Kwenye mfumo dume hakuna kitu kinaitwa Ushoga

Kwenye mfumo dume hakuna kitu kinaitwa Ushoga

MUNGU ALIUMBA DUNIA NA KUWEKA MFUMO WAKE, (MFUMO DUME).
SHETANI ANATAWALA DUNIA NA KAWEKA MFUMO WAKE (MFUMO JIKE).

SASA UNAWEZAJE KUPINGA USHOGA WAKATI NDIO MFUMO WA DUNIA?
WANADUNIA NDIO WAMECHAGUA MFUMO HUO KWA KISINGIZIO CHA USAWA WA KIJINSIA,
MFUMO WAO UMESTAWISHA WASALITI (MAARUFU KAMA WANAHARAKATI).
HAWA WAKO PALE KUTETEA MFUMO NA MATOKEO YAKE.

OLE OLE YALE MATUMBO YABEBAYO NA KUACHA URITHI WA LAANA DUNIANI!
 
Sasa ndugu Robert haya mambo wanayazungumzia siku hizi mbili kila nikifungua mada nakuta mambo ya kishoga. Swali langu he ushonga unasababishwa na nini? Je ni tamaa au ni mapungufu ya kimwili?

Kwa sababu nishawahi sikia kuwa wakiwa wafpgo wakiwaishwa hospital kuna therapy au dawa wanapewa kuwarekebisha hii hali. .

Kwanza nadhani serikali ingeangalia pia vichochezi vya haya mambo. Nasikia wanadai P2 na wengine wanafai wanaotumia dawa za uzazi wa mpango na kuzaa bila kusafisha kizazi. Tunasikia mengi Je hakuna tafiti za kisayansi zinazoonyesha inasababishwaje. .

Pili, kuna wanaoamini mambo haya ya laana, kurithi au kulogezana. Je kuna ukweli ndani yake? kama yapo wanatumia njia gani kuepusha na haya mambo. .

Tatu, viongozi wa dini wanahusishwa sana na mambo haya. Je usikute wadhunguuu wandezi wameamua kutumia viongozi wa dini kusambaza mambo haya. Hata masheikh wako kibao wanafanya mambo haya hata huko madrassa. La kufanyia uchunguzi


Naona niishie hapa ingawa nina mengi sana maswali kichwani mwangu. Mungu aepushe. .
wakristo mmeruhusiwa na Papa kuffirana
 
KWENYE MFUMO DUME HAKUNA KITU INAITWA USHOGA.

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani.

Nimeona andiko la Kaka Mshana Jr akionesha masikitiko yake kuhusu janga la ushoga ambalo kwa kiasi linaongezeka hapa nchini. Nikaona nami niseme KITU.

Familia, koo, makabila na mataifa yanayoendekeza mfumo dume hayana kitu kiitwacho Ushoga sijui usagaji na matakataka ya namna hiyo.

Mfume dume sio rafiki kwa mambo ya kijingajinga, mfumo dume ni Katili na hauna huruma na mambo ya hovyohovyo. Baba mwenye mfumo dume kamwe hawezi kuruhusu Mtoto wake awe Shoga dunia ingalipo yeye akiwepo.

Ukifuatilia Kwa umakini Watu wenye ushoga na hapa nazungumzia ushoga wa Aina Mbili;

1. Ushoga wa kitabia
2. Ushoga wa kimatendo

Ukiwafuatilia Watu hao wengi wao wamelelewa aidha na Mama tu, au Wanawake, au wamelelewa kwenye familia zenye mifumo ya Haki Sawa, demokrasia, na mifumo jike.

Kukubali kukaliwa tu na Mwanamke ndani ya nyumba ni ushoga tosha, mwanaume anayekaliwa na Mkewe hana la maana atakalo-offer Kwa Kijana wake wa kiume hasa kwenye upande wa malezi.

Mfumo dume, hautampa nafasi kijana kukaakaa na kuwaza ujinga kwani utampa majukumu yanayotumia nguvu na Akili. Mfumo dume utamjenga mtoto katika mazingira ya kumfanya awe kadiri, shujaa, na mwenye aibu na mambo ya ajabuajabu yasiyohusu jinsia ya kiume.

Kupigwa na adhabu za kiume katika familia yenye mfumo dume ni kitu cha kawaida. Wakati mfumo jike unajikita katika perepete, kudekeza mtoto, kumuadhibu mtoto wa kiume huku unambembeleza.

