Lile kundi linalofurahia utekaji, mauaji, kunywa damu, ukatili, kutofata sheria, bado lipo

Lile kundi linalofurahia utekaji, mauaji, kunywa damu, ukatili, kutofata sheria, bado lipo

Binafsi naona jambo hapa, yaani kujadiliwa mtu ambaye hayupo na anaumiza vichwa vya watu walio hai kuandika nyuzi za kumjadili tena kwa mabaya ilhali replies zinaonyesha kushindwa, basi ni ajizi kubwa.

Yule mzee aliwaweza kweli kweli aseee!.
Alijua kuwakeketa hawa mbwa
Hawatamsahau kwenye maisha yao.
 
Mkuu watu wamekariri we acha tu maana unaweza kujiuliza huyo Ben alikuwa ni nani hasa? Maana matukio ya uhalifu bado yapo hayajawahi kuisha ila watu wamekariri Ben tu.
Ben na Tundu ni ajenda maalumu, sio kwamba wanapendwa sana, Ila ni namna ya kuficha ndugu zao halisi magaidi ya kibiti yaliyoteketezwa na mwamba
 
Binafsi naona jambo hapa, yaani kujadiliwa mtu ambaye hayupo na anaumiza vichwa vya watu walio hai kuandika nyuzi za kumjadili tena kwa mabaya ilhali replies zinaonyesha kushindwa, basi ni ajizi kubwa.

Yule mzee aliwaweza kweli kweli aseee!.
Somo la history kwa asilimia kubwa huwahusu watu walioishatangulia mbele ya haki!
... sisi tulio hai tunasoma history ili TUSIRUDIE MAKOSA!
 
Wameuliwa na dhalimu? Kumbuka hata hao waliouliwa maiti zao zilikuwepo na wamezikwa. Je aki a Ben, Azory nk wamezikwa wapi?
Yeye ben ni wa kwanza kupotea?

Kipi kinachokufanya useme Magufuli ndio aliomua?

Vipi kama alipotea kama walivyouawa wale 7 wa kigoma?
 
Muuaji si amekamatwa ? Au huna taarifa ndugu....Tunahitaji kumfahamu muhusika wa mauaji ya Ben pia
Unataka ufahamu toka kwa nani?

Watu kibao wanauwa na kupotea kimyakimya na kesi zinaisha kimya kimya alafu huyo ben wenu ndio alikuwa nani hapa nchini?
 
At least umetuthibitishia alikuwa anapita kwa kura halali na kwamba alikuwa anapendwa na Watanzania wengi (majority).
 
Tuna kundi kubwa lililosherehekea utekwaji, mauaji, ukatili, kubambika kesi, kunyanyasa watumishi, dhuluma kwa wafanyabiashara, kundi Hilo kubwa ni la JPM.
Masalia bado yapo. Mama Samia anajitahidi kuyadidimiza lakini hayataisha leo.
 
Unataka ufahamu toka kwa nani?

Watu kibao wanauwa na kupotea kimyakimya na kesi zinaisha kimya kimya alafu huyo ben wenu ndio alikuwa nani hapa nchini?
Mleta mada anauliza wako wapi kumbe bado mpo🤣🤣
 
Wewe ndio mjinga hujui kitu ila kuwaza maslahi ya kundi la wanyonyaji wa umma. Umeandika kirefu ila kwa ujinga wako hujaweka chochote kutambua maisha ni mapambano ya kitabaka.
Nchi inaweza kupata maendeleo pale tu tabaka la wengi likiinuka kiuchumi na kudhibiti serikali.
Unalaumu eti wafanyakazi kutoongezwa mshahara kana kwamba fedha inatoka mbinguni. Huoni chochote kuhusu jitihada za kserikali kupata pesa. Serikali inapata hela kwa njia ya kodi. Sasa hao unaosema wamenyanyaswa na jpm kama je ni wafanyabiashara wanaokwepa kodi au watumishi wa serikali wanaofuja fedha ya serikali mishahara unayoona wafanyakazi wangeongezwa ingetoka wapi? Huu ni mfano mmoja tu. Hapo bado hatujszungumzia serikali kutoa huduma muhimu na kujenga miundombinu.
Kwa ufupi ulichoandika ndio ujinga. Wananchi waliyowengi tanzania wana akili zaidi yako.
Bado mpo
 
Mbona ndiyo hao hao wapo kwenye system? Tungeanza na yule aliyesema Nondo alikuwa kwa demu wake
 
Wewe ni zoba , we si ndio ulikuwa mmoja WA wajinga waliokuwa wanamsifia mwendawazimu WA chato Yule kila siku humu ,?
Aisee tunakokwenda ni kuzuri huyu yamaa amebadilika. Leo amekubali kuwa walikuwa wajinga. Huyu ana ID nyingine Chinembe.


