LATRA yaruhusu Mabasi ya Dar - Mtwara yapite Barabara ya Songea, Makambako, Iringa kwa dharura

LATRA yaruhusu Mabasi ya Dar - Mtwara yapite Barabara ya Songea, Makambako, Iringa kwa dharura

31 January 2024​

BARABARA YA IRINGA MLIMA KITONGA HADI MOROGORO​

Mlima Kitonga Ukipanuliwa Barabara ya Njia Nne, Vioo Maalum Kuwekwa | Iringa

View: https://m.youtube.com/watch?v=RDCGFd0WPBM
Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Iringa imeanza kazi ya kuboresha barabara na kupanua mlima Kitonga ili kupata mwanya wa kujenga barabara ya njia nne kwa lengo la kupunguza kero za muda mrefu ikiwemo msongamano wa magari, kudhibiti ajali na kuufanya mlima kitonga upitike kirahisi zaidi.

Akizungumza mbele ya kamati ya siasa CCM mkoa wa Iringa ilipofika kujionea kazi inayoendelea katika barabara ya Mlima Kitonga Januari 31, 2024, Meneja wa TANROADS mkoa wa Iringa Mhandisi Yudas Msangi amesema ujenzi wa mradi huo utagharimu bilioni 6.4 mpaka kukamilika.

Mhandisi Yudas amesema baada ya mlima Kitonga kupanuliwa itajengwa barabara ya kiwango ya njia nne ambayo itakuwa na mifereji mikubwa ya kuongoza maji lakini pia itafungwa vioo maalum kwenye kona zake kwa ajili ya kuongeza uono na kusaidia upishano mzuri wa magari nyakati zote."

Katika mradi huu Shughuli ambazo tumepanga ni kuchoronga mwamba, baada ya hapo barabara itatengenezwa vizuri alafu tutaweka layer tofauti tofauti ambayo ya kwanza inaitwa G15 itakuwa na unene wa milimita 150, itafuata G45 itakuwa na unene wa milimita 150""baada ya hapo tutaweka zege lenye upana wa mita tano kutoka sehemu tuliyochonga, pia itajengwa mifereji kwajili ya kuongoza maji na kuweka vioo maalum" - Amesema Mhandisi Yudas Msangi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa CCM Mkoa wa Iringa Daud Yassin ameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kiasi cha bilioni 6.4 ili kufanikisha ujenzi wa mradi huo.

Yassin amesema Pesa ya kupanua mlima Kitonga na kujenga barabara ya njia nne imetolewa na Rais Samia baada ya kusikia kilio cha wananchi huku akisema mradi huo haukuwamo kwenye mipango na ahadi za CCM lakini serikali imeamua kuutekeleza kutokana na kuwepo kwa ajali, kero na changamoto katika barabara mlima Kitonga


View: https://m.youtube.com/watch?v=mg38KQRvb8U
 
1. Kwa hiyo mabasi kupitia njia zinazopitika inabidi LATRA itoe ruhusa?

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

2. Nchi imejaza misukule kila mahali hadi JF!

3. Si ajabu akashukuriwa mama Samia hapo!

4. Kwamba dereva haoni Wala hawezi kuamua apite wapi?

5. Siku moja LATRA watataka watoe ruhusa hadi za ku overtake, kuwasha gari, kupiga indiketa, kupumua na hata kuj*mba!
Ila we jamaa chenga sana 😂😂😂😂😂
 
Ila we jamaa chenga sana 😂😂😂😂😂

1. Na huo ndiyo ulio ukweli mchungu.

2. LATRA bus lao liko wapi? Si walipe masharti hayo lao?

3. Ya wengine wayanunue wenyewe kuanza kuwapa ati ruhusa ya kupita palipo salama waiona je ndugu?

4. Kwamba hapo ndipo wamewajibika kweli kweli na sisi ndiyo tunakenua sasa?!

5. Kwamba kwa kutuona je vile?

6. Kwa kweli kama taifa kazi ipo. Tutegemee Hadi ruhusa za kuamka au kwenda kuk*joa!

7. Kwa hakika, safari Bado sana!
 
1. Na huo ndiyo ulio ukweli mchungu.

2. LATRA bus lao liko wapi? Si walipe masharti hayo lao?

3. Ya wengine wayanunue wenyewe kuanza kuwapa ati ruhusa ya kupita palipo salama waiona je ndugu?

4. Kwamba hapo ndipo wamewajibika kweli kweli na sisi ndiyo tunakenua sasa?!

5. Kwamba kwa kutuona je vile?

6. Kwa kweli kama taifa kazi ipo. Tutegemee Hadi ruhusa za kuamka au kwenda kuk*joa!

7. Kwa hakika, safari Bado sana!
Na hapa mkuu nataka nipate ruhusa niende dasalam sa sijui wahusika ni kina nani wanipe ruhusa moja kwa zote 😂😂😂😂😂😂
 
1. Na huo ndiyo ulio ukweli mchungu.

2. LATRA bus lao liko wapi? Si walipe masharti hayo lao?

3. Ya wengine wayanunue wenyewe kuanza kuwapa ati ruhusa ya kupita palipo salama waiona je ndugu?

4. Kwamba hapo ndipo wamewajibika kweli kweli na sisi ndiyo tunakenua sasa?!

5. Kwamba kwa kutuona je vile?

6. Kwa kweli kama taifa kazi ipo. Tutegemee Hadi ruhusa za kuamka au kwenda kuk*joa!

7. Kwa hakika, safari Bado sana!
Muwe mnakaa kimya kwenye Mambo ambayo hamna utaalamu nayo.
 
Muwe mnakaa kimya kwenye Mambo ambayo hamna utaalamu nayo.

1. Utalaamu gani mnahitaji kwenye kuona njia ipi inapitika?

2. Kwani hata kimbuga "Hidaya" ilikuwa TMA kukiona na kutabiri?

3. Kwamba si kuwa pamoja nao tulikuwa tumekodoa macho BBC, CNN, na Al Jazeera huko kujua kitatua wapi, lini na athari zake?

4. Kwamba tunakuwa tunanyamaza kwenye mambo mengine? Tusichukuliane poa!

5. Kwa kweli namwelewa sana Shivji:

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

6. Msitutake kuwa misukule, tumewabamba!

7. Hapo #6, utalaamu wa LATRA ni upi na hasa kwenye kutoa ruhusa ya pa kupita wao wakiwa si madereva wala wenye mabasi?!

8. Kwamba wanawashwa pilipili siyo?
 
Unahukumu sana mkuu.
😂😂😂😂😂😂

1. Hapana mkuu.

2. Ni haki yetu kuhoji.

3. Tunachukuliwa poa sana.

4. Ndiyo maana wako bungeni huko, wanalipana posho kwa siku ambazo ni zaidi ya mshahara wa kima cha chini kwa mtu, kwa mwezi.

5. Bila kuwahoji hawa, mdogo mdogo utasubiri ruhusa zao kwenye hadi kuoga, kuzaa, kuoa na hata kula!
 
Hakuna barabara Kati ya liwale - ifakara pia liwale- Nangurukuru haipitiki hapa ndo naona umuhimu wa serikali kutengeneza barabara Kati ya liwale na ifakara
 
Hakuna barabara Kati ya liwale - ifakara pia liwale- Nangurukuru haipitiki hapa ndo naona umuhimu wa serikali kutengeneza barabara Kati ya liwale na ifakara

Ngoja kwanza watoe ruhusa ya pa kupita kwanza. Barabara kutengeneza si kipaumbele. hIzo watatengeneza baadaye.
 
Back
Top Bottom