Kwanini Watanzania wengi hawafanikiwi kutokana na kazi zao?

Kwanini Watanzania wengi hawafanikiwi kutokana na kazi zao?

Sasa ndiyo uelewe kwanini Elon Musk alihamisha mitaji yake toka Afrika Kusini ambayo iko kwenye bara tajiri na rasilimaliwatu rahisi kwenda US na Canada ambako siyo rahisi kukwepa kodi za serikali na pia ambako kuna rasilimaliwatu ghali.
US & CA zinatoa equal chances kwa mtu yoyote yule kufanikiwa endapo atajituma na kufuata sheria.

Nimeshuhudia watu wamekuja kwa green card tu na ujuzi wa kawaida ila leo hii wako mbali watu walirudi darasani taratibu na wako mbali sana.

Musk pengine aliachana na mambo ya Africa sababu Africa ikitokea mtu na mgogoro naye na anakuzidi pesa mahakamani humshindi.

Africa wengi hawajielewi , hawajui ipi ni haki ipi ni hisani.

Africa unaweza kufanikiwa kwa kumjua tu mtu akakuunganisha kiujanja ujanja aidha anaweza kuwa tajiri au mwanasiasa anayeogopwa na mahakama na polisi kiufupi Africa sheria zipo kwa masikini tu.

CA & US unaweza kuwa tajiri bila kuassociate na chama kilichopo madarakani , unaweza kupishana nacho kimtazamo na wasikufilisi, leo hii tuliona kina Sabaya walikuwa wanachangisha wafanyabiashara $5000 kudhamini ziara binafsi ya DC kuelezea utekelezaji wa ilani.

Kiufupi Africa kufanikiwa au kutofanikiwa hutegemea na utashi wa wanasiasa waliopo madarakani ndio maaana banana republic ni nyingi.
 
Tatzo la africa utafanya kazi kwa bidii lakini wategemezi ni wengi mno
Yaan afrika wanaofanya kaz ni wachache afu tegemezi ni wengi
Tumepofushwa macho na akili kuamini kwamba wingi wa tegemezi ni kikwazo cha maendeleo. Kwanza hawa hawakwepeki labda uende kuishi Mbinguni.

Wingi wa walaji ni kigezo cha ukuaji kiuchumi. China, India, US, Nigeria nguvu zao za uchumi zinategemea idadi kubwa ya watu.

Hao tegemezi siyo laana ni lulu kwa faida ya maendeleo yako na taifa. Watengenezee programu kabambe maalum ya ku-match consumption na production alafu isimamie vilivyo, utatamani u-rush Kijijini kuongeza tegemezi wengine hata toka ujombani au ukweni.
 
Dr. John C. Maxwell ni Mwalimu mashuhuri wa uongozi duniani. Kabla ya kufika barani Afrika, aliamini yafuatayo kuhusu mafanikio, kwamba:

1. Mafanikio yanatokana na kufanya kazi kwa bidii.

2. Wamarekani wanaongoza kwa kufanya kazi kwa bidii.

Lakini baada ya kufika Afrika, alibadilisha mtazamo. Kwa mara ya kwanza maishani mwake alishuhudia watu wanaofanya kazi sana lakini bado hawana maendeleo.

Sijui "case study" yake ilikuwa nchi gani Afrika, lakini maadam ni Afrika, na Tanzania inahusika, na ni kweli kuwa kuna Watanzania wengi wanaofanya kazi kwa bidii lakini wangali wana hali ngumu kiuchumi.

Kwanini iko hivyo?
Msuli tembo matokeo sungura
 
Yanini nieleze kwa kirefu kitu ambacho tayari umekieleza kwa kirefu tena kwa usahihi kabisa?

Nimetoa tu summary ya maelezo yako ambayo kwangu nayaona upo sahihi kwa asilimia 100
Mkuu actually nilikua natoa complement.

Halafu umeona hiki kilichotokea cha mimi kuandika sana wewe ukaandika kwa uchache. Bosi ataona haya maandishi mengi ndiyo kazi imefanyika haswa.

Wakati maandishi kidogo yameokoa muda na kuleta ujumbe ule ule
 
Sahihi pia, ni vigumu kufanya maendeleo kama mtu hafanyi saving.
Dhana ya Saving imebaki kuwa ya kundi la maskini tu. Matajiri wakubwa wamefuta dhana ya Saving wamebakisha dhana ya Investment.

Yaani income yao wanaigawa mara 2 tu: Expenditure na Investment.

Maskini wanagawa income mara 3: Expenditure, Saving na Investment.

Matajiri wanaamini saving is keeping money idle and idle money creates poverty.

Money must constantly circulate in the economy through investment.
 
