LATRA yaruhusu Mabasi ya Dar - Mtwara yapite Barabara ya Songea, Makambako, Iringa kwa dharura

LATRA yaruhusu Mabasi ya Dar - Mtwara yapite Barabara ya Songea, Makambako, Iringa kwa dharura

Waruhusu wapite njia ya masasi, liwale hadi ifakara/mahenge japo sio rasmi lakini ni fupi kuliko huo mzunguko na kupunguza gharama ya nauli kwa abiria
Mji wa ifakara umezingirwa na maji ya mto lumemo kutokana na mto kufurika
 
25 January 2024

BARABARA YA SONGEA NJOMBE MAKAMBAKO KUJENGWA UPYA


View: https://m.youtube.com/watch?v=w_W-Mvw4QZY

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali inatarajia kuanza kujenga upya barabara ya Songea – Njombe - Makambako kwa kiwango cha lami kutokana na barabara hiyo kuwa nyembamba na muda wake kuisha.

Waziri Bashungwa amesema hayo Wilayani Ludewa, mkoani Njombe wakati akizungumza na wananchi wa Mlangali katika mkutano wa hadhara ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kufungua mikoa na nchi jirani kwa barabara za lami


View: https://m.youtube.com/watch?v=qjae7T-g68Y


HABARI KWA KINA BARABARA YA SONGEA, NJOMBE HADI MAKAMBAKO
24 January 2024

03c45fe2fe50958b48fcbfb35315219b.jpeg

Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ameeleza kuwa Serikali inatarajia kuanza kujenga upya barabara ya Songea – Njombe - Makambako kwa kiwango cha lami kutokana na barabara hiyo kuwa nyembamba na muda wake kuisha.

Bashungwa amesema hayo Wilayani Ludewa, mkoani Njombe wakati akizungumza na wananchi wa Mlangali katika mkutano wa hadhara ambapo pamoja na mambo mengine ameeleza mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kufungua mikoa na nchi jirani kwa barabara za lami.

Bashungwa amesema hadi kufikia mwezi Machi mwaka huu 2024 Serikali itakuwa imempata Mkandarasi atakayenga upya barabara hiyo ikiwa ni dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufungua mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.

“Ukitoka bandari ya Mtwara unakuja kwa lami hadi Songea, na kutoka Songea kuja Njombe mjini kwenda makambako, lami ilijengwa miaka ya 80 imechoka, tayari Mheshimiwa Rais ametupatia fedha na kufika mwezi wa tatu au wa nne 2024 tutakuwa tumepata mkandarasi anakuja kuijenga upya”, amesema Bashungwa.

Bashungwa amewataka wananchi kuendelea kuheshimu Sheria na kutofanya shughuli katika maeneo ya hifadhi ya barabara ili kuondokana na usumbufu pale Serikali inapotumia Sheria zilizowekwa kuwaondoa katika maeneo ili kujenga miundombinu ya barabara.
Source : tovuti MOW

"ikiwa ni dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufungua mikoa ya Nyanda za Juu Kusini"! Sifa isiyostahili, mikoa ya nyanda za juu kusini ilifunguka tangu wakati wa ukoloni kutokana kuwa na mazao mengi ya kila aina.
 
Nchi kubwa hivi acheni uchoyo,wamegeeni wenzenu kidogo
 
Dar / Moro 8h:15mins! Hapo sijaelewa naomba nieleweshwe.
No. Ni Iringa. Angalia kidude chekundu ndio destination.

Niliiforce Google Map inipitishe Iringa Songea Mtwara.

Maana ukiandika Dar to Mtwara inakupitisha Mkuranga huku.
 
Na haya mafuriko nadhani hiyo option itakuwa sio feasible

Liwale pia madaraja yamebebwa
 
1. Kwa hiyo mabasi kupitia njia zinazopitika inabidi LATRA itoe ruhusa?

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

2. Nchi imejaza misukule kila mahali hadi JF!

3. Si ajabu akashukuriwa mama Samia hapo!

4. Kwamba dereva haoni Wala hawezi kuamua apite wapi?

5. Siku moja LATRA watataka watoe ruhusa hadi za ku overtake, kuwasha gari, kupiga indiketa, kupumua na hata kuj*mba!

Na. 4. Sasa unataka kila mtu ajiamulie njia ya kupita? Pengine nyie ni vijana wadogo, miaka ya nyuma kulikuwa hakuna utaratibu wa njia au route katika jiji la Dar. Daladala hazikuwa na rangi. Walitumia vibao kutambulisha route. Ilikuwa ni shidaa. Maana daladala zilikuwa zikienda route ambayo ina abiria wengi. Na kila daladala ilikuwa na rundo la vibao chini ya kiti cha dereva. Yeye alichokuwa akifanya ni kuangalia abiria wengi wanaelekea wapi. Kisha kuweka kibao hicho. Yaani ilikuwa ni shida na vurugu kubwa.
kupanga route ni jambo lisilo kwepeka ili kulinda haki za mlaji.
 