Wengine waliookoka kutoka kwenye laana ni

1. Imhotepu
2. Ndege john
3. The baptist
4.britanicca
Etc
 
hilo kundi ndio wale watanzania zaidi ya 59.5 milion.

waweza kuwa wajinga,ila wapumbavu laki 5 waliobaki ndio kundi hatari zaidi.

hili kundi la watu laki tano au pungufu zaidi,linajumuisha wafuatao.
wauza unga pamoja na mademu zao.
wezi wa vyeti na wavivu kazini.
mashoga na watumiaji wa madawa ya kulevya.

kama taifa tuna kazi ngumu sana ya kufutilia mbali hilo kundi la watu laki 5,ambai hata baada ya JPM kufariki bado uhakika wao wa kuishi uko kashakani.
Acha uongo. Tanzania sasa kuna amani.
Kama unakula unga we kula tu athari utaipata mwenyewe.
 
Kuondoa ujinga ni dhana Pana, haimaanishi kujua kusoma na kuandika tu ndio kuondoa ujinga. Moja kati ya fursa tuliyoipata katika awamu ya tano, ni kujua kwamba, kama taifa, tuna kundi kubwa sana la wajinga, ambalo, limekaa pale, linasubiri mtu alitumie tu, na litampa uhalali wa kutenda maovu makuu ya kuchukiza, ya kihayawani, na ya makufuru. Lakini, maovu hayo yatakuwa na uhalali wa sanduku la kura, kama ilivyokuwa kwa Hitler, na yeye alishinda kwa kura nyingi. Muovu ana uhalali wa kura! Hivyo ni kiongozi halali kikatiba!

Tuna kundi kubwa lililosherehekea utekwaji, mauaji, ukatili, kubambika kesi, kunyanyasa watumishi, dhuluma kwa wafanyabiashara, kundi Hilo kubwa ni la JPM.

Kama taifa, lazima tuwe na mikakati ya kuondoa ujinga katika kundi hili. Ujinga wa kuwafanya waelewe kwamba yale yalikuwa ni matendo ya kihayawani kabisa na hayafai katika nchi hii.
Fikiria mhitimu wa chuo kikuu asiye na ajira aliyekuwa anashangilia JPM kuzuia ajira serikalini na kuua uwezo wa sekta binafsi kuajiri.

Muajiriwa wa mfanyabiashara anafurahia uonevu dhidi ya bosi wake, baada ya mwezi kampuni inakufa, anakosa ajira

Fikiria mkulima wa korosho, mnazi mkubwa wa JPM japo aliona zao la korosho lilivyonajisiwa.

Tafakari mwananchi anayesifu sera za kunyima watumishi maslahi, halafu anaishi kwa kutegemea ndugu zake ambao ni watumishi ... Kila siku kupiga mizinga.

Fikiria watanzania waliokuwa wanashangilia kwa furaha kubwa kuona au kusikia fulani katekwa, mfanya biashara fulani kafilisiwa au kabambikwa mamia ya kesi, au kanyanganywa fedha zake zikizokuwa benki.

Mkuu wa Mkoa anaiba au kudhukumu magari, halafu anayawekea plate number za serikali, na like kundi la wajinga linatopea katika kumsifu sana kwamba ni kiongozi bora,gari ya wizi anaweka plate number za Mkuu wa Mkoa (RC)!

Nadhani kama nchi, tuandae programu maalum ya kuufuta ujinga huu ili kundi hili kubwa la wajinga,lipate uelewa. Haijalishi ni shilingi ngapi itatumika, lakini taifa litaponywa.

Kundi hili bado lipo, lina kiu ya damu ya watanzania wenzetu na halijashiba, ilibidi wengine wafukuziliwe Malawi, maana muda wote walikuwa wanaimba damu! Damu! Damu!.

Tutumie Redio,tv, na wasanii, shule, vyuo, viongozi katika hotuba kuufuta ujinga huu. Kila kiongozi akipata fursa ya hotuba aseme hili.

Kundi hili linahitaji elimu tu na uwazi wa taarifa ili kulivua utando wa propaganda za kipumbavu na kijinga kutoka awamu ya tano.

Kundi hili yule aliyefukuziliwa Malawi alikuwa anahangaika kuliweka pamoja ili limpe kura, jitihada zifanywe kuibomoa gundi iliyolishikamanisha, viongozi wanaoendelea kulitegemea ili wapate kura, wabomolewe kisiasa kabla hawajabomoa taifa.

Mama Samia amefanya makubwa sana kulijenga taifa na kulifanya liwe pamoja ...tumuunge mkono kwa namna yoyote ile
Lile kundi la wauaji akina Musiba lilikufa pamoja na dikteta wao
 
Back
Top Bottom