THE BIG SHOW
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 16,950
- 13,527
Mimi nimeshangaa, mafunzo ya judo na karate china watoto wanajifunza tokea wakiwa watoto wadogo kabisa, cha ajabu ni nini watoto wakifunzwa mafunzo hayo??Labda waseme kuwa wameachishwa shule na kutoroshwa au hiko chuo hakina usajili sawa, ila mafunzo hayo yana kasoro gani?Tuweke udini pembeni
Je Watanzania hawapaswi kujifunza karate na judo? Je mbinu za kujilinda ni kinyume na sheria za nchi? Hizi tahariko tunazobabatizwa nazo kila mara kwa jina la ulinzi na usalama, kwa nini serikali isipeleke mamluki wake hapo nao wakajifunza hayo mafunzo ili kuyachuja kama ni hatari kwa jamii? Naona badala yake ni hizi Kamati za Ulinzi na Usalama zimejikita kwenye kupambania taharuki kuliko kutumia weledi na akili kudeal na haya mambo
Labda watuambie kuwa wamekuta silaha na mabomu labda, wanaacha mambo ya msingi wanakimbilia kupiga vita mafunzo ya ukakamavu?