Lissu na Lema wamerudi Salama. Chadema wameanza kufanya Mikutano. Rais Samia ashukuriwe sana

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Tangu Rais Samia Suluhu aingie madarakani upepo wa kisiasa nchini umebadilika sana . Tumeona Mikutano ya kisiasa ikirejea nchini, siasa za vyama vya upinzani majukwaani zimerudi tena na mazungumzo ya kuimarisha Demokrasia yanazidi kushika kasi.

Kubwa zaidi tangu Rais Samia ashike madaraka tumeona Tundu Antipas Lissu akirejea nchini na leo aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amerejea nchini na katika matukio yote haya Jeshi la Polisi limeimarisha ulinzi na usalama kwa hali ya juu kabisa.

Tanzania kama Taifa la Kidemokrasia tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kututoa gizani na kuweza kushuhudia tena Demokrasia ikitamalaki katika nyanja zote.

 
Samia Suluhu Hassan is a Man.

Sio mwanamke, waliokuwa wanaogopa mikutano ya kisiasa ni wanawake
 
N wenje karudi
 
Mungu hakufurahishwa na urais wa mtu yule dhalimu
 
kuna nyuzi zingine zinaanzishwa makhsusi ili wachangiaji wamtukane kipenzi cha watu Magufuli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…