Kweli kuna Wanachadema Hamnazo. Utawezaje kupigania haki bila kuwa na kiongozi mwanaharakati?

Kweli kuna Wanachadema Hamnazo. Utawezaje kupigania haki bila kuwa na kiongozi mwanaharakati?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
KWELI KUNA WANACHADEMA HAMNAZO. UTAWEZAJE KUPIGANIA HAKI BILA KUWA NA KIONGOZI MWANAHARAKATI?

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Kwa kweli Wanachadema wamenishangaza Sana. Uchaguzi huu umeniongezea uelewa kuhusu CHADEMA inawatu wa aina gani.

Hivi mtu anawezaje kupambania HAKI, ukombozi pasipo kuwa mwanaharakati?

Huwezi tenganisha ukombozi na uanaharakati never ever.
Kama kweli CHADEMA ni chama cha ukombozi kwa wananchi, kupigania HAKI na mabadiliko ya taifa letu haiwezekaniki kuepuka uanaharakati.

Upinzani ambao kimsingi unalenga kupigania ukombozi wa haki za watu kama HAKI za kisiasa, HAKI za kujieleza, Katiba mpya, kukomesha mifumo kandamizi; hauwezi kuitwa chama cha maendeleo bila kuwa chama cha uanaharakati.

Huwezi kuipata Demokrasia bila harakati. Huwezi.


Baada ya ukombozi chama ndio hugeuka kuwa chama cha siasa. Kwa sababu kunakuwa na uwanja sawa, HAKI sawa katika nchi.

Lakini CHADEMA hakitaki kiongozi mwanaharakati alafu wakati huohuo ati wanaitisha maandamano ya kudai Katiba, hivi mmelogwa ninyi au?

CHADEMA hakihitaji kiongozi mwanaharakati lakini kila siku kinaimba kinataka tume Huru ya uchaguzi. Hivi ninyi ni nyumbu?

CHADEMA hakihitaji kiongozi mwanaharakati lakini kila siku kinahangaika kupigania HAKI ya kufanya mikutano ya siasa kwa Uhuru kama wafanyavyo ndugu zao ccm. Hivi ninyi ni kenge Maji?

CHADEMA kila mara wanawekwa korokoroni, wanatekwa, na wengine wameuawa, wanapigania HAKI uchunguzi wa Haki ufanyike lakini hayohyo majitu yanakuambia hayataki kiongozi mwanaharakati! Hivi wanafikiri kwa kutumia makamasi au kitu gani?

Unapopigania Jambo lolote ambalo ni HAKI yako wewe tayari ni mwanaharakati.

Ikiwa upo kwenye chama ambacho kinapigania HAKI Fulani lakini hutaki kiongozi mpigania(mwanaharakati). Ujue wewe unaitwa Nyumbu.
Yaani hujielewi, huelewi nini unafanya, huelewi upo wapi.

Naachia maiki. Nawatakia maandalizi Mema ya sikukuu ya Christmas

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Watanzania sio wajinga.
Huwezi jiunga kupigana ukiongozwa na watu wanafiki.

Mbona wakati wa Slaa watu walikuwa wanatoka
Sahihi kabisa.. Sio Slaa tu hata mchungaji Mtikila watu walitoka Sana.. Kifupi CDM wamepoteza mvuto, na kauli zoo haziaminiki tena.
 
Sahihi kabisa.. Sio Slaa tu hata mchungaji Mtikila watu walitoka Sana.. Kifupi CDM wamepoteza mvuto, na kauli zoo haziaminiki tena.
Kwa hiyo ni chama gani ambacho kinawavutia wananchi na kinaweza kuitisha maandamano yakuipinga serikali na watu wakatoka ?
 
Wakati wa Slaa alikuwepo Rais ambaye aliitwa dhaifu...

Alikutana na viongozi shupavu.

Nshakuambia watu hata wawe bilioni Mia kama hawana kiongozi mahiri ni useless.

Lakini watu wakiwa Wachache wakiwa ma kiongozi mzuri, shupavu, shujaa, Jasiri hao watu ni Moto Mkali Sana.

Ndipo ule msemo usemao, mpige mchungaji na Kondoo watatawanyika wenyewe.

Watu ni kiongozi
 
Kwa hiyo ni chama gani ambacho kinawavutia wananchi na kinaweza kuitisha maandamano yakuipinga serikali na watu wakatoka ?

Hatuzungumzii kupinga serikali kwa sababu watu hawawezi kuishi bila serikali.

Tumia NENO watu kuitisha maandamano kudai HAKI Fulani au kupigania HAKI Fulani.
 
Hatuzungumzii kupinga serikali kwa sababu watu hawawezi kuishi bila serikali.

Tumia NENO watu kuitisha maandamano kudai HAKI Fulani au kupigania HAKI Fulani.
Huko Ndio kuipinga serikali , umekupa majina mengi lakini ni kuipinga serikali inapokuwa imenyanganya haki fulani za wananchi🐼
 
Alikutana na viongozi shupavu.

Nshakuambia watu hata wawe bilioni Mia kama hawana kiongozi mahiri ni useless.

Lakini watu wakiwa Wachache wakiwa ma kiongozi mzuri, shupavu, shujaa, Jasiri hao watu ni Moto Mkali Sana.

Ndipo ule msemo usemao, mpige mchungaji na Kondoo watatawanyika wenyewe.

Watu ni kiongozi
Slaa mwenyewe na "ushupavu" wake aliondoka kwa njia zile zile.….mazingira yaliyokuwepo yaliruhusu zaidi maandamano na sio ushupavu wa viongozi.
 
Lissu ni muhimu sana kwa siasa za kipindi hiki. CCM haitakiwi ikutane na viongozi lia lia tena bali walio shupavu, wenye maono mapya na ari mpya ya mabadiriko.
 
Lissu ni muhimu sana kwa siasa za kipindi hiki. CCM haitakiwi ikutane na viongozi lia lia tena bali walio shupavu, wenye maono mapya na ari mpya ya mabadiriko.

Lisu ni mpigania Haki (mwanaharakati) CHADEMA haitaki kuongozwa na mpigania Haki (mwanaharakati)lakini kutwa kuchwa hudai wanaonewa, wanaibiwa Kura, na kufanya maandamano
 
Back
Top Bottom