Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Kwanini watoto wa Mzee Mchonga hawana nyadhifa kubwa Nchini?

Kuna jambo halipo sawa kuhusu watoto wa Mwalimu manake hata wale waliowahi kupata kuwatumikia wananchi hawakuonesha consistence yoyote. Na kuhusu Hussein Mwinyi, CV yake inasema tofauti na unachosema wewe. Kwa bahati mbaya sifahamu taaluma ya afya inavyoendeshwa endeshwa lakini CV ya Hussein inaonesha badala ya kumaliza MD, amefanya kazi Muhimbili kama Registral na MD, Kaiuruki kama Specialist na Lecturer. CV yake inaonesha amepata nafasi ya kwanza ya uteuzi miaka 7 baada ya kuwa ameshachukua MD (awamu ya Mkapa).

Nisichofahamu ni kuona muda huo ambao ni takribani miaka 9 pia alikuwa anasoma Masters na PhD UK. Sasa kama udaktari na wenyewe unaweza kusoma bila coursework, hapo ndo sina uhakika. Sasa kama unaweza kusoma bila kuingia darasani (hususani masters) sioni kubebwa kwa Hussein kunaingiaje ingiaje hapo hasa ukizingatia wakati anachukua uteuzi kwa mara kwanza, alishakuwa mbunge. CV inaonesha amemaliza MD 1991, wakati ubunge na uteuzi ni mwaka 2000.
CV unayosoma ni ya kupindapishapindisha. Aliteuliwa na Mkapa kama Waziri mdogo mwaka 1995 akiwa ama bado mwanafunzi au la; hiyo ya kufanya kazi Muhimbili au Kairuki ni vitu vya pembeni labda katika nia ya kupika CV lakini jamaa amekuwa Waziri tangu 1995; aliteuliwa kipindi kimoja na Magufuli.
 
Pamoja na yote hayo, tabia binafsi za watoto wale si tabia njema
Mwalimu "aliwatupa" mwenyewe watoto wake. Kuna siku Madaraka alikuwa anahojiwa kwenye TV -TBC, alidai kuwa alienda kusoma nje ya nchi kwa msaada wa jamaa mmoja, (Mzee Dossa) baba yake akiwa ni Rais

Akaulizwa alichokosa baada ya baba yake kufa, alidai, sana sana ushauri, na ile kukosa baba. Sio amekwama kifedha angeweza kumtegemea kuwa angepata kwake

Pia, mwangalie Makongoro. Alikuwa mwanajeshi. Wenzie alioanza naye wakawa wanapanda vyeo, yeye aliishia vya chini. Wengi wa watoto wa marais, wana nafasi kubwa kupata vyeo vikubwa jeshini. Kabila mtoto, miezi sita tu huko Arusha, akaruka na U - mejajenerali!

Mwangalie mtoto wa Mseven, Kagame nk.
 
Nyerere alikuwa mjanja ila hakupenda watoto wake wawe kama yeye.

Najua sijaeleweka ila nitarudi...
Hivi sera ya ujamaa haiwezi kuwa sehemu ya kumfanya mtu awe mtizamo fulani juu ya familia na jamii?

Sasa kipi ambacho wanawe waweza kufanya ili kuvaa uhusika wa kisiasa?
 
Kwa ulevi wa Makongoro unampa cheo gani ambacho atakimudu? Vyeo hawapati kutokana na familia ila na uwezo pia
Wanasiasa na viongozi wengi duniani ni walevi sana wa Pombe na wanawake!

Tatizo ni Chama cha mapinduzi kuwatenga familia ya Baba wa Taifa na kuwachekea mdomoni ila mioyoni mwao hawapo nao kabisa.
Hivi Makongoro hana uwezo kweli wa kuwa hata mbunge wa kuteuliwa ?
Kwa nini Watoto wa waasisi wengine wanabebwa mpaka wake zao wanateuliwa badala ya kukaa nyumbani wawalee wastaafu wetu?

Makongoro ni msema kweli hapendi unafiki ndio maana wanamkwepa. Sio muoga na anajiamini? Afrika watu kama hao hawapendwi sana.
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Unataka wapenye ili iweje??
 
Tusidanganyane. Makongoro ameshawahi kufanya siasa lakini zikamshinda. Kuna binti mwingine wa Mwalimu alishawahi kuteuliwa ubunge lakini haku-shine.
Baada ya kushuhudia madhila yatokanayo na siasa na unafiki wake ndo maana walishindwa.Makongoro alipata kuwa mbunge wa Arusha mjini kupitia Nccr Mageuzi.Wakati huo baba yake bado yupo, ukipata jibu kwanini bb nccr na siyo ccm utakubaliana na mimi
 
Mtu mwenye akili timamu hawezi ruhusu wanae kwenda ikulu.Ikulu ni mzigo,ni lawama,ni ufungwa,hakina kitu chenye thamani maishani Kama kuwa huru
I salute.Na anatakiwa mtu anayesononeshwa na matatizo ya watu kama Lissu siyo yule apendaye kusifiwa
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Hili litamtokea na mzee
 
Wanabodi, Salaam!
Kwa wabobezi wa saikolojia na sosholojia naombeni mniambie kwa nini tangu tupate Uhuru kisha kuungana Zanzibar na Tanganyika familia za Mwinyi na Karume tushapata marais mara mbili (Ally Hassan Mwinyi, Hussein Ally Hassan Mwinyi na Abeid Karume na mwanaye Aman Abeid Karume

Kwa familia ya Mwl Nyerere tangu ang'atuke nadhani mwaka 1985 hadi leo hakuna mtoto hata mmoja aliyeweza hata kufurukuta na kuingia kwenye tatu bora ya wagombea urais nchini - hata Madaraka Nyerere juzi tu kura za maoni kwa nafasi ya ubunge zilimtupa mbali kisha kamati kuu ya CCM haikurudisha jina lake.