US & CA zinatoa equal chances kwa mtu yoyote yule kufanikiwa endapo atajituma na kufuata sheria.

Musk pengine aliachana na mambo ya Africa sababu Africa ikitokea mtu na mgogoro naye na anakuzidi pesa mahakamani humshindi.

Africa wengi hawajielewi , hawajui ipi ni haki ipi ni hisani.

Africa unaweza kufanikiwa kwa kumjua tu mtu akakuunganisha kiujanja ujanja aidha anaweza kuwz tajiri au mwanasiasa.

CA & US unaweza kuwa tajiri bila kuassociate na chama kilichopo madarakani , unaweza kupishana nacho kimtazamo na wasikufilisi, leo hii tuliona kina Sabaya walikuwa wanachangisha wafanyabiashara $5000 kudhamini ziara binafsi ya DC kuelezea utekelezaji wa ilani.

Kiufupi Africa kufanikiwa au kutofanikiwa hutegemea na utashi wa wanasiasa waliopo madarakani ndio maaana banana republic ni nyingi.
Elon Musk kila siku anamshambulia Biden na chama cha Democrats ila kampuni zake za SpaceX zinakula tenda za NASA, Starlink wanakula tenda za Pentagon na Tesla inakula ruzuku za serikali pia. Hii ni miujiza sehemu kubwa ya Africa, haitokei.
 
Dhana ya Saving imebaki kuwa ya kundi la maskini tu. Matajiri wakubwa wamefuta dhana ya Saving wamebakisha dhana ya Investment.

Yaani income yao wanaigawa mara 2 tu: Expenditure na Investment.

Maskini wanagawa income mara 3: Expenditure, Saving na Investment.

Matajiri wanaamini saving is keeping money idle and idle money creates poverty.

Money must constantly circulate in the economy through investment.
Huwezi kufanya investments kama hufanyi saving.
 
Dhana ya Saving imebaki kuwa ya kundi la maskini tu. Matajiri wakubwa wamefuta dhana ya Saving wamebakisha dhana ya Investment.

Yaani income yao wanaigawa mara 2 tu: Expenditure na Investment.

Maskini wanagawa income mara 3: Expenditure, Saving na Investment.

Matajiri wanaamini saving is keeping money idle and idle money creates poverty.

Money must constantly circulate in the economy through investment.
Ni sawa, lakini usiache kusave for rainy days

Wekeza ni mhimu sana lakini lazima uweke hela keshi sehemu fulani kwa matukio ya dharura na uwekezaji zaidi
 
Tumepofushwa macho na akili kuamini kwamba wingi wa tegemezi ni kikwazo cha maendeleo. Kwanza hawa hawakwepeki labda uende kuishi Mbinguni.

Wingi wa walaji ni kigezo cha ukuaji kiuchumi. China, India, US, Nigeria nguvu zao za uchumi zinategemea idadi kubwa ya watu.

Hao tegemezi siyo laana ni lulu kwa faida ya maendeleo yako na taifa. Watengenezee programu kabambe maalum ya ku-match consumption na production alafu isimamie vilivyo, utatamani u-rush Kijijini kuongeza tegemezi wengine hata toka ujombani au ukweni.
SAwa nimekuelewa,lakin watu wengi wapo na tegemezi wasio zalisha

Na ukitaka tegemezi wazalishe inabid uwe bandidu zaidi ya magufuri maana kizazi cha Sasa ni wavivu na hawataki kutumwa na ni wezi pia(yaan unaweza lea watu lakin wakawa tena wanakuibia vitu hata chakula)
 
Huwezi kufanya investments kama hufanyi saving.
Mkuu Yoda.

Ukifanya saving (tena iwe kubwa kuliko expenditure) masoko ya mitaji (capital markets) zitafanya kazi gani?

Saving ikiwa kubwa huna sababu ya kukopa kwenye capital markets. Mikopo ndiyo inayofilisi matajiri duniani.

Usipokopa kwenye capital markets zitalazimika kutoweka.
 
SAwa nimekuelewa,lakin watu wengi wapo na tegemezi wasio zalisha

Na ukitaka tegemezi wazalishe inabid uwe bandidu zaidi ya magufuri maana kizazi cha Sasa ni wavivu na hawataki kutumwa na ni wezi pia(yaan unaweza lea watu lakin wakawa tena wanakuibia vitu hata chakula)
[emoji16][emoji16][emoji16]
 
SAwa nimekuelewa,lakin watu wengi wapo na tegemezi wasio zalisha

Na ukitaka tegemezi wazalishe inabid uwe bandidu zaidi ya magufuri maana kizazi cha Sasa ni wavivu na hawataki kutumwa na ni wezi pia(yaan unaweza lea watu lakin wakawa tena wanakuibia vitu hata chakula)
[emoji16][emoji16][emoji16] unajuwa mkuu dhana ya tegemezi ni tafsiri na mtizamo tu. Hata wazungu wana tegemezi kutuzidi.

