LATRA yaruhusu Mabasi ya Dar - Mtwara yapite Barabara ya Songea, Makambako, Iringa kwa dharura

LATRA yaruhusu Mabasi ya Dar - Mtwara yapite Barabara ya Songea, Makambako, Iringa kwa dharura

25 January 2024

BARABARA YA SONGEA NJOMBE MAKAMBAKO KUJENGWA UPYA


View: https://m.youtube.com/watch?v=w_W-Mvw4QZY

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali inatarajia kuanza kujenga upya barabara ya Songea – Njombe - Makambako kwa kiwango cha lami kutokana na barabara hiyo kuwa nyembamba na muda wake kuisha.

Waziri Bashungwa amesema hayo Wilayani Ludewa, mkoani Njombe wakati akizungumza na wananchi wa Mlangali katika mkutano wa hadhara ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kufungua mikoa na nchi jirani kwa barabara za lami


View: https://m.youtube.com/watch?v=qjae7T-g68Y


HABARI KWA KINA BARABARA YA SONGEA, NJOMBE HADI MAKAMBAKO
24 January 2024

03c45fe2fe50958b48fcbfb35315219b.jpeg

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali inatarajia kuanza kujenga upya barabara ya Songea – Njombe - Makambako kwa kiwango cha lami kutokana na barabara hiyo kuwa nyembamba na muda wake kuisha.

Bashungwa amesema hayo Wilayani Ludewa, mkoani Njombe wakati akizungumza na wananchi wa Mlangali katika mkutano wa hadhara ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kufungua mikoa na nchi jirani kwa barabara za lami.

Bashungwa amesema hadi kufikia mwezi Machi mwaka huu 2024 Serikali itakuwa imempata Mkandarasi atakayenga upya barabara hiyo ikiwa ni dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufungua mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

“Ukitoka bandari ya Mtwara unakuja kwa lami hadi Songea, na kutoka Songea kuja Njombe mjini kwenda makambako, lami ilijengwa miaka ya 80 imechoka, tayari Mheshimiwa Rais ametupatia fedha na kufika mwezi wa tatu au wa nne 2024 tutakuwa tumepata mkandarasi anakuja kuijenga upya”, amesema Bashungwa.

Bashungwa amewataka wananchi kuendelea kuheshimu Sheria na kutofanya shughuli katika maeneo ya hifadhi ya barabara ili kuondokana na usumbufu pale Serikali inapotumia Sheria zilizowekwa kuwaondoa katika maeneo ili kujenga miundombinu ya barabara.
Source : tovuti MOW

Serikali kama ina nia kujenga upya njia hiyo ingepanua angalau njia mbili kila upande ili kupunguza makali ya mabonde, milima na kona kali hasa toka Njombe mpaka Madaba
 
1. Kwa hiyo mabasi kupitia njia zinazopitika inabidi LATRA itoe ruhusa?

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

2. Nchi imejaza misukule kila mahali hadi JF!

3. Si ajabu akashukuriwa mama Samia hapo!

4. Kwamba dereva haoni Wala hawezi kuamua apite wapi?

5. Siku moja LATRA watataka watoe ruhusa hadi za ku overtake, kuwasha gari, kupiga indiketa, kupumua na hata kuj*mba!
Mabasi yana Bima inayomlinda mmiliki wa gari, abiria na mizigo yake.
Bima inatambua njia rasmi zilizoidhinishwa na LATRA.

Bima haitambui njia za kuchochora (diversion) ambazo zitamfanya dereva awahi kufika au kuchelewa kwa utashi wake.

LATRA ipo kisheria kusimamia na kutoa miongozo ya njia sahihi za kupita ili kuepuka kurundika magari mengi kwenye njia moja.

Hivyo kwa dharula kama hii ya Kilwa LATRA walitakiwa watoe mwongozo.
Bila mwongozo wa LATRA polisi watakamata magari yanayofanya mchepuko wa aina hiyo ili kumlinda abiria na mali zake.
Kila kitu kipo kisheria.
 
Kuna ongezeko la km 1000 zaidi, ni safari ndefu mno kama hauna dharura ni vizuri kusubiri tuu,
 
Kama huna ulazima wa kusafiri bora kukaa tu, kwa nini?

1. Madereva hawana uzoefu na route.
2. Ni risky.

Ikibidi sana usafiri, vunja safari mwenyewe usitumie gari moja kwenye route yote hiyo.
 
1. Umeelewa tofauti ya ulichoandika na nilichoandika hapo #4?

2. Kwamba kujua unakoelekea hata kama njia si salama mpaka wenye akili ya kulijua hilo wakwamulie.

3. Angalia tena hoja yako, Kulikoni kulazimisha mabasi kwenda kusiko na abiria au njia isiyokuwapo?

4. Hapo #3, wadhani Kuna njia yenye abiria na kupitika itakosa abiria?

5. Kulikoni kulazimisha mtakayo kwenye biashara za watu? Myatakayo nyie si mpeleke ya kwenu?

Kwa hiyo unaamini katika watu kufanya biashara bila utaratibu? Kwa sababu tu ni biashara zao?
 
Kama huna ulazima wa kusafiri bora kukaa tu, kwa nini?

