MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Ukienda Zambia utajuta.. kule ugali ni 24/7Ni chakula kizuri sana,sema ugali mnaouleta pichani sijui mnautoa wapi,hauna mvuto
Ile sio mboga ni chakula cha nguruwe.binafsi hata kabeji huwa najiuliza ni nani alibuni kua ni mboga
We yaelekea ni wa kudeka deka sana,huo ugali kabichi una shida gani chief?Ugali inategemea unakula na mboga gani, ugali na kabichi lazima uukasirikie. Ila ugali maini rosti, ugali nyama choma, ugali maziwa mgando hii napenda na naweza kula muda wowote.
Ukisha ona chakula ambacho kinategemea mboga gani ndio kivutie ujue hakuna kitu hapo,coz hapo kinakua kitamu kwa msaada wa mboga gani,Ugali inategemea unakula na mboga gani, ugali na kabichi lazima uukasirikie. Ila ugali maini rosti, ugali nyama choma, ugali maziwa mgando hii napenda na naweza kula muda wowote.
🤣🤣🤣🤗Hata wewe pia
NAKAZIA HAPAMie nishajiapisha jinsi ugali ulivyonitesa shule hautakuja ukanyage kwangu hata nikiandikiwa na daktari
Ndo maana wengi wenu mmedumaa.Wengi wao wasiopenda ugali ni wazaliwa wa mijini, sie tuliozaliwa kijijini chakula chetu ni ugali.
Kabichi nakula rafiki na ni mboga yangu pendwa ila kama nakula na ugali lazima niweke na mboga nyingine. Mfano samaki, dagaa, nyama nk.We yaelekea ni wa kudeka deka sana,huo ugali kabichi una shida gani chief?
Kuna wengine wanaupasha asubuhi wanaunywea chai😃😃
Wadau habari ya Jioni,
kwani ugali una shida gani, mimi
nilijua ni hapa tu jamiiforum kumbe hata majumbani kwa watu.
Mimi ni mzanaki wa pale Kyabakari mbona kule kwetu tunakula ule ugali wa mtama na tupo fresh tu.
Tena ukila ugali wa mchanganyiko wa udaga na mtama alafu mboga yako ikawa kuku wa kienyeji jogoo ukalipika chuku chuku mbona tunakuwa tupo strong tu, kimwili na kiakili.
Watanzania tuachane na mambo ya kuzungu, Kama unapenda ugali basi dondosha comment yako kwa aina ya ugali unaopikwa kwenye kabila lako.
Nawasilisha;
Unajisikiaje kuandika kuwa mama yako alipewa onyo mbele yako? Umeandika ushuzi mtupu.Nakumbuka kuna kipindi tulikua na beki tatu mvivu kupika akawa anapika ugali mpaka night coz mother alimpa mandate ya kuamua apike nini baba akiwa kasafiri, ilifika stage mzee karudi tukakiamsha beki tatu akafukuzwa na mother akapewa onyo kali na mzee tukatengeza ratiba yetu ya msosi no ugali
Kwani ugali unaandaliwa kwa kutumia nafaka gani?
Wadau habari ya Jioni,
kwani ugali una shida gani, mimi
nilijua ni hapa tu jamiiforum kumbe hata majumbani kwa watu.
Mimi ni mzanaki wa pale Kyabakari mbona kule kwetu tunakula ule ugali wa mtama na tupo fresh tu.
Tena ukila ugali wa mchanganyiko wa udaga na mtama alafu mboga yako ikawa kuku wa kienyeji jogoo ukalipika chuku chuku mbona tunakuwa tupo strong tu, kimwili na kiakili.
Watanzania tuachane na mambo ya kuzungu, Kama unapenda ugali basi dondosha comment yako kwa aina ya ugali unaopikwa kwenye kabila lako.
Nawasilisha;
Kunde au Mbaazi.Kwani ugali unaandaliwa kwa kutumia nafaka gani?