Raia Mwema
JF-Expert Member
- Jun 30, 2008
- 535
- 79
Tunapenda sana kutumia muda mwingi wa maisha yetu kulalamika
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
a. Viongozi wabovu; wachoyo na wanaopenda wananchi wawe maskini ili watawale kirahisi 1961-1985...
b. Viongozi wabovu; wachoyo na wanaopenda kutumia akili za IMF na WB kuliko akili zao na wananchi wao 1985-1995
c. Viongozi wabovu; wachoyo na walafi kuibia wananchi, kuuza mali za umma, kuingia kwenye miktaba mibovu 1995-2005
d. Viongozi wabovu; wachoyo na wanaopenda kutumia akili za IMF na WB kuliko akili zao na wananchi 2005-2015..
Tatizo la kwanza uongozi, la pili wananchi na la tatu technology
Shukran sana umetimiza moja ya sababu za umaskini wetu.. Hatupendi kusoma...Mkuu, nimefanya makusudi kabisa kuandika hivi ili nipate kuona ni wangapi watapenda kuisoma yote na kutambua mapungufu yetu..
...............
Baada ya kuwa mwanajanvi wa JF kwa muda mrefu sana, kusoma mabandiko mbalimbali na kusoma makala za magazeti, mawazo ya wasomi wetu na kadhalika nimegundua kitu kimoja ya kwamba sisi Watanzania - We are into denial..Ni maskini lakini hatudhani kama sisi ni maskini kweli na tumejenga fikra za kwamba MTU akifanya kazi kwa bidiii kubwa bila shaka ataweza kufanikiwa kutokana na umaskini. Lakini tunasahau kwamba Umaskini ni stage ya mtu kukwama ktk hali na mali na mbinu zinazotumika hapa ni tofauti kabisa na zile za kujiendelea mbele. Sasa unapoweka nguvu kubwa ktk uzalishaji kweli unaweza kujiondoa ktk umaskini hali umaskini unatokana na sababu zake kama vile gari lililokwama tunatakiwa kutazama limekwamba wapi ktk tope, mchanga au shimo na ndipo tutafahamu jinsi ya kujikwamua na sii kuganyaga mafuta kuongeza kasi. Magurudumu yatazunguka tu hatutatoka hapo tulipokwama.
MTU, hili neno pekee linajenga Ubinafsi na kubomoa nguvu ya jumla, inavunja Utaifa na kuelekeza mapambano haya kwa fikra za kila mmoja wetu atachunga mzigo wake kama abiria walikosa matumaini ya usafiri baada ya gari lao kukwama na hivyo kila mmoja wao atafute usafiri wake..Fikra hizi za kila mmoja atafute usafiri wake, ndicho kinachofanyika nchini na ndio sababu tumeshindwa kutoka ktk umaskini maana sote tumeliacha gari la Taifa lilipokwama na kila mmoja wetu anatazama usafiri wake hali tuko katikati ya msitu na pasipo dira..na maskini ya Mungu hatufahamu tunaelekea wapi. Ni kweli kabisa kwamba uongozi mbaya ndio ulotupeleka ktk korongo hili la umaskini na tumekwama lakini sio uongozi mbaya unaotufanya tuchukue maamuzi ya kila mtu abebe msalaba wake..
Je, tunafikiri fikra za kwamba tukipata kiongozi au uongozi mzuri tutaweza kujinasua ktk umaskini tulipokwama? na huyu kiongozi au viongozi wanatakiwa wawe na moyo gani, wananchi wenyewe wanaweka matumaini yapio ikiwa leo kila mmoja wetu anadai maisha magumu aongezewe mshahara na posho ili hali wanajua fika kwamba tumekwama sote. Hivi kweli ikiwa wabunge kujiongezea posho ni makosa basi yatulazimu sisi wote tuombe raha hizo sawa na wao japokuwa tunajua fika kwamba wanayodai viongozi wetu ni makosa makubwa na ndizo sababu zinazotuweka ktk umaskini?..Ndizo sababu zinazotufanya tuwatake waondoke ktk madaraka na mageuzi ya kweli lazima yazingatie kwanza kwamba tumekwama na uzalendo unatakiwa kwanza.
