Lengai Ole Sabaya ashinda rufaa na kuachiwa huru na Mahakama Kuu ya Arusha
Ukiwa ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Bongo wala huwezi kushangazwa na hukumu hii. Na kwa jicho la ndani ukiwa mfuatiliaji mzuri wa siasa za bongo ni kuwa, kuna uwezekano mkubwa wa wahusika kuachiwa kwa makosa mengine yaliyobaki kwa kile kinachoitwa ' Mwendesha mashtaka hana nia ya kuendelea na kesi hizo'.
 
..Sabaya alikiri kwa kinywa chake kwamba alihusika na makosa aliyokuwa akituhumiwa.

..utetezi wake ulikuwa kwamba alitumwa na wakubwa zake.

..Sasa inashangaza Jaji kumkuta mtuhumiwa wa aina hiyo hana hatia.

..Ndio maana nasisitiza ni vizuri tukaisoma hiyo hukumu ili kuelewa msingi wa maamuzi ya Jaji.

Cc Nguruvi3 , Proved, Matola
 
Mbowe alikutwa na kesi ya kujibu kwa tuhuma za ugaidi ambapo DPP kwa huruma yake akaamua kumsamehe.

Otherwise Mbowe alikua anakula kifungo cha miaka sio chini ya 50.
 
Sasa wewe iba mbuzi wa jirani ndio utazijua mahakama za Tanzania.
 
Serikali kwa mara nyingine ijitathmiini katika uwezo wa Idara na Taasisi zake kutayarisha kesi na mashahidi kwani zimefeli hivyo kushindwa ku-i-move Mahakama Kuu kuwa kulikuwa na kesi ya kusikilizwa kwa kutumia mizania ya kisheria.


Je tatizo ni kukosekana wanasheria wa serikali walioiva ? Je mfumo haki jinai (criminal justice system) yaani Polisi, TAKUKURU, DPP na Mahakama za chini zinakosa rasilimali watu wabobevu wa kuchunguza, kuandaa na kusikiliza tuhuma / kesi toka mwanzo wa mchakato mzima wa kutoa haki Au kesi hii ilikuwa kuna shindikizo?



06 May 2022
Arusha, Tanzania
Hukumu ya Jaji Ezedekia Kisanya wa Mahakama Kuu ya Tanzania :


Mahakama Kuu Kanda ya Arusha imemuachia huru aliyekuwa DC wa Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili waliokuwa wamekata rufaa ya kupinga kuhukumiwa miaka 30 kwenda jela kila mmoja kwa sababu mbalimbali kwakuwa Mrufani namba mbili Silvester Nyegu na namba tatu Daniel Mbura hawakupewa haki ya kumhoji Shahidi namba mbili wa Jamhuri na kutokufanya hivyo kunawanyima haki yao msingi.

Jaji Ezedekia Kisanya amesema kulikuwa na mkanganyiko kwenye mwenendo wa usikilizwaji wa kesi hiyo ikiwemo kutofautiana kwa mashahidi na kuufanya ushahidi kuwa batili.

Jaji amesema Lengai Ole Sabaya na wenziwe, watakuwa huru endapo watakuwa hawana kesi nyingine kwenye Mahakama yoyote
Mkuu, Utawala wa Haki Jinai Kwa Ujumla Umejikita Katika Kanuni Kuu Zifuatazo:-

i. Lazima kuwepo na sheria inayoainisha kwa uwazi kwamba matendo flani yanapofanywa na watu kuwa ni jinai.

ii. Sheria hiyo lazima pia ianishe adhabu kwa matendo hayo ambayo ni makosa ya jinai.

iii. Wajibu wa kuthibitisha shitaka dhidi ya mshitakiwa ni wa yule anyelalamika, na kwa Tanzania ni Jamhuri, hivyo upande wa mashitaka unapaswa kuthibitisha shitaka lake dhidi ya mshitakiwa pasipo kuacha shaka.

iv. Mtuhumiwa atachukuliwa kuwa hana hatia mpaka itakapodhibitika hivyo.

v. Mtu yoyote hatapelekwa gerezani pasipo kufikishwa kwanza Mahakamani.

Maeneo yote manne yana matatizo katika msingi wa Haki Jinai Tanzania.
.
Na ndio maana kuna muda niliandika kwamba chain ya Jinai mpaka inafika mahakamani inahusisha vyombo vingi katika kuanzia upande wa Upelelezi wa Kesi mpaka kuunda kesi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
..Sabaya alikiri kwa kinywa chake kwamba alihusika na makosa aliyokuwa akituhumiwa.

