Lini Tanzania ilibadili msimamo wake kuhusu Israel?

Lini Tanzania ilibadili msimamo wake kuhusu Israel?

Mzee wangu, mwandishi nafahamu umeandika vitabu na huwa nafauatilia makala zako za uhuru na historia iliyofichwa na nazipenda makala lakini kwa hili nikuukize swali moja kama lizakisha jingine sawa.
Nimesoma elimu ya msingi na kuendelea na wewe vivyo hivyo.
Swali. Niambie nikipindi gani darasani tulibaguliwa kwa udini aidha kulingana na maeneo tuliyotoka au kwa majina ambapo ilipelekea waislamu wasifundishwe vipindi au masomo fulani na ikapelekea kufeli na wasiendelee? Iwe shule ya msingi, sekondari au chuo?
Omu...
Sijapata kusikia hilo.
 
Hiki ni tatizo kwake( Mzee Mohamed) na baadhi ya Waislam...! Wao Kila kinachofanywa na Mwarabu ni kizuri! Hmmbonankuna Waislam weusi huko Sudan wanajmchinjwa na Janjaweed wamekaa kimyaaaa!
Wanaona fahari Mwarabu akimegewa Bandari zetu kama Peremende.
 
Ndugu zangu,

Lini Tanzania ilibadili msimamo wake?

Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma Mjini na Mwenyekiti wa ACT Wazalendo ni kijana hodari mwenye kujua kuchagua maneno yake vyema.

Hapo chini ameandika masikitiko yake kuhusu Tanzania kukataa kupiga kura kulaani mauaji ya Waislam Myanmar.

Katika maandishi yake neno, ''Waislam,'' halipo.

Lakini dunia nzima inajua kuwa wanaouliwa Myanmar ni Waislam si suala la kuuliwa ''wananchi.''

Iwe itakavyokuwa Zitto Kabwe kaeleza masikitiko yake ili Watanzania wajue nini kimetokea.

Kwa sera ya Tanzania kuhusu msimamo wake wa kusimamia haki duniani kote kitendo hiki ni mabadiliko makubwa sana katika msimamo huo uliowafikisha Watanzania kupigana Msumbiji bega kwa bega na Frelimo na kutoa misaada kote kulikokuwa na dhulma sawa na kauli ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliposema, ''Tunataka kuwasha mwenge uangaze kote na kuleta matumaini kule watu walikokata tamaa.''

Hii sera mpya ya kushindwa kulaani mauaji ya Waislam wanaouliwa Myanmar huenda ikawa ni sera mpya ambayo kwa sasa ndiyo inaongoza Tanzania na uhusiano wake na mataifa mengine.

Ndiyo kusema kuwa sasa Tanzania haijali tena dhulma bali inaongozwa na maslahi yake mengine ambayo kwa bahati mbaya kwa sasa hayajakuwa bayana.

Tanzania ilianza na kurejesha uhusiano na Israel uliovunjwa na Baba wa Taifa mwenyewe nusu karne iliyopita.

Leo Tanzania imeridhia kutopiga kura kwenye mauaji ya kimbari ya Waislam wa Mynmar.

Wachunguzi wa siasa wanasubiri kutazama nini lingine litafuatia.

Labda hilo litatoa mwanga zaidi kuonyesha nchi yetu imesimama upande gani na kwa nini.

Ingekuwa ni kura ya East Timor na wanaouliwa ni Wakatoliki Tanzania ingekaa pembeni ikaacha kupiga kura?

Jibu unalo wewe ndugu msomaji wangu.

Maandamano ya kuwaunga mkono Wapalestina yamezuiwa yasifanyike na kiongozi wake Sheikh Issa Ponda, Katibu wa Shura ya Maimamu Tanzania amekamatwa.

Ndugu zangu iwe iwavyo.

Kweli Tanzania ni ya kuwazuia wananchi kufanya maandamano ya amani kuwaunga mkono Wapalestina?

Nitaweka hapa historia ya Wapalestina na Tanganyika kuanzia miaka ya 1940 hadi uhuru unapatikana na msimamo wa Nyerere katika kuwaunga mkono Wapalestina.

Umma unasubiri.

Hicho kijikofia alichovaa balozi ni alama ya uyahudi
tangu lini balozi wetu ni myahudi?
 
Nelson...
Nimekujibu lakini kuna jibu ulilotegemea kutoka kwangu hukulipata.
Hapana sikukuuliza mm hilo swali mzee wangu.
Bali nilikuuliza mbona hujajibu ulichoulizwa kuhusu mauaji ya wabantu north darfur na Blue Nile,,,,wanaouliwa na waarabu wa janjaweed.
Na ukakimbilia kusimulia historia ya Mahid movement.
Au waislamu waafrika wa Sudan kwako hawana thamani ya uhai kama waislamu waarab wa Palestine ????
 
Hapana sikukuuliza mm hilo swali mzee wangu.
Bali nilikuuliza mbona hujajibu ulichoulizwa kuhusu mauaji ya wabantu north darfur na Blue Nile,,,,wanaouliwa na waarabu wa janjaweed.
Na ukakimbilia kusimulia historia ya Mahid movement.
Au waislamu waafrika wa Sudan kwako hawana thamani ya uhai kama waislamu waarab wa Palestine ????
Nelson...
Samahani kama nimekosea kukupa jibu wewe.

Kukimbilia: "kukimbilia," historia ya Mahdi.

Labda unifafanulie mtu anakimbilia vipi?
 
Nelson...
Samahani kama nimekosea kukupa jibu wewe.

Kukimbilia: "kukimbilia," historia ya Mahdi.

Labda unifafanulie mtu anakimbilia vipi?
Tutaongea kesho mzee wangu.
Nipo naandika makala mbili zipitie uzisome.
RISASI SIO SULUHISHO NA MZOZO KATI YA FDRL NA RPF KIMBUKUMBU ZANGU
 
Hapana sikukuuliza mm hilo swali mzee wangu.
Bali nilikuuliza mbona hujajibu ulichoulizwa kuhusu mauaji ya wabantu north darfur na Blue Nile,,,,wanaouliwa na waarabu wa janjaweed.
Na ukakimbilia kusimulia historia ya Mahid movement.
Au waislamu waafrika wa Sudan kwako hawana thamani ya uhai kama waislamu waarab wa Palestine ????
Nelson...
Inabidi umjue unaejadiliananae kwanza ndiyo ufanye mjadala.

Mimi nimesoma elimu ya mjadala na nimefundushwa miko yake.

Siwezi kutumia kalamu yangu kuunga mkono dhulma.

Haya ndiyo mafunzo niliyopitia.

Ukishikilia habari za Dafur kutafuta undani wangu utakuwa unapoteza muda wako.

Niulize maswali yenye maana nikujibu ukumbi ufaidike.
 
Back
Top Bottom