Watanzania wenzangu ifike mahala tufikirie tumetoka wapi na tumekwama wapi, badala ya kuendelea kufikiria tunakwenda wapi.. Tanzania tumekwama ktk umaskini na tumeshindwa kutoka ktk umaskini. Na kibaya zaidi ni kwamba - WE CAN"T HANDLE THE TRUTH!.. bado tupo ktk kuamini kutoamini kwamba tuna watu wachache sana WAZURI (A few good men) ktk ngazi zote za uongozi na uwajibikaji kuweka Uzalendo mbele ya kila kitu. Hivi kweli Utawala wa leo toka Azimio la Zanzibar wamekosa aibu kabisa ya kufikiria Ufisadi mkubwa wanaoufanya kwa wananchi wao huku wakiendesha siasa za chuki baina ya watanzania kwa kutumia mapungufu ya Mtanzania huyo (ujinga, umaskini na maradhi) kama nyenzo ya kumuumiza zaidi.
Tuna msemo wa kwamba TAIFA MBELE? hivi tunaposema Taifa kwanza huwa tuna maana gani? Ni vitu gani vinatangulia ktk kulinda maslahi ya Taifa hadi tuseme TAIFA kwanza hali nafsi zetu zimegawanyika ktk makundi ya Ukabila, dini, rangi wanawake na wanaume, vyama na kadhalika. Hivi tunaposema Utaifa kwanza huwa tunatazama sifa zipi za uzalendo ikiwa kila mmoja wetu anatafuta riziki yake, anapanga malengo yake kwa manufaa ya maslahi yake ikiwa ni haki yake ya kuzaliwa na kama mtu huru?. Nini maana na kipimo cha UTU wa kila mmoja wetu ktk Utaifa wetu na huu utaifa unatokana na mipaka gani?.
Wanabodi lazima tukubali ukweli uliosimama ya kwamba tumeshindwa!...TUMESHINDWA!... na hakuna njia bora zaidi ya kufikiria - Ikiwa kweli tumeshindwa, je tulikosea wapi?... Mada nyingi sana hapa JF zinazungumzia sana matumizi mabaya ya mamlaka kwa viongozi wetu lakini katu tumeshindwa kujitazama sisi wenyewe sote kama ni MASIKINI na tumekwama ktk umaskini kama Taifa na sii mtu au kundi la watu pekee.. Vita ya kujikomboa kutokana na umaskini, ujinga na maradhi imekuwa sii vita ya kitaifa japokuwa tunasema na kulalama siku zote kwamba sisi ni Maskini.
Ebu tufikirie mfano mmoja mdogo sana ktk kutazama mbinu za kidunia ktk ubunifu. Leo hii Somalia wako ktk matatizo makubwa ya Ukame (drought and famine) na wamekwama... Hivi kweli itakuwa busara kwao leo kufikiria kupambana na matatizo haya ya ukame inatakiwa regime change?.. au kila mmoja wao atie nguvu ktk uzalishaji. Kama ndivyo tumewahi jiuliza kwa nini Somalia imeshindwa kuondokana na vita kwa zaidi ya miaka 20 sasa hivi hadi wamefikia hapo walipo!...
- Je, kumpata kiongozi bora inaweza kuwaondolea njaa na ukame ili hali regime change na nguvu ya kumtafuta kiongozi bora zaidi ndio chanzo cha mtafaruku baina yao toka aondolewe Siad Barre na leo wamefikia hapo walipo?..
- Je, sii kweli kwamba ukame ni matokeo ya vita ambayo imetokana na kupoteza UZALENDO unaomfanya kila mmoja wao kuto heshimu na kuwajibika kwa taifa lake kwanza. Somalia wamekwama na hawataweza kujikwamua hata siku moja kama hawatarudi nyuma na kutazama jinsi gani walipoteza Utaifa wao.
Kwa hiyo, wanabodi tuumize vichwa vyetu kutazama tumekwama wapi na sababu zipi zilizotukwamisha na sii wapi tunakwenda ama tunataka kwenda. Ni imani yangu kwamba siku tuloomba Uhuru tulijua fika tunataka kwenda wapi na nadhani hakuna shida ya leo kujua tunataka kwenda wap bvali kuondoka ktk shimo hili la umaskini tulipokwama. Ni lazima tukubali vichwani mwetu kwamba tumekwama ili tupate kufikiria na kutunga mbinu zote za ujasiri, mhanga na uzalendo zilenge ktk kujinasua ktk shimo hili.
