Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

Historia inasema Maréchal papa Mobutu wa iliyokuwa Zaire ambayo sasa ni DR Congo alipenda kila alipo au alipoenda azungukwe na umati, bendi, sarakasi, kwaya na kazi zote zisimame kwa siku hiyo aliyokuwa ana tukio au ziara huku chama chake cha Mapinduzi MPR kilihakikisha nchi inasimama kwa attention yote ielekee kwa bwana mkubwa mfalme wa machifu wote wa Zairoise video clip inaonesha hapa chini

Huyo jamaa aliyeimba mwanzo anaitwa nani?bado yupo hai?kama unamjua jina nitajie.Anaonekana alikuwa mhamasishaji mzuri sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili si suala la wanawake, marais wote wa Tanzania wameuza sura.

Na kwa kweli, kuuza sura ni sehemu ya kazi ya urais.

Wanasheria wana msemo wao kwamba haki si tu ifanyike, bali pia ionekane kwamba imefanyika.

Kwenye siasa nako ni hivyo hivyo, watu wana haki ya kikatiba ya kujulishwa habari za uongozi wa nchi yao.

Kwa hivyo, kwa upande fulani, rais asiyejali image ni rais asiyejua kazi yake.

Ila, kuna namna ya ku handle image bila ya kufanya habari ya image iwe ina derail mazungumzo.

Samia kashindwa kuweka proportion, inaonekana kuwa anakereka sana na anavyosemwa, na hana kifua cha kupuuzia maneno asiyajibu wakati hapohapo anayafanyia kazi.

Kwenye kujali image ni sawa rais kujali image. Na marais wote wamekuwa so careful kwenye image.
Yeye kaona anahujumiwa ili hali sisi tunapomuuliza maswali mustakabali wa kero zetu anatuuelekeza tukawaambie wa chini yake, kwani sisi hatujawaona hao wa chini yake? Kwaiyo kaona lake halijawekwa sawa ndio anaropoka.Vip kuhusu matatizo yetu? Tunapomueleza afu anayatupa kapuni ww kwa ubongo wako ni sawa?Mbona Magufuli alikua anayatatua hapo kwa papo kama linahusiana na mahakama anampa mtu wa mahakama aliangalie kwa haki.
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Iko hivi, huo umati zaidi ya 70% wanahudhuria kwa vitisho na shuruti,na hao wapiga picha wanajua ni umati wa mchongo. Kwanini wapige picha za kuhadaa umma kwa umati wa kulazimisha?
 
CCM na watendaji wa serikali wanaotayarisha ziara waende wakajifunze kwa makada wa chama cha MPR ya Mobutu waliobakia, jinsi ya kutukuza, kusifu pamoja na kufanya nchi isimame wote wakifuatilia matamasha ya chama tawala

 
Hujuma za waziwazi hizi wako ambao wanaumia kweli juu ya urais wa MH. SAMIA, alipaswa kubadilisha timu yote ya mwendazake mara moja, ndio wanaohujumu kwani hamfahamu katika ziara za namna hii hapo baadae hupunguza UGUMU wa kampeni maana mama anakwenda kila chochoro nyanda za juu kusini huku akifungua miradi mingi kweli tena mizito lakini maredioni hatuoni zile taarifa zilizotufikia wakati huu kama ilivyokuwepo wakati hule.

Hata angetaza hizo ziara kila chombo cha habari hapa duniani, bado watu wameichoka CCM. Magufuli ndio alikuwa bingwa wa media, lakini ndio kiongozi aliyenajisi uchaguzi kuliko kiongozi yoyote yule. CCM haitegemei kura kukaa madarakani, huo ugumu wa kampeni unatoka wapi?
 
Mh Rais mama Samia Alipokelewa kwa shangwe Sana huku mkoani Mbeya Tangia aliposimama katika mji wa Mbalizi, kwa kuwa wananchi wanamkubali Sana na wanamuunga mkono

Kwa hela anazohonga na watu kusombwa kwa malori atakosaje watu? Hilo neno kumkubali sana liondoe. Hakuna mtu anakubali majizi ya kura.
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Kwani huko kampeni zimeanza mpaka mtu kutaka kuwe na nyomi?
 
Historia inasema Maréchal papa Mobutu wa iliyokuwa Zaire ambayo sasa ni DR Congo alipenda kila alipo au alipoenda azungukwe na umati, bendi, sarakasi, kwaya na kazi zote zisimame kwa siku hiyo aliyokuwa ana tukio au ziara huku chama chake cha Mapinduzi MPR kilihakikisha nchi inasimama kwa attention yote ielekee kwa bwana mkubwa mfalme wa machifu wote wa Zairoise video clip inaonesha hapa chini


Hapo wanamuombea aishi milele 🤣
 
Chuki mchukieni HAKI YAKE MPENI!
Hakika Hali yake ya kumpongeza na kumtia moyo Tunampatia mh RAIS wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa afanyazo kututumikia wananchi wake, sisi vijana tunaendelea kumuunga mkono Rais wetu

Tunasema mama aendelee kuchapa kazi bila kuchoka Wala kukatishwa Tamaa na mtu yoyote yule, Tulio bega kwa bega na Rais Ni wengi kuliko wachachee wasiofurahia kazi nzuri afanyazo,maana walitegemea waone akishindwa lakini kwa mshangao wao wanashangaa namna anavyo endelea vizuri na kupata uungwaji mkono mkubwa toka kwa wananchi
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Ngoja kwanza nipige nduru!
 
Huyo jamaa aliyeimba mwanzo anaitwa nani?bado yupo hai?kama unamjua jina nitajie.Anaonekana alikuwa mhamasishaji mzuri sana

Sent using Jamii Forums mobile app

Ngoja tupite mitaa ya Château Rouge jijini Paris France au ikishindikana baadaye nifike Matonge Brussels Belgie lazima tutapa historia kamili ya huyu John Komba wa MPR ya Mobutu.

Diaspora ya Jamaa zetu hawa wa DR Congo wanamkubali sana Mobutu na vitu vyake alivyofanya ktk siasa za Congo.
 
Rais Samia Suluhu amedai kwamba, Waandishi wa habari wanaandika kwamba kwenye ziara yake inayofanyika Nyanda za Juu Kusini watu wanaohudhuria ni wachache.

Jambo analoliona kama ni Upotoshaji , Kwake yeye anaamini Umati ni mkubwa wa kutisha, amewaomba waandishi waandike uhalisia, huku akiwataka Wapiga picha wapande juu ili wapige vizuri picha za umati unaohudhuria mikutano yake.

Kwa kadri ya kumbukumbu zangu hili ni jambo Jipya tangu niifahamu Tanzania , sijawahi kusikia Rais wa Tanzania akilalamikia kuhusu taarifa za ziara zake kupotoshwa na wanahabari na wapiga picha.

Hivi Ikulu haina Wapiga picha ambao wanaweza kunogesha.

Ziara ya Rais hata kwa Propaganda za uongo , kama enzi za akina Michuzi?
 
Back
Top Bottom