1. Madereva hawana uzoefu na route.
2. Ni risky.

Ikibidi sana usafiri, vunja safari mwenyewe usitumie gari moja kwenye route yote hiyo.
Hata Mimi hofu yangu madereva kusinzia njiani.
 
Mabasi yana Bima inayomlinda mmiliki wa gari, abiria na mizigo yake.
Bima inatambua njia rasmi zilizoidhinishwa na LATRA.

Bima haitambui njia za kuchochora (diversion) ambazo zitamfanya dereva awahi kufika au kuchelewa kwa utashi wake.

LATRA ipo kisheria kusimamia na kutoa miongozo ya njia sahihi za kupita ili kuepuka kurundika magari mengi kwenye njia moja.

Hivyo kwa dharula kama hii ya Kilwa LATRA walitakiwa watoe mwongozo.
Bila mwongozo wa LATRA polisi watakamata magari yanayofanya mchepuko wa aina hiyo ili kumlinda abiria na mali zake.
Kila kitu kipo kisheria.

1. Bima ni biashara yenye wateja na supplier.

2. Hapo #1 ni willing buyer and willing seller.

3. Bima kufungamanishwa na njia siyo kutokea mbinguni!

4. Hapo #3, kwani magari madogo ya watu yana fungamanishwa na bima ya njia ipi, wapi?

5. Si kweli kuwa mabasi bima zinafungamanishwa na njia.

6. #5, huwa mnatokea wapi na hizi sifia sifia bila facts?!

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

7. Wapi nani kasema kuchochora ni ujanja? Au kupitia iringa kwenda lindi kwako ni kuchochora?

8. Kulikoni kuwaona wengine ni wajinga ila ninyi?!

9. Bure kabisa!
 
Lipo Somanga Mkuu, madaraja jumla yaliyokatika ni matatu
Watafute sehemu kupitisha barabara ya dharula... Lakini kuzunguka songea kupitia iringa ni safari ndefu mno... Utoke Dar saa 12 asubuhi... Uingie Songea saa 4 Usiku... Kisha uanze kuitafuta mtwara..??
 
Na. 4. Sasa unataka kila mtu ajiamulie njia ya kupita? Pengine nyie ni vijana wadogo, miaka ya nyuma kulikuwa hakuna utaratibu wa njia au route katika jiji la Dar. Daladala hazikuwa na rangi. Walitumia vibao kutambulisha route. Ilikuwa ni shidaa. Maana daladala zilikuwa zikienda route ambayo ina abiria wengi. Na kila daladala ilikuwa na rundo la vibao chini ya kiti cha dereva. Yeye alichokuwa akifanya ni kuangalia abiria wengi wanaelekea wapi. Kisha kuweka kibao hicho. Yaani ilikuwa ni shida na vurugu kubwa.
kupanga route ni jambo lisilo kwepeka ili kulinda haki za mlaji.
Hapo ndio namkumbuka bw Mwaibula, alianzisha kupiga mistari ya rangi tofauti, na maandishi ya Kila ruti ya daladala,
 
Mabasi yana Bima inayomlinda mmiliki wa gari, abiria na mizigo yake.
Bima inatambua njia rasmi zilizoidhinishwa na LATRA.

Bima haitambui njia za kuchochora (diversion) ambazo zitamfanya dereva awahi kufika au kuchelewa kwa utashi wake.

LATRA ipo kisheria kusimamia na kutoa miongozo ya njia sahihi za kupita ili kuepuka kurundika magari mengi kwenye njia moja.

Hivyo kwa dharula kama hii ya Kilwa LATRA walitakiwa watoe mwongozo.
Bila mwongozo wa LATRA polisi watakamata magari yanayofanya mchepuko wa aina hiyo ili kumlinda abiria na mali zake.
Kila kitu kipo kisheria.
N
Watafute sehemu kupitisha barabara ya dharula... Lakini kuzunguka songea kupitia iringa ni safari ndefu mno... Utoke Dar saa 12 asubuhi... Uingie Songea saa 4 Usiku... Kisha uanze kuitafuta mtwara..??
Hivi ndege za ATC haziwezi kupunguza nauli, na zikafanya ruti za kwenda Mtwara na kurudi kipindi hiki cha dharura?
Hizi si zimenunuliwa kwa kodi ya hawa wanyonge wanaotaabika kuzunguka Songea,
Au wakishazipokea kwa shangwe na shuhuli Yao imeisha, Zinabaki kuwa za viongozi,
 
N
Hivi ndege za ATC haziwezi kupunguza nauli, na zikafanya ruti za kwenda Mtwara na kurudi kipindi hiki cha dharura?
Hizi si zimenunuliwa kwa kodi ya hawa wanyonge wanaotaabika kuzunguka Songea,
Au wakishazipokea kwa shangwe na shuhuli Yao imeisha, Zinabaki kuwa za viongozi,
Nimeona leo taarifa, basi zinatoka mtwara kuja Dar via Songea na nauli ni 120k, Atcl hawana route ya Dar _ Mtwara
 
Sijasoma hiyo barua ya LATRA vipi nauli ni Ile Ile au itaongezeka?!
 
Back
Top Bottom