Uchaguzi 2020 Maajabu ya Gwajima: Waumini wananyeshewa mvua, yeye anaahidi kujenga barabara kwa pesa zake mwenyewe

Mkuu hii miaka 10 tutashuhudia mengi sana anadai kuketa boti za uvuvi mbona kwa nini asingeanza kwa waumini wake😁😁😁😁😁😁 inawezekana lisu alisema kweli kuna watu Yohana anawaokota majalalani
 
Hakuna mahali tapeli amewahi kuwa mkweli hata kwa kwake mwenyewe
Wakati akiwa kwenye saccos yenu mlikuwa mnamsifia sana tu ametoka amekuwa tapeli!! Wanasaccos naona akili zenu ni utopolo!!
 
Kura yangu nitampa halima ✔ , Gwajima akadanganye huko kanisani kwake, uzur kawe tunauwelewa mkubwa kuliko Gwajima
 
Kawashika pabaya kawe imekwenda kiumeni halisi, huyo kidude mtafutieni kazi ingine
 
Sijui lihonga wajumbe au ukabila umemsaidia kupitishwa
 
Wapinzani bwana hamna hoja kabisa
Wewe hoja yako ni IPi
Kupora KOROSHO za WAKULIMA?
Kuua na kuteka watu wanaokupinga kimitizamo?
Kubomoa nyumba za watu bila kulipa fidia?
Kununua wabunge na madiwani kisha kuwarudisha kwa kupitia wizi wa kura?
ULISIKIA WAPI MBUNGE AKIJENGA BARABARA KWA PESA ZAKE CASH ? ALIZIPATAJE? ATALIPWAJE?
Ajenge kwanza kabisa lake
 
Umekinukisha mbaya mwache DR bishop mzee wa wa mabastolaz, ngadaz according to bashite, mzee wa mabodyguard wenye bindukiz
 
Nyuzi za Gwajima zinaongezeka Sana, inawezekana huyu bwana anaonekana ataukwaa ubunge hivyo wapinzani wake wanajitajidi kumwongelea vibaya ili asiupate. Asingekua tishio kwenye siasa asingeanzishiwa nyuzi zote hizi.
Naona Kama nikuzuia mafuriko kwa mikono.
Ngoja tusubiri 28/10/2020.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Wapepeta kiuno wenzie ndio watamchagua.
 
Huna ushahidi wa unayoyasema zaidi ya porojo tulizozizoea kila siku
 
Siipendi Chadema lakini Kawe bora wampe Halima
 
Alishasema kuwa mbunge ni kujishusha kaamua sasa sio tu kujishusha, kujidhalilisha
Umenikumbusha aliwahi kusema yeye ni zaidi ya Rais, inakuwaje sasa anautaka ubunge[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Huna ushahidi wa unayoyasema zaidi ya porojo tulizozizoea kila siku
Ushahidi kwamba KOROSHO ziliporwa ? Mm ni kati ya walioporwa mzee
Ushahidi kwamba watu wameuwawwa na kuteka ben Sanane, azory gwanda, tundu Lisu na Mauaji ya kibiti.

Ushahidi kwamba watumishi hawajaongezewa mshahara mm mtumishi wa umma
Ushahidi kwamba nyumba zimebomolewa vila watu kulipa nenda KIMAra ukaone
Huyu ni raisi katili kuliko waliowahi kuwa makatili hapa nchini
 
Wewe ni Kangomba lazima useme uliporwa korosho. Kumbe Ben sanane ameuawa? Kama unaushahidi wa kutosha Katoe ushahidi wako polisi ili wauaji wakamatwe na haki itendeke. Huna jipya mzee mauaji ya kibiti yanahusika vipi na Magufuli?
Kipindi cha Kikwete mlisemaje? Mnataka rais dikteta sio nyie? Nenda kimara leo uone barabara zinavyopendeza foleni imekwisha kabisa. Suala la kutolipwa fidia tulishalijadili sana humu.
Hujapandishwa mshahara acha kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…