Zamani tulikuwa tunaenda mtwara na meli hasa kipindi cha masika.
Kwanini serikali wasilete meli kubwa kama Ile SANTORINI nakumbuka miaka Ile ya 1995-1999 kulikuwa na meli nyingi Sana zinaenda mtwara
 
MOJA YA MIKOA AMBAYO NAHISI SIO TANZANIA BASI NI MTWARA KWA NAMNA ULIVYO NA MIUNDO MBINU MIBOVU.!!! KUNA VIDARAJA UCHWARA SANA.! NJIA YA HOVYO HOVYO KABISA KUWAI KUTOKEA

KWA HIYO NJIA BORA UPANDE NDEGE TU
 
MOJA YA MIKOA AMBAYO NAHISI SIO TANZANIA BASI NI MTWARA KWA NAMNA ULIVYO NA MIUNDO MBINU MIBOVU.!!! KUNA VIDARAJA UCHWARA SANA.! NJIA YA HOVYO HOVYO KABISA KUWAI KUTOKEA

KWA HIYO NJIA BORA UPANDE NDEGE TU
 

31 January 2024​

BARABARA YA IRINGA MLIMA KITONGA HADI MOROGORO​

Mlima Kitonga Ukipanuliwa Barabara ya Njia Nne, Vioo Maalum Kuwekwa | Iringa

View: https://m.youtube.com/watch?v=RDCGFd0WPBM
Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Iringa imeanza kazi ya kuboresha barabara na kupanua mlima Kitonga ili kupata mwanya wa kujenga barabara ya njia nne kwa lengo la kupunguza kero za muda mrefu ikiwemo msongamano wa magari, kudhibiti ajali na kuufanya mlima kitonga upitike kirahisi zaidi.

Akizungumza mbele ya kamati ya siasa CCM mkoa wa Iringa ilipofika kujionea kazi inayoendelea katika barabara ya Mlima Kitonga Januari 31, 2024, Meneja wa TANROADS mkoa wa Iringa Mhandisi Yudas Msangi amesema ujenzi wa mradi huo utagharimu bilioni 6.4 mpaka kukamilika.

Mhandisi Yudas amesema baada ya mlima Kitonga kupanuliwa itajengwa barabara ya kiwango ya njia nne ambayo itakuwa na mifereji mikubwa ya kuongoza maji lakini pia itafungwa vioo maalum kwenye kona zake kwa ajili ya kuongeza uono na kusaidia upishano mzuri wa magari nyakati zote."

Katika mradi huu Shughuli ambazo tumepanga ni kuchoronga mwamba, baada ya hapo barabara itatengenezwa vizuri alafu tutaweka layer tofauti tofauti ambayo ya kwanza inaitwa G15 itakuwa na unene wa milimita 150, itafuata G45 itakuwa na unene wa milimita 150""baada ya hapo tutaweka zege lenye upana wa mita tano kutoka sehemu tuliyochonga, pia itajengwa mifereji kwajili ya kuongoza maji na kuweka vioo maalum" - Amesema Mhandisi Yudas Msangi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Siasa CCM Mkoa wa Iringa Daud Yassin ameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kiasi cha bilioni 6.4 ili kufanikisha ujenzi wa mradi huo.

Yassin amesema Pesa ya kupanua mlima Kitonga na kujenga barabara ya njia nne imetolewa na Rais Samia baada ya kusikia kilio cha wananchi huku akisema mradi huo haukuwamo kwenye mipango na ahadi za CCM lakini serikali imeamua kuutekeleza kutokana na kuwepo kwa ajali, kero na changamoto katika barabara mlima Kitonga


View: https://m.youtube.com/watch?v=mg38KQRvb8U

Hiyo bajeti iliyotengwa si dhani kama itakidhi hiyo plan inayofanyika hapo. Pia namashaka sana na uwezo wa mkandarasi aliyepewa hiyo kazi.
 
Na. 4. Sasa unataka kila mtu ajiamulie njia ya kupita? Pengine nyie ni vijana wadogo, miaka ya nyuma kulikuwa hakuna utaratibu wa njia au route katika jiji la Dar. Daladala hazikuwa na rangi. Walitumia vibao kutambulisha route. Ilikuwa ni shidaa. Maana daladala zilikuwa zikienda route ambayo ina abiria wengi. Na kila daladala ilikuwa na rundo la vibao chini ya kiti cha dereva. Yeye alichokuwa akifanya ni kuangalia abiria wengi wanaelekea wapi. Kisha kuweka kibao hicho. Yaani ilikuwa ni shida na vurugu kubwa.
kupanga route ni jambo lisilo kwepeka katoka kulinda haki za mlaji.

1. Umeelewa tofauti ya ulichoandika na nilichoandika hapo #4?

2. Kwamba kujua unakoelekea hata kama njia si salama mpaka wenye akili ya kulijua hilo wakwamulie.

3. Angalia tena hoja yako, Kulikoni kulazimisha mabasi kwenda kusiko na abiria au njia isiyokuwapo?

4. Hapo #3, wadhani Kuna njia yenye abiria na kupitika itakosa abiria?

5. Kulikoni kulazimisha mtakayo kwenye biashara za watu? Myatakayo nyie si mpeleke ya kwenu?
 
Back
Top Bottom