Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

Itakuwa hivyo hivyo,kwanza mshukuri Bei zimeshuka kidogo maana natamani gunia lifike laki Ili nipige hela ila sioni likifika hata hiyo disemba au mwezi wa 2 unless mvua zizingue.
Mkuu Kwa bei za debe la Mahindi kuwa 18,000 manake ukihitaji guni Moja la debe 10 manake hapo unalipia 180,000/- so it's already there.

Mimi na wewe tunaweza kumudu kununua but imagine watu wa kipato Cha Chini?

Kama hali itaendelea kuwa hivi ni hatari Kwa maisha ya watu.
 
Haujamuelewa mleta mada.

Camera ni kisingizio, haiwezekani video zinazorushwa ambazo ni ndefu sana kukosa kuona umati. Kubwa ni kuwa ziara hizo hazisemi kuwa kiongozi leo ana miadi ya kufanya nini kwa manufaa ya wanaotembelewa na pia mguso mkubwa kitaifa.

Lakini ziara ikiwa imekaa kama sherehe, nderemo, vifijo na matamasha bila ujumbe basi hukosa mvuto.

Lazima idara ya Mawasiliano ikulu iseme madhumuni ya ziara siku kibao kabla ya safari na pia kiongozi ajikite katika kutatua au kubainisha mikakati ya kutatua changamoto za wananchi.

Watu hawaangalii video sababu kwanza hawana bando la kutosha kutokana na ughali wa huduma hiyo , pia hata wenyewe nchi wamiliki wa YouTube, FB, Twitter , TIKTOK n.k au vituo vya televisheni hawana mtindo wa kurusha video au ziara live / mubashara ya masaa mawili, matatu au manne kama wafanyavyo waandishi wa habari wa kiTanzania wawe wa Ikulu au vituo binafsi na TV za online mitandao .


Wenzetu hurekodi, halafu wakafanya editing / review kuona ktk tukio zima ni jambo gani la msingi limeongelewa na kurusha kipande hicho.

Suala hili halina cha watu kutaka kuona umati au ulinzi au wasanii walitumbuiza nini ktk ziara ya kiongozi.

Watu wamekinai habari ndefu zilizopitiliza au mapicha picha ambayo hayatawasaidia ktk kukabiliana na ugumu wa maisha walio nao.

Watu wanahamu ya kujua serikali ina mikakati gani kutatua changamoto kibao tena kwa kifupi tu na siyo hotuba ndefu za kupitiliza ambapo pia wamechomekea sala, dua , kampeni ya CCM 2025, ngoma na tamasha hii ni kwa kutaja machache mengi yanayochomekwa ktk ziara ya rais.

 
20220811_172014.jpg
20220811_194809.jpg
20220811_194813.jpg
20220811_194819.jpg
20220811_194822.jpg
20220811_194830.jpg
20220811_194834.jpg
20220811_194843.jpg
20220811_194847.jpg
20220811_194850.jpg
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Hivi kwa nini Mpiga picha nguli Muhidin Issa Michuzi hayupo timu ya Mama ya Habari?

Huyu mzee inabidi arudishwe ni mtu wa picha mzuri sana , alifanya kazi nzuri sana na Mzee kikwete na Marehemu Magu
 
Hii ni taaluma ya watu,
Wenye vigezo hawapewi nafasi...
Wanashindwa afford hata drone ya 1.5M?
Najiuliza
 
Kwa hiyo kumbe na yeye ana affectiwa na maneno ya mitandaoni?
Inner strength yake iko strong kweli?
Unaweza ukaona members katika mitandao ni wachache lakini wanaopita na kusoma hizi comments na threads ni mamilioni!! Kwahiyo mitandao ya kijamii sio ya kubezwa !!
 
Wanajua kazi yao hakuna haja ya kuwaekekeze wakae wapi wakati wa kazi .. Hata kamera zikimwangalia yeye tu tutajua kwamba yuko kuhutubia

Mambo ya umati kuwa wengi sijui wachache ....., , ...
 