Hao Somalia leo hawawezi kufikiria kutafuta chakula kilichopikwa na chef toka hotel za nyota tano kama suluhisho la ukame. Itakuwa ujinga na ulimbukeni mkubwa sana lna bahati mbaya sisi Watanzania tunajaribu sana kutafuta suluhisho la umaskini wetu kwa kutafuta vitu kutoka nyota tano, kutafuta ushauri wa ki nyota tano bila kujali kwamba tumekwama. Huu ni ulimbukenii wa kuficha uchafu wetu wenyewe, ni ulimbukeni wa kujisitir aibu na kamwe hatuwezi kupambana na imaskini kwa majigambo na usanii wa kuweka viraka ktk nguo iliyochakaa. Watanzania wenzangu hatuwezi ondokana na Ujinga umaskini na maradhi ikiwa vita hii ni ya mtu mmoja mmoja kwa fikra kwamba umaskini wetu ni wakujitakia, kila mmoja wetu atabeba msalaba wake wa matatizo.
Sio Ufisadi wala uongozi mbaya ndizo sababu kubwa, bali haya yote ni matokeo ya upungufu ktk imani inayomjenga mtu mmoja mmoja kujinasua ktk lindi la Umaskini, hivyo ktk jitihada za kujikomboa tunajikuta tunakanyagana hovyo kila mmoja wetu akitaka atoke yeye kwanza utafikiri kaa wa bahari waliowekwa ktk kapu wakisubiri kutiwa ktk sufuria la maji ya moto.
Hivi kweli watumishi wa umma hasa wataalam na mabingwa wetu wanaolipwa mshahara chini ya mil 2 lakini hupewa nyumba, wasilipe maji na umeme, wamepewa fursa ya kufanya biashara nje ya ajira walizoajiriwa wakijenga conflict of interest kiutawala kwa taaluma zao ili kujineemesha bado wana haki ya ki UTU kudai wao malipo zaidi kutokana na ugumu wa maisha japokuwa wanajua fika kwamba Tanzania ni nchi maskini na tumekwama kt umaskini. Viongozi wetu ngazi zote za kijamii tafadhali lihurumieni Taifa letu, wahurumieni waja wenu walipa kodi maana mnawaweka ktk nafasi ngumu sana ya kufikia maamuzi ya kinyama maana tofauti baina ya binadamu na mnyama kifikra ni ndogo sana..
Kwahiyo mtazamo wako ni kwamba tatizo kubwa ni uongozi. Fine. Tukianza na seheme ya kwanza hapo juu i.e. 1961 - 1985, Nyerere inaonekana ndio unamlenga hapa. Alipenda wananchi wawe maskini, awatawale kirahisi ili afaidike na nini kama nyerere? Sehemu 'b' contradicts with sehemu 'a' in the sense kwamba sehemu 'a' kulikuwa na self determination, sio WorldBank na IMF. Vinginevyo sehemu b, c, and d, naunga mkono hoja kwa kiasi fulani, ingawa Mwinyi kwa kiasi fulani hakuwa na jinsi.
Ila nina swali - Je, kwa mtazamo wako, sababu kuu ya umaskini wetu ni sababu za ndani tu? Sababu zote za umaskini wetu zipo ndani ya uwezo wetu?
Dah ama kweli sasa wewe unafanya ubishi ule ule unaoturudisha nyuma. sasa kama ningekuwa na jibu si ningeandika kichwa cha mada kisomoke - Hili ndilo suluhisho la umaskini wetu?Bandiko hilo hapo juu ndilo lilonishawishi kurudi kwenye post ya kwanza ya uzi huu.
Vurugu zote hizo hapo chini nilikuwa najaribu kutafuta kuona kama umekuja na wazo jipya la ufumbuzi wa juu ya swali la msingi ulilouliza katika 'title' ya uzi huu. Nimejitahidi kusoma neno kwa neno na kutafakari kwa muda kila sentensi uliyoandika kwa utulivu. Nasikitika kukwambia/kukuandikia kuwa sikuona jipya. Sikuona suluhisho la swali hilo la msingi. Umeishia kulalamika tu juu ya hali halisi iliyopo hapa nchini. Ninachokijua sifa nyingine ya ziada ya Great thinker akishakuona tatizo,akalitafakari , akaelewa kiini chake anatakiwa aje na suluhisho la tatizo hilo. Suluhusho hilo linatakiwa liwekatika maelezo yanaoeleweka kwa kada zote zinazohusika. Huo ndio mtazamo wangu juu ya namna ulivyoleta mada yako. Ninakuomba unisamehe kama nitakuwa nimekukwaza kwa jinsi nilivyotafakari chapicho/andiko/post yako.
