Lucas Mwashambwa toa maoni yako kuhusu kauli ya Rais Paul Kagame

Lucas Mwashambwa toa maoni yako kuhusu kauli ya Rais Paul Kagame

Nimefika na kumaliza madarasa yote hapa Nchini kuanzia chini hadi juu wanakoshindwa kufika watu wengi.
Ila mimi sijaongea kisiasa kama wewe unavyoongea kwa kujilinganisha na jumuiya ya kitanzania unaposema wengi hawajafika. Je una data and statistics za ku prove point yako malafyale?
 
Lucas Mwashambwa kwa kweli umesahau wajibu wako. Sijaona sehemu umesifia watanzania walivyoupiga mwingi wakiwa Korea. Hijaongelea ule mkutano wa wakorea wanne na watanzania lukuki huku kukiwa na Lulu yule aliyekua na kesi ya mauaji na wasanii wenzake.
Hebu tupe taarifa kwa undani.
 
Ila mimi sijaongea kisiasa kama wewe unavyoongea kwa kujilinganisha na jumuiya ya kitanzania unaposema wengi hawajafika. Je una data and statistics za ku prove point yako malafyale?
Ndio ninazo na zipo wazi kabisa kwa yeyote ambaye akizitaka.
 
Haka kazee Kapuuzi Puppet wa wazungu wanakatumia kufanya machafuko DRC Congo Ili waibe madini, alafu kampuni ya Total ilimtumia kupeleka wanajeshi wake Msumbiji kakafeli.
 
"If the owners of the natural resources go around begging, then you should know there's something wrong with their minds”

View attachment 3009379
Mwashambwa yaani tafsiri yake ni kwamba anashangaa kuona nchi yenye rasilimali nyingi kama tanzania kwenda kuombaomba kwa wazugu na kwamba lazima kuna tatizo kwenye vichwa vya viongozi wa CCM
 
Siyo Rasilimali za asili pekee unazomiliki ndio zinakufanya uwe tajiri.bali inahitaji akili ,pesa, teknolojia,maarifa na ujuzi wa watu wako unaotokana na kupata Elimu bora na ya viwango vikubwa.

Embu fikiria hata kama una gesi asilia lakini huna pesa, wataalamu wenye ujuzi na uzoefu, teknolojia na mengine mengi ni vipi utavuma gesi hiyo?

Hiyo ndio sababu ya viongozi wenye Akili kubwa ,maarifa na maono makubwa aina ya Daktari Samia Suluhu Hasssan hutumia akili kutafuta pesa kwa njia mbalimbali kama ya mikopo nafuu kabisa isiyo na athari wala maumivu kwa walipakodi na mali na utajiri wa Taifa letu.

Lakini pia kuna masuala ya ubia kati ya serikali na Secta binafsi kama ambavyo hufanyika hapa Nchini na njia nyingine mbalimbali zinazokubalika na zenye maslahi kwa Taifa letu.

Angalia hata Mheshimiwa Paul Kagame yeye na Nchi yake wanadaiwa shilingi ngapi kutoka mataifa ya nje,taasisi za kifedha na mashirika mbalimbali ya kifedha kutoka maeneo mbalimbali Duniani?
Umesahau lile neno lako pendwa "mama anaupiga mwingi"
 
Kuna Raisi mmoja Alishawahi kusema "uchumi mnao ila mmeukalia", mkadhani anawatukana.
 
Yule mtutsi itakuwa tumemkanda mahali si bure, na sasa tuongeze majeshi yetu yakawakumue zaidi M23 watokomee kwao Rwanda na wakija bongo tuwadake tuwakabidhi kwa serikali ya Congo DRC.

Ni hatari mno kuruhusu waasi wa Congo toka Rwanda kumiliki sehemu ya Congo maana wakitamalaki huko Goma lazima watatest mitambo bongo.

Sisi bongo hatuombi tunakopa na uwezo tunao tunalipa, mtutsi anajitekenya na kucheka mwenyewe. Hayo ni aina tu ya mayowe ya mkosaji.

Mama Sa100 mbele kwa mbele
 
Acha ujinga wako wewe. kwa hiyo unafikiri kuna pesa zinazogawiwa kama njugu huko Duniani ?
Mimi niwe "mjinga" wewe utakuwa nini? Kwanza tayari wewe ni chizi, hata kwenye ujinga humo.

Hapo unaposema "pesa zinazogawiwa", umesoma popote nilikoeleza hivyo? Wewe unachojuwa ni pesa tu basi! Wigo wa elimu mnayopata inawanyima uwezo wa kutumia akili alizowapa muumba wenu. Hasa wewe ni kiazi kweli kweli.
 
Acha dharau zako wewe. Mimi nimepiga shule sana na nilikuwa kinara wa kuongea kizunguu kwenye mijadala shuleni mpaka wanafunzi wanashangilia kwa kelele za shangwe huku wanabubujikwa na machozi ya furaha.
Kuongea na kuandika ni vitu viwili tifauti, tuwekee audio kuthibitisha hayo unayoyasema au ungeandika kwa kithungu ukijibu comment yake, ukweli ni kwamba umepitia darasani lkn haukuelimika na yawezekana ukawa masters degree.
 
Back
Top Bottom