Lema: Kuna Vijana walitaka kuiba Mwenge Arusha wakaukosa, nilisikitika sana

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426

Akizungumza kwenye Oparesheni 255 inayoendelea Kanda ya Nyasa, Nabii wa Mungu Godbless Lema, amedai kwamba ni aibu kubwa sana kwa Nchi hii leo kuendelea kukimbiza kibatari kinachowaka kinachoitwa Mwenge wa Uhuru.

Amesema kuna vijana Arusha walipanga kuuiba Mwenge huo ili kuutupa, lengo likiwa kuuondoa Nchini ili kuepusha Laana ya Mungu, Lakini kwa bahati mbaya zoezi hilo lilishindikana, jambo lililomsikitisha sana!

Mytake: Vijana wa Nchi hii hatimaye wameanza kujua anayewaloga, si siku nyingi zoezi hili litafanikiwa
 
Anathibitisha kazi yake ya awali, mja asili haachi asili yake!
 
Labda moja ya siri ipo kwenye hili suala hapa👇
 
Yaani mnatumia milioni 50-70 kukimbiza mwenge Halmashauri kwenda kufungua mradi wa kufyatua matofari, mara mashine ya wazee mara wanakosa mradi wanaenda kwenye uwekezaji binafsi mara unafungua gesti mara bar ni ufwallaaaa......
 
Yeye amewahi kuona wapi mzimu unaibwa?.Ibeni muone kama hamjafa ukoo wenu wote,dadeki!🤣🤣🤣
 
Yeye amewahi kuona wapi mzimu unaibwa?.Ibeni muone kama hamjafa ukoo wenu wote,dadeki!🤣🤣🤣
Ule ni ujinga sana... Ungekuwa unaingia kwenye vikao vya maandalizi ya mwenge katika eneo lako utacheka...kwanza miradi ya kufungua ni ya kutafuta.... Gharama za kukimbiza mwenge ni za hovyo sana.... Sijawahi kuonaga umuhimu wake ....
 
Libarikiwe tumbo lililomzaa Lema
kwa kupanga vijana wakaibe mwenge" bro mbona hujakamilisha sentens nimeona bora nikumalizilid, nb tz tuna vijana wa hovyo like mtoa mada na viongozi wa ajabu like lema, unaibaje mwenge? na ukishaiba ndio mwisho kwamba hawatakimbiza tena,, ndugu zangu chadema kwa mawazo haya nimeamin tupo kwaajil ya ruzuku ya vyama na si uongozi pleas naomben nafasi hapo chadema niwape mikakati ya kukiipindua ccm mana naona hapo hakuna kichwa wote miguu tu tena ya bata, nawahakikishia mkinipa nafas yoyote ndan ya chama mnipe miaka miwili tu ccm naipiga dole la kati pale kati
 
Kweli CHADEMA ina viongozi wahuni wahuni tu wanaopanda majukwaani wakiwa wamelewa.hivi kweli mjumbe wa kamati kuu anaweza kuongea ujinga wa Namna hiyo kweli? Mambo hayo na ujinga huo ndio wa kuongelea jukwaani? Ndio sera za kukipa ushindi chama hizo? Ndio zinazoweza wafanya watu wakaacha vyama vyao wakajiunga na Sacco's ya Mwenye kigoda? Ndio anachohitaji kusikia Bibi wa kijijini anayekuja kwenye mikutano yenu? Ndio maono ya viongozi hayo? Ndio alichojifunza Canada hicho? Ndio utafiti uliofanywa na chama unajuwa ndio wana nyanda za juu kusini wanataka kusikia hicho?

Kwanini mnaendesha chama kihuni kiasi hicho? Kwanini hamtambui kuwa kuna vitu kiongozi mkubwa hapaswi kutamka au kutoa katika ulimi au mdomo wake? Kwanini mnashinda kuwa na viongozi wenye kuchuja maneno na kuwa na staha? Kwanini wote akili zenu zipo kama za mvuta bangi Mdude? Kwanini mnakifanya chama kuwa kama kusanyiko la wahuni ,vibaka,watu waliozibuka akili? Mnakwama wapi? Kwanini hamkui akili na bongo zenu?
 
Tutauiba tu ngoja uje tarime
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…