Well watu nyerereism lazima muogope kwamba tunamlenga kwasababu ni ukweli; ili apate nini nimesema ili AWATAWALE kirahisi amefanikiwa ndio maana ame-over stay 24 yrs bankrupty country and people ...
Yes sababu kubwa ni ya ndani; na ni uongozi mbovu; kwani uongozi wa ndani unatakiwa ufanye analysis za external effects na kufanya uamuzi ambao ni kwa faida ya wananchi wake..
Umaskini ni tatizo la uongozi mbovu 1961-1985; 1985-1995 to date
Mkuu wangu nashukuru sana kuungana nami ktk kuumiza kichwa ktk swala hili. Nadhani tumepata majibu mengi sana kuhusiana na sababu zilizotufanya tufike hapa tulipo.Mkuu Mkandara,
Nakubaliana na wewe kimsingi kwenye maeneo mengi. Mimi naomba tu niuchokoze tu huu mjadala kidogo. Mtazamo kuhusu umaskini wetu umegawanyika katika maeneo mawili:Mtazamo wa ndani na Mtazamo wa Nje. Kwa upande moja, mtazamo wa ndani una jenga hoja kwamba umaskini wetu ni matokeo ya vitu kama uongozi mbovu (especially lack of political will), sera za ovyo, ufisadi na attitude ya watanzania kuhusu ‘kazi' (attitude towards work). Wajenga hoja hii wanadai kwamba haya ni matatizo ambayo yapo ndani ya uwezo wetu. Kwa upande mwingine, mtazamo wa nje unajenga hoja kwamba umaskini wetu ni matokeo ya ukoloni mamboleo ambao umetufunga nchi maskini kwenye mfumo wa kibepari wa kimataifa usiotendea haki mataifa madogo kama Tanzania. Wajenga hoja hii wanadai kwamba haya ni matatizo yaliyo nje ya uwezo wetu.
Nadhani mjadala ungekuwa na afya zaidi iwapo tungejaribu kutenganisha mitazamo hii kabla ya kuichanganya pamoja ili kubaini majibu sahihi.
Mkandara, kwanza nisamehe kwa kuwa nilipfunguwa nyuzi yako nikaanza kucheka, nimechaka kwa kuwa ni ndefu sana, sikipitia kwa kina yote nime "peruse" tu, lakini nn uhakika nimekuelewa.
Kwanza napenda ufahamu kuwa viongozi wanatokana na wananchi wanawatumikia. Ikiwa wananchi wajinga, wazembe, wavivu, waongo, wazandik, wachawi, mafataani, wapenda vya bure, omba omba, roho mbaya, husda, chuki, hawana uaminifu, wazikaji, matapeli, hawapendi wenzao wafanikiwe, wala rushwa na watowa rushwa, wazinzi, waficha maovu, wanaogopana, wanalindana uovu, na kila sifa mbaya uijuwayo.
Sasa fikiri. Hiyo ndio jamii ya Watanzania walivyo na hiyo ndivyo uongozi wa mwanzo ulivyoiacha ikawa hivyo kwa kuweka misingi mibovu na kutokujuwa walifanyalo na kuifanya nchi ni "lab" ya kufanyia majaribio. Hivyo ndivyo 90% ya Watanzania walivyo. Kuwabadilisha kwa haraka haraka si rahisi. Kubomoa ni rahisi kuliko kujenga. Nyumba inayojengwa miaka mitano mpaka 10 inabomolewa kwa dakika moja tu. Sisi tumebomolewa kwa miaka 24 mfululizo, chukuwa hiyo halafu kila mwaka mmoja tuliobomolewa uupe miaka mitano tu ya kutengeneza, itatuchukuwa kwa uchache miaka 120 toka tulipoanza kutengeneza, imepita miaka 26 toka matengezo yaanze bado tuna miaka 94 kwa uchache.
Usitegemee neema zote mpaka baadaa ya miaka hiyo kuanzia leo. Tunajitahidi na dalili zinaonekana na "improvements" zipo. Toka tulikuwa tunatowa wahitimu wachache wa vyuo vikuu sasa wamezidi maradufu, toka tuliwa tukitaka hata kwenda Mwanza tupite Kenya, sasa hakuna tena hilo. Toka ilikuwa hatuwezi kumiliki majumba, sasa tunaweza kumiliki majumba na maroshan. Tutafika, lakini hesabu zake ndio hizo.
Siku ntakayoona Tanzania kuna kiwanda cha kutengeza sindano za cherehani ndio siku ntajuwa sasa tunaanza kuendelea, kabla ya hapo ni bado kabisa.