Utajipa tabu bure na kujiumiza kichwa,sehemu nyingi Tanzania,hasa sehemu za Pwani,ndani ya familia moja wamechanganyika wakristo na waislamu, na wanashirikiana kwenye furaha na huzuni,usishangae kwenye mashindano ya Qur'an kukuta wa dini zote wapo.
Na mashindano yakimalizika ni saa saba,wakiondoka hapo wote kwa pamoja wanakwenda kutembea kwenye Pasaka.
Kuna wakati kulikuwa na jirani zangu ni waislamu,wakawa wamefiwa na mjukuu wao,kufika mjukuu ni mkristo na maiti imeletwa kwa babu yake muislamu,wakachanganyika waislamu na wakristo,bila kubaguana.