Hawako nao ndani ya miji yao lakini wako nao huku Afrika (yaani sisi Waafrika).

Hata siku 1 wazungu hawajatuacha kwamba tumekuwa mzigo kwao.

Hata siku 1 wazungu hawajakosa kuendelea kwa sababu tumewaelemea kupitia utegemezi wetu kwao.

Wanachofanya wazungu ni kuhakikisha kuwa hatutafuni jasho lao bure tu kupitia utegemezi wetu kwao bali tunawafidia kwa faida ya ziada jasho lao.

Weka program mezani, kaa nao muichakate, waanze kuwa wa faida kwako.
 
Una
[emoji16][emoji16][emoji16] unajuwa mkuu dhana ya tegemezi ni tafsiri na mtizamo tu. Hata wazungu wana tegemezi kutuzidi.

Hawako nao ndani ya miji yao lakini wako nao huku Afrika (yaani sisi Waafrika).

Hata siku 1 wazungu hawajatuacha kwamba tumekuwa mzigo kwao.

Hata siku 1 wazungu hawajakosa kuendelea kwa sababu tumewaelemea kupitia utegemezi wetu kwao.

Wanachofanya wazungu ni kuhakikisha kuwa hatutafuni jasho lao bure tu kupitia utegemezi wetu kwao bali tunawafidia kwa faida ya ziada jasho lao.

Weka program mezani, kaa nao muichakate, waanze kuwa wa faida kwako.
Unapokuwa unategemewa lazima upige hatua Sana tatizo unajikuta unategemewa na watu ambao huwezi kuwafanyia win win situation kama wazungu.


Personally ukiwa MTU unayepambania tumbo lako tu huwezi kupiga hatua. hii mbinu ya kujua nyuma Una watu wanakutegemea huwa inamfanya MTU kuwa smarter and wiser towards the success
 
Elon Musk kila siku anamshambulia Biden na chama cha Democrats ila kampuni zake za SpaceX zinakula tenda za NASA, Starlink wanakula tenda za Pentagon na Tesla inakula ruzuku za serikali pia. Hii ni miujiza sehemu kubwa ya Africa, haitokei.
Africa achilia mbali kukosoa serikali.

Mwenge umetengewa bajeti ila ajabu bado watu wanachangishwa pesa zinapokwenda haijulikani hata tija ya huo mwenge haijulikani

Mtu akigoma kuchangia mwenge 50,000 kwa kigezo kuwa hajawiwa kufanya hivyo anaweza kufilisiwa biashara ya milioni 200 .
 
Africa achilia mbali kumkosoa serikali.

Mwenge umetengewa bajeti ila ajabu bado watu wanachangishwa pesa zinapokwenda haijulikani.

Mtu akigoma kuchangia mwenge 50,000 kwa kigezo kuwa hajawiwa kufanya hivyo anaweza kufilisiwa biashara ya milioni 200 .
Terrible!
 
Tufanyeje mkuu?
Mifumo yetu ni mibovu. Hasa Tanzania ukianza tu biashara,na ukifanya kwa halali kabisa,utakutana na vibali zaidi ya 15 ulipie serikalini. Ni kama waliopo kwenye madaraka hawataki wengine wainuke. Hata elimu tunayopewa ni uoga uoga tu ni elimu ya kuishia humu hunu. Angalau Nigeria wanawapa elimu ya kuvuka nje ya mipaka yao,ndio maana unakuta Wanigeria wako kibao ulaya wanapiga kazi,na wamefanikiwa sana wananchi wa Nigeria na wanarudi kuijenga Nigeria. Ona hata Kenya sasa,majengo yote yale marefu pale Nairobi yanajengwa na wananchi walioko ng'ambo wanapiga kazi.

Mimi huwa nawaambia mara nyingi vijana. Unapoendelea kusoma pambana kutafuta kila njia ya kwenda kupiga kazi ulaya. Hasa Canada na South Korea,hata ulaya poa,USA sawa.
.Wasikudanganye wanaosema kule kugumu. Hao ni wake wakifika kule wanataka kuiga wenyeji kufanya kazi za ofisini tu.
Ukienda kule ukaachana na makundi, ukafanya juhudi kama umetumwa na kijiji huku,miaka mitano tu utarudi huku na B kadhaa ambazo kwa huku ungefanya kazi maisha yako yote usiiguse hata robo ya hiyo hela.

Pamoja na kwamba nina 40+ bado natamani nikipata chance ya huko,nikapige kazi miaka mitano tu. Nirudi nikiwa sawa.
 
Back
Top Bottom