Sasa, hii hali ya watoto wa mwasisi wa taifa hili kutopenya kwenye vinyanganyiro vya nafasi za uongozi zinatokana na nini?
Vipi familia yenu nyie hamtaki uRais?
 
Watoto wa Mwalimu Nyerere hawakuandaliwa vyema kwa "kazi kubwa" ! Mwalimu alikuwa busy sana na mambo ya Uhuru na Ukombozi wa Afrika!

Katika kufeli kwa Watoto wa Mwalimu Nyerere ,Mama Maria anaomchango mkubwa sana!
Watoto wengi uaribika kimalezi kama mama ni legelege na si mentor mzuri.

Pia waliomzunguka Mwalimu Nyerere akina Joseph Butiku walikuwa watu wabinafsi sana na wasiomwambia Mwalimu ukweli kuhusu malezi ya familia yake.

Walibaki kumwabudu na kumsifia tu Mwalimu bila kuangalia succession plan yake.
Familia ya Mwalimu Nyerere imedhihirisha kabisa kuwa " Leaders are made and not born"!

Kwa akili (IQ) aliyokuwa nayo Mwalimu Nyerere hata kama angeoa mwanamke " dull" kiasi gani lazima angezaa " nyoka" walau mmoja au wawili!
Hawapendi rushwa hao jamaa, huwezi kupata madaraka bila kutumia rushwa
 
I think we are missing the point!!
There is nothing wrong na watoto wa Nyerere!
Tatizo ni kwamba wamelelewa katika maadili ya undugu na ujamaa!
Sasa hivi ccm mpya inataka waheshimiwa wanaojimwambafai na nyumba kubwa, magari makubwa na majina makubwa! Usipomwita “Mheshimiwa” unaweza kufukuzwa kazi!
Watoto wa Mwalimu ni watu wa kawaida! Sasa hivi mtu wa kawaida, ndugu, asiyejua wizi hachaguliwi ccm ya sasa!
Lazima mtu aendane na muundo wa sasa- uwe na pesa, uwe mwongo, uwe mbaguzi wa rangi/dini/kabila/ukanda/wa sasa na siyo wa zamani/ usifie uwongo/unyime watu haki, n.k
Hakuna mtoto wa Nyerere nwenye hizo sifa!
They are too true to humanity to belong to this bew ccm!!!!!!!
 
Tukisema Mwl hakuwaandaa sio kweli maana watoto wake wote wana elimu nzuri tu, na hayo ndo maandalizi tosha, Kinachotakiwa ni viongozi Kuwashika mkono, hilo ndo linakosekana, kwani hata hao watoto wa Mwinyi na Karume wana pata support kwa kushikwa mkono, sasa katambi ana elimu gani na uzoefu upi kumshinda Makongoro nyerere? , hata Uhuru Kenyatta alikuwa introduced by the system na Moi baadae Mwai kibaki akamteua kwenye serikali yake kuwa waziri wa fedha na safari yake ikaanza hivyo, kumbuka Mwai na Uhuru ni mtu na mtoto wake.

Usanii wa CCM ndo mtakapo ujua, kwenye shida utawasikia Mwl nyerere alisema hivi , ni wanafiki kuliko watu wote duniani.
 
Watoto wanatengenezwa kuwa watu flan baadae, na watoto wanatakiwa kuwa na shauku ya kufanya vitu flani maishani mwao.
 
Hili litamtokea na mzee
Haliwwzi kumtokea sababu walau yeye ameandaa mazingira mbadala ya uzalishaji - ana nyumba, ni mfugaji kwa hiyo watoto waweza kutumia uwekezaji huo kujijenga

Mwl Nyerere sijui maisha aliyachukuliaje
 
Ngoja nikachimbe dawa,familia ya Mwl siyo ya kuisema tumbo likiwa ovyo.
 
CV unayosoma ni ya kupindapishapindisha. Aliteuliwa na Mkapa kama Waziri mdogo mwaka 1995 akiwa ama bado mwanafunzi au la; hiyo ya kufanya kazi Muhimbili au Kairuki ni vitu vya pembeni labda katika nia ya kupika CV lakini jamaa amekuwa Waziri tangu 1995; aliteuliwa kipindi kimoja na Magufuli.
Mwaka 1995?! Sio kweli!!! Wanaweza kupika elimu yake lakini hawana sababu ya kupika mwaka alioanza kuingia kwenye siasa!!! Hata baada ya kushinda urais Zanzibar, BBC waliandika habari, na walisema wazi kwamba aliingia kwenye siasa mwaka 2000 baada ya kugombea Mkuranga. Nikatumia dakika chache kutafuta source ya ziada, nikakuta habari ya The Citizen ikisema hayo hayo yaliyosemwa na BBC! Au unataka kusema, both BBC na The Citizen awalitoa habari bila kufanya utafiti wakati miaka inayozungumzwa ni juzi tu hapa!!! Au unataka kutuambia hiyo 1995 ubunge ni wenyewe ulikuwa wa kupewa na sio wa kuchaguliwa?! Na kama aligombea na kushinda, huko kubebwa kunatoka wapi? Lakini kwa upande mwingine Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi ana nini special cha kuwafanya marais wote waliomfuata wambebe mtoto wake yeye tu?!
 
Back
Top Bottom