KadaMpinzani,
Ok tuseme JK anafahamu matatizo ya Watanzania kwa lugha kwamba ni Watanzania wenye mapungufu na sio yeye ama nchi, hapa mjomba utakuwa hujaitazama shilingi yetu sisi wananchi kwani tunachodai ni kwamba rais wetu JK kutokana na majibu yake hafahamu matatizo ya nchi - Tanzania.
Mathlan umesema mwenyewe kuwa hatuna maji safi wakati tuna maziwa mangapi?...Tunajua kwamba anafahamu yote haya lakini anaposhindwa kukidhi mahitaji kama haya tuseme kitu gani?
Kama ukimwambia mtu aliyeko Ulaya kuwa Tanzania ina matatizo ya maji hatakuelewa kwa sababu jibu lake ataangalia ramani na kuyaona maziwa na mito mingi yenye maji safi. Mtu huyu hawezi kamwe kukubaliana na usemi wetu na ndio JK na wenbgiu manazi wake wanavyoitazama Tanzania.
Huyu mzungu alotazama ramani atakuomba Ushahidi na sio rahisi kwetu kumpa ushahidi huo bila yeye kufika Tanzania na kuyaona yeye mwenyewe.
JK anachokiona ni mali nyingi lakini anashindwa kuelewa kwa nini bado nchi ni maskini. For a President hii ni aibu kubwa sana mjomba! anapozidi kukana ukweli huu namwona kama yule mzungu aliyetazama ramani na hakuamini tanzania kuna shida ya maji!
Hivi alipojipanga kugombea kiti cha Urais alifikiria kazi yake kubwa pale Ikulu ilikuwa ni kitu gani?.
Kama ulivyosema mwanzoni bora kwanza tuifahamu mikakati aliyoiweka kisha tunaweza weka hoja zetu kwa kunukuu mikakati hiyo.
Hadi sasa hivi mikataba ama niseme mikakati yote inayohusu madini, Utalii na viwanda tumeona hazina faida kwa taifa letu na yeye mwenyewe kesha kubali mapungufu ya mchango wa vitu hivyo ktk pato la taifa. Then ikiwa kesha fahamu ni kitu gani kakifanya kuhakikisha malipo zaidi ktk mali hizo?... NOTHING! sii ajira wala uzalishaji isipokuwa tunapewa hesabu ya mchango wa vitu hivyo ktk GDP ya nchi.
KadaMpinzani,
Tunachodanganywa sisi wananchi ni hizi hesabu za kupanda kwa GDP ambazo hazijengi msingi botra kwa maendeleo ya nchi yetu.
Ikiwa pato la taifa ni billioni 10, mchango wa madini uwe asilimia 40, Utalii 20, Kilimo 20, viwanda na services asilimia iliyobaki bado hesabu nzima haitakuwa tofauti kwa jumla ktk mahesabu kama tutaambiwa Kilimo kinachangia asilimia 50, madini 20, Utalii 10, viwanda na services kilichobaki.
Kimba lipo ktk hiyo asilimia 5 ama 6 inayopanda toka Billioni 10 kisha vitu kama madini ni vitu vinavyokwisha! tunachoachiwa ni mashimo matupu tofauti na kama Kilimo kikichukua nafasi kubwa zaidi, hapa kidogo mtu unaweza kuwa na hope kwa miaka ijayo!
Pia tatizo kubwa la uchumi wetu sio kupanda kwa asilimia ya GDP isipokuwa ni mchango mzima wa hizo sector ktk maendeleo yetu. Tunakatiwa ngapi? hakuna anayefahamu kwa uhakika!..na tumeshindwa kuona Ufisadi unaotendeka nchini kwa sababu tumekoma kufikiri nje ya sanduku la CCM!
Ebu tazama somo dogo sana, naomba kurekebishwa kama nimekosea!
Mauzo ya dhahabu sasa hivi yamepanda kishenzi lakini kodi tunazopokea ni punje ya ongezeko la bei yake. Tulipoweka mikataba yetu ya dhahabu hasa miaka ya 2000 hadi 2002 dhahabu ilikuwa ikiuzwa kwa dollar 200 kwa ounce moja leo hii dhahabu hiyo hiyo inauzwa mara tatu ya bei ile - at 600 Usd!.. sasa piga mahesabu ikiwa kodi yetu ilikuwa tukipokea asilimia 5 tu ktk mauzo ya Usd 200 per ounce leo hii tunapokea bado asilimia ile ile 5 ktk mauzo ya Usd 600 kwa ounce. je, inakuwaje ongezeko la pato la taifa liwe asilimia 6 kwa mwaka hali hadithi hiyo utaikuta ktk Utalii, viwanda na kadhalika kote bei za bidhaa imeongezeka mara 3 ktk miaka 5 iliyopita.
Je, sii kweli asilimia ya pato la taifa ktk kodi zetu nayo inatakiwa iongezeke kwa uchache mara 3?... kumbuka pia mbali na kupanda kwa bei za bidhaa zetu nje kila mwaka kumekuwa na ongezeko la Productivity ktk sectors zote. Uchimbaji wa madini umeongezeka, Watalii na viwanda vimeongezeka kila mwaka lakini bado pato la taifa limekuwa likijikongoja kwa asilimia ndogo sana... How come?
Hakuna ukweli ktk jambo hili unless Government inataka kutuambia kwamba asilimia ya kodi zetu imepunguzwa sana tofauti na miaka ya 2000 kwa hiyo ime affect moja kwa moja pato la taifa.
Nje ya hapo tunaibiwa na rais wetu JK hafahamu kinachoendelea na kama anafahamu basi yeye ni mmoja kati ya mafisadi hao.