Lissu: Naishi kwenye makazi ya balozi(Ujerumani) kwa sababu maisha yangu hayako salama, nitarejea Ubelgiji

Lissu: Naishi kwenye makazi ya balozi(Ujerumani) kwa sababu maisha yangu hayako salama, nitarejea Ubelgiji

Ametafuta justification ya kuhalalisha kuishi Brussels. Nani ahangaike na Lissu wakati huu ambapo hana madhara. Labda ndani ya CHADEMA huenda anatishia uenyekiti wa mtu ambapo ni sawa na uhaini.
Mwanzoni mlisema hivihivi halafu mkaenda kumpiga risasi mchana saa sita. Nyie hata shetani atakua anawaogopa
 
Ni mvinyo uleule ndani ya chupa mpya. Lengo ni kuingiza watu barabarani na kuvuruga amani yetu. Lissu anautaka Urais either kwa shari ama kwa amani.
Urais mmeunyakua kwa kura za kupika kule JAMANA printers. Wasukuma in waoga sana
 
Njama, hila na ulaghai wa Lissu umeshajulikana. Yaani kipindi chote cha kampeni hakukuwa na tishio, iweje baada ya Uchaguzi awe anatishiwa?

Asichofahamu ni kudhani alikuwa anapendwa na watanzania kumbe wananchi walikuwa wanaenda kwenye kampeni zake kumfurahisha maana alikuwa anataka Kura za huruma.

Uzuri ni kuwa hata hao Wazungu anawalilia sasa hivi wameshamfahamu kwamba ana matatizo ya kisakolojia.
Hata pale mwanzo mlisema hivi hivi kabla ya kummiminia risasi. CCM hata shetani atqkua anawaogopa
 
Maelezo yako na conclusion uliyofikia kama haviendani. Awali umeeleza wasiwasi aliokua nao TL kuhusu usalama wa maisha yake hadi akaamua kuomba hifadhi kwenye makazi ya Balozi wa Ujerumani.

Sasa jinsi ulivyomalizia ndio sijaelelewa. Ni kwamba tujihadhari naye kwasababu tu ya yeye kua mwanasheria tricky au ni kitu gani? Jamaa hana jeshi, hana polisi au hata mgambo. Hana chombo chochote cha habari pengine ataeneza propaganda zake za "kuhatarisha amani" na usalama wa nchi, na hata angekua nacho kingefungiwa na Mamlaka za Udhibiti, Hiyo hatari yake mpaka sisi tulioshinda kwa tsunami na wananchi wanatupenda kwelikweli tuanze kumuogopa iko wapi?
Hakuna amani yoyote inayohatarishwa. Uoga wenu ndo unawafanya mjazwe na roho ya kishetani kuua watu
 
Huyu anajishitukia tu, na hilo lipo wazi anatafuta huruma za mabeberu waendelee kumfadhili ili siku moja aje kuwalipa fidia hana jipya kwa sasa wala hata hao anao wahic hawanahabari naye

sent from HUAWEI
No. Acheni roho chafu ya kuua raia wenzenu. Hata Mara ya kwanza mlikua MNA beza hivi hivi baadaye mkampiga risasi. Ccm ya wasukuma waoga sana
 
Tundu Lisu atakua ni muongo kuliko hata uongo wa shetani
Waongo ni nyie ambao mnabiasha hapa Ku spin story huku MNA bastora viunoni . last time mlibisha hivi hivi mitandaoni kabla ya kutimiza azma yenu ya kutaka kumuua.
 
Watanzania hawawez kukimbilia ubalozin kama unabisha na wewe nenda
Nimekwambia hata last time kabla jamjaenda kumpiga risasi kule dodoma mlianZa kwanza kubisha kipropaganda hivi hivi humu kwenye mitandao. By the way uelewa wako ni mdogo. Ulitaka akimbilie wapi ambapo labda ungempata kirahisi ?
 
Wasanii wa kiwango Cha kimataifa. Lissu tulikuwa tunamwambia bado kinda, haelewi nchi inaendeshwaje anatua na beberu wake eti mwanasheria Amsterdam.
 
Tunajua unakimbia kesi yako ya uchochezi.
Kweli uzunguuke miezi miwili ukiwa unafanya kampeni maisha yako yasiwe hatarini, leo ndio maisha yawe hatarini???

Lissu jua kuwa watanzania sio watoto wadogo tunajua unachokifanya ni kukimbia kesi yako mahakamani. Nenda kwenye kesi walio kuwekea dhamana wana hangaika, kama kweli unapenda wananchi wako basi nenda mahakamani ili walio kuwekea dhamana wajitoe.

Acha kukimbia kama mtoto this time you will eat fruits of your mouth.
Hapana nikwasababu mmejawa na roho ya shetani. Hata last time mlibisha sana hivi mitandaoni kabla hamjaenda kummiminia risasi kule dodoma
 
Tundu anapenda tu kupakatwa na wazungu. Anadai maisha yake yako hatarini, mbona alikuwa anatemebea kwa miguu feri, Kariakoo na kwingineko bila kubughudhiwa, alikuwa na hatari gani?
 
Once a liar always a lier.

Kwanini asylum aepewe yeye pekee na sio na wenzake?

Kuna kumbukumbu ya picha walau akinZisha safari ya maandamano ya amani walau tumpe kongole kwa hili kama au ndio wale kuwatanguliza wenzie huku yeye an surety ya mkate toka kwa mabeberu??
 
Hata pale mwanzo mlisema hivi hivi kabla ya kummiminia risasi. CCM hata shetani atqkua anawaogopa
Kama nia ni kumuua, ilishindikana nini asiuawe wakati wa kampeni? This is just a cooked story, kutaka kuleta taharuki bila sababu!
 
Ndugu, kama hana madhara kwa nini wanakata kutoa clearance ili aondoke zake.
Kuna ishu za kimahakama inabidi zishughulikiwe, au hujui kana ana kesi sita hazijaisha?
 
Unaelewa maana ya nchi?

Huelewi unachoongelea, kuingia kwake kwenye ubalozi wa nchi technically anakuwa yupo kwenye "foreign soil", jaribio lolote la kumgusa linakuwa halina maana kwa sababu gharama itakayolipwa ni kubwa mno. Jaribu kuangalia jinsi Jullian Assange alivyowasumbua waingereza kwa kukimbilia Ecuador, kama sio kutemwa na Ecuador alikuwa haguswi.

Kiufupi kuendelea kukimbizana na Lissu kwa sasa ni kupoteza muda, kama anataka kuondoka aachwe aondoke, ikumbukwe kuwa hivi sasa kuna chokochoko nyingi zinaendelea kuhusiana na malalamiko kuhusiana na uendeshaji wa uchaguzi wetu, mataifa ambayo ni marafiki wa hao hao wajerumani wametoa matamko mengi yanayosihi uchunguzi wa mapungufu hayo.

Kwenda na kujaribu kumgusa Lissu ndio itaongeza madoa kwa serikali yetu, hakuna haja ya kuvunja mahusiano ya kimataifa kwa sababu ya mwanasiasa mmoja aliyeshindwa uchaguzi.
 
Back
Top Bottom