Mfumo dume unamuandaa kijana kukabiliana na Hali ngumu, na kumkomaza kijana bila kukata tamaa na kuikubali hali yoyote. Lakini mfumo jike unakuta litoto halijaandaliwa kukabiliana na hali ngumu, ni kama dume jike hivi, akikutwa na shida kidogo analia Lia. Inafikia hatua kijana anaambiwa ili apewe kazi basi itabidi atoe 0712.

Kuna mmoja akileta Uzi humu ATI sijui Mwalimu wake anamtaka sijui kimapenzi, sijui anamshika Matako, kesi kama hiyo ingepaswa iripotiwe na Media, redio na Luninga Baada ya kijana huyo kumpa kichapo huyo Mwalimu. Lakini Watoto wakiume wamefundishwa uoga.

ATI anaomba ushauri, mwanaume mzima unaomba ushauri kwenye ishu za kipuuzi. Umekuwa Mwanamke? Tena siku hizi Wanawake wanamaamuzi Hawana muda wa kuomba ushauri.

Mfumo dume unamuandaa kijana awe ndio mzalishaji Mkuu, mlinzi Mkuu, mhudumiaji wa familia, jamii na taifa.

Ushoga ni pamoja na kila saa kuwaza mambo ya urembo na utanashati kama Mwanamke. Unataka uwe na Mvuto kila muda kujizingatia kama toto la kike. Kushinda kwenye Gym wiki nzima ni sehemu ya ushoga WA kitabia. ATI lengo ni kutengeneza Mvuto.

Kiasili mwanaume ni mzuri hata asipojiremba, mwanaume kuwaza kujiremba remba ndio ushoga wenyewe huo hasa ushoga wa kitabia. Unajiremba remba ili iwe nini? Mara Kulitoboa pia, mara hereni, mara kuvaa shanga na mikufu, Mfumo dume hauruhusu mambo kama hayo.

Mlezi Mkuu wa familia ni Baba, mafunzo na Maadili yote yanatoka Kwa Baba. Sasa kama libaba lenyewe Mkewe aanamuendesha unategemea huyo MKE ndio amlee kijana katika misingi Bora ya kuwa mwanaume kamili.

Wanaume ni Wakati wa kushika nafasi zetu vizuri. Ubaba ni ubabe lakini ubabe wenye manufaa Kwa familia na jamii.
Sio unacheka Cheka tuu kama lipumbavu.

Unakuta Mbaba anaona kabisa familia yake inaenda mrama, alafu anakalia kusema Hawa Wanawake ndio wanaharibu Watoto. Wanaharibu Watoto wewe ukiwa wapi? Jukumu lako kama Baba hulijui mpaka Mkeo aharibu Watoto? Kama anaharibu Watoto si umfukuze!

Oooh! Sisi Wakristo hatutoi talaka. Pumbavu! Mwanaume mzima unakubali kuamuliwa Maisha na wanaume wenzako hata kama unaona kabisa Jambo hili halipo Sawa. Kisa dini? Kisa nini?

Mfumo dume hautambui Dini isiyotambua nafasi na maamuzi ya mwanaume pale anapoona mambo hayaendi Sawa. Ni aidha, Mkeo na watoto wafuate unachotaka au Waondoke iwe Kwa hiyari au Kwa nguvu yaani kivyovyote bila kujali Matokeo.

Toto linakuwa Shoga unalichekea, ATI liache! Aisee! Familia zenye mifumo dume Hilo kamwe halitotokea na likitokea maamuzi magumu lazima yafanyike bila kujali Nani atasema nini na nini kitatokea.

Nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Huyu ndio mwanaume aliyeamua liwe na liwe hata Kama atatengwa na Western Countries zinazosupport ushoga. 👏👍
 

Attachments

  • IMG-20230228-WA0015.jpg
    IMG-20230228-WA0015.jpg
    54.7 KB · Views: 4
Dini ya kweli,Ubabe na maadili mema ndio nguzo kuu ya kulea familia imara
 
Style ya woman on top ni mfumo jike ipigww marufuku
 
Mapunga yapo mda sana, kwasasa ni kwamba yanajitangaza waziwazi.
Miaka yetu mtu unatangazwa unatafuna punga kumbe kwako wewe ni mshkaji na mnaonana,mnaenda out kula mnaenda club fresh tu hafanyi hata huo ushogashoga wake.
We unakua labda mgeni sehemu hiyo kumbe watu wote wanamjua.
Inakuja tu mlevi mmoja anaropoka we unampakua yule jamaa ndo unashtuka.
Katika kipindi chote uko naye hujawai hata kuwaza km anashiriki mambo hayo.
Unamwona tu mstaarabu mwenzio ndo mana mnaonana.
Badae unafwatilia yes jamaa ni kweli yuko ribbon.

Noma Sana hiyo
 
Back
Top Bottom