaka takribani 52 sasa, chama kinaongoza taifa la watu wavivu? Huoni kuwa ni dalili za chama kushindwa katika sera na mikakati yake? Kwani ilipaswa iwe na mikakati ya kuwafanya watu wafanye kazi!!

Kwa maana hiyo, taifa la watu wavivu na wapenda porojo ndilo utoa viongozi wavivu na wapenda porojo. Hivyo taifa la rais mvivu na mpenda porojo, waziri mkuu na mawaziri pia!!
Hii inamaanisha pia serikali ya wavivu na wapenda porojo.

Sasa na wewe chifu unawatetea wavivu na wapenda porojo?

Kwani CCM imeingia madarakani kwa mtutu wa bunduki?
 
Jibu lako ni RUSHWA. Watanzania ni wapenda rushwa. Kila mmoja anataka kujichumia zake. Na hili tatizo liko kwa wote sio CCM bali kwa watanzania wote.

Rushwa? Sasa serikali ya CCM inaendeleaje kuongoza taifa la wapenda rushwa? Kwa nini isiseme imeshindwa na iachie ngazi?
 
Kwani CCM imeingia madarakani kwa mtutu wa bunduki?

Kwa nini isiachie ngazi kama imeshindwa kutoa uvivu na upenda porojo wa watanzania?

Ndiyo haijaingia kwa mtutu, lakini kama unaona hiyo ndiyo sababu ya umasikini, basi serikali yako ya CCM iachie ngazi, maana imeshindwa kazi.
 
Back
Top Bottom