Kwani ni ziara ya kampeni anafanya? amekwenda kutekeleza majukumu yake yake hivyo kikubwa ni kusikiliza changamoto na kuzitatua tu. issue ya nyomi haihusu sana
 
Sasa mbona Kuna umati ila kwenye picha za mitandaoni haonyeshi,hiyo ndio concern ya Rais..

Nimefuatilia ziara yote toka Mbeya,Kote huko Rais amepokelewa kwa shangwe na umati mkubwa sana..

Ila pale Makambako ilikuwa noma zaidi.
She needs to get her priorities straight if that's her concern.... Mambo ya wingi na uchache wa Umati awaachie kina Diamond na Harmonize....
 
Waandishi wa habari na taasisi ya urais wanajichulia wenyewe, maana ziara ya rais clip video urefu masaa mawili, matatu mpaka manne sasa nani ataangalia video ndefu kiasi hicho.


Nashauri waandishi wa habari Ikulu, media binafsi na za serikali wafanyie review na kurusha vipande vifupi vyenye mambo ya msingi badala ya kugeuza ziara ya rais video zake kuwa ndefu kama za movie za kihindi au series za televisheni.


Wananchi hawana muda wala hela ya kununua bando la kutazama video za urefu huo.
Upo sahihi kabisa, inabidi wajifunze CGTN kwenye mitandao yao ya kijamii hasa hasa YouTube waangalie ziara za Xi Jinping mfano poverty alleviation in China.
 
Mkuu Kwa bei za debe la Mahindi kuwa 18,000 manake ukihitaji guni Moja la debe 10 manake hapo unalipia 180,000/- so it's already there.

Mimi na wewe tunaweza kumudu kununua but imagine watu wa kipato Cha Chini?

Kama hali itaendelea kuwa hivi ni hatari Kwa maisha ya watu.
Watu wa kipato cha chini waliokimbia kufanya Kazi Vijijini wamejazana huko mjini wanauza maji Hawa wanatakiwa wapate moto Ili wapate akili..

Hata hivyo hao watu wa chini huwa wananunua vyakula vya kila siku kwa kupima hivyo wataimudu hiyo Bei maana hawanunui debe zima ila wanapima kilo moja ,kilo mbili nk.
 
Miaka hiyo ya karne zilizopita 1600-1700 wafalme, malkia na ma Sultani, wasaidizi wao wa jumba la mfalme au malkia walipenda kugeuza ziara za mfano miaka ya 1700s mfalme King Louis XIV wa Ufaransa kuwa siku za mapumziko, shule na shughuli zote zifungwe, mabunda ya fedha kugawiwa kwa makundi ya watu n.k

Zama hizo zimepitwa na wakati, na hivyo kwa vitendo ile salamu yetu-pendwa ya 2022 Jamhuri ya Muungano kazi iendelee, kweli kazi iendelee kwa kutumia muda wetu vizuri badala ya matamasha kumtatiza kiongozi wetu kwa kumrundikia ratiba ya kikazi yenye makandokando ya kuzuia kazi .

King Louis XIV wa Ufaransa aliandalia makandokando mengi ktk ziara zake za miaka 1700s, historia inanukuu.

1660241217718.png
 
Historia inasema Maréchal papa Mobutu wa iliyokuwa Zaire ambayo sasa ni DR Congo alipenda kila alipo au alipoenda azungukwe na umati, bendi, sarakasi, kwaya na kazi zote zisimame kwa siku hiyo aliyokuwa ana tukio au ziara huku chama chake cha Mapinduzi MPR kilihakikisha nchi inasimama kwa attention yote ielekee kwa bwana mkubwa mfalme wa machifu wote wa Zairoise video clip inaonesha hapa chini

 
Mama yeye achape kazi tu. Hata kama watu hawajai ukweli ni kwamba Magufuli alishakufa na hawezi kufufuka. Rais ni Samia!
 
Back
Top Bottom