..utetezi wake ulikuwa kwamba alitumwa na wakubwa zake.

..Sasa inashangaza Jaji kumkuta mtuhumiwa wa aina hiyo hana hatia.

..Ndio maana nasisitiza ni vizuri tukaisoma hiyo hukumu ili kuelewa msingi wa maamuzi ya Jaji.

Cc Nguruvi3 , Proved, Matola
Na kweli mpk mtu akaomba mahakam imuonee huruma Ni was kuwa Katenda jinai hyo Sasa huyu jaji alitoa sababu gani kumuachia huyu ndugu yangu 7ya
 
huyu dogo kaachiwa kwa kazi maalumu.
Walionewa mjipange mmalizane Naye kitaa Hakuna kumuonea mtu huruma
 
Nimeona ndugu zake wanalia sn.Wamkanye mtoto wao,na wamfunde suala la kuumiza watu na kuwapa vilema.Kwanza akitoka aombe radhi na akome kutafuta vyeo kwa kuumiza watu.

Kama wanafanya mchongo atoke,basi saa hii huku uraiani atakutana na "asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu"
 
Lakini Leo anaenda kuvunja amri ya sita na mkewe nyumbani kwake
Loohh... huna information ndugu. Ana kesi nyingine ya uhujumu uchumi ambayo haina dhamana na inasubiri hukumu tarehe 30 mwezi huu May. Amerudi ndani kusubiri hukumu hiyo. Baada ya hizi za Arusha, kuna kesi zinaandaliwa na TAKUKURU Kilimanjaro.
 
..Sabaya alikiri kwa kinywa chake kwamba alihusika na makosa aliyokuwa akituhumiwa.

..utetezi wake ulikuwa kwamba alitumwa na wakubwa zake.

..Sasa inashangaza Jaji kumkuta mtuhumiwa wa aina hiyo hana hatia.

..Ndio maana nasisitiza ni vizuri tukaisoma hiyo hukumu ili kuelewa msingi wa maamuzi ya Jaji.
Proved, Matola
Mkuu unachosema ni kweli kabisa kwamba watu waangalie hukumu inasema nini, kwa bahati mbaya zama hizi si zile za Mahakama tulizokuwa nazo.

Hakuna shaka yoyote kwamba mahakama zetu zimepoteza credibility na integrity.
CJ aliposimama na kusema hukumu zizingatie mihimili mingine alipigilia msumari wa mwisho.

Confidence na Mahakama zetu imekuwa eroded katika kipindi hiki. Mfumo mzima

Lakini si mahakama tu, DPP naye aliposimama kumkingia kifua Makonda ilieleza jambo

Ni watu wangapi, masikini, viongozi, maarufu au matajiri waliowahi kukingiwa kifua na DPP

Ni kwa mantiki hiyo Sabaya alikiri kushiriki na kutumwa na wakubwa hawezi kuachwa aozoe magereza.

Kuna kundi la vijana waliokuwa na kazi maalum, lina siri nzito sana vifuani mwao.
Mahakama inatumika kama JIKI

Jamani mifumo yetu yote imeoza, ndio maana tunataka katiba mpya kuihuisha.

Mahakama ni mmjoa wa mifumo iliyopoteza imani ya umma
 
Jaji amefanya vizuri,
Haki imetendeka kwani sabaya aliiarifu mahakama kuwa alikuwa anafanya kwa amri ya mteule wake.
 
Tutafika tu. Kuna mmoja enzi za nyerere alimalizana na mbwa akamtia kwenye 109 yake akampeleka polisi akawambia Kuna mbwa kwenye gari
Wakati huo hakukua na 109, alimtia kwenye buti ya Peugeot 504.
 
Wewe mjinga mahakma ni huru kwenu tu! Juzi hapa makengeza kaachiwa mkaanza kushangilia! Punguza wenge mpuzi wewe!
Sishabikii huo upuzi. Hoja ni Bei za mafuta hayupo kiongozi wa kutatua. Tuitoe kafara CCM this time.
 
Ashinde hii na hii ya mwisho wa mwezi Tena?
Sabaya amepewa temporary relief tu Ila makao yake ya kudumu ni jela
 
Back
Top Bottom