Uchaguzi 2020 Maalim Seif anapodai "Mamlaka Kamili" anamaanisha kuvunja Muungano?

Uchaguzi 2020 Maalim Seif anapodai "Mamlaka Kamili" anamaanisha kuvunja Muungano?

Seif anawahadaa wapambe wake kwani ili kuvunja muungano inabidi ipatikane theruthi mbili ya bara na mbili ya Zanzibar wakati Zanzibar wagombea wake 15 wameshaenguliwa ni wazi hatazipata.

Wapemba wengi wamewekeza bara ikiwamo na yeye mwenyewe ana nyumba bara hivi unafikiri ni wajinga wamruhusu avunje muungano maana kitakachofuata kila mtu arudi kwao

Hivi huyo aliyekwambia kuwa muungano ukivunjika kila mtu atarudi kwao ni nani?

Acha mawazo ya KiCCM hayo ndugu
 
Akilazimisha anafunguliwa kesi ya uhaini hata yeye anajua.
Muungano ukivunjika na faida zake zinavunjika bakhresa atabaki kama mwekezaji, wapemba aliowaajili watapunguzwa na wanaobaki itabidi walipiwe work permit na resident permit atakosa faida nyingi sana ndio utambue nani anafaidika na muungano

Mkuu unafahamu kuna waTanganyika wangapi waliojariwa katika sekta ya Utalii Zanzibar?
 
Zanzibar ina nafasi nzuri ya kuwa taifa lenye maendeleo makubwa ikijitenga kuliko sasa.
Lakini inaweza ikaendeleza undugu na Bara ikiwa nje ya Muungano.
Bara itafaidika zaidi Kibiashara ikiwa Zanzibar itajitenga,itauza bidhaa nyingi mno katika visiwa hivyo.

Tatizo kubwa linalotusumbua ni kuwa na roho mbaya pamoja na kukosa muono wa mbali.

Muungano unaizuia sana Zanzibar kimaendeleo.

Na Zanzibar ikipata maendeleo ya Kibiashara na Utalii basi wa Tanganyika ndio watakua wanufaikaji wakubwa kuliko watu wanchi yoyote nyengine.

Watanganyika wataendelea na fursa ya kuuza mazao yao visiwani
Watanganyika watapata fursa ya kununua bidhaa za nje kwa urahisi Zanzibar
Employment opportunities hasa kwa kazi za sekta za kitalii zitawanufaisha sana waTanganyika.
 
Kwa uelewa wangu. Tuna serikali mbili.Serikali ya Wazanzibar na Serikali ya Watanganyika. Huu ndio ukweli.
Serikali ya Tanganyika imechuku Kofia Kama Serikali ya Muungano, na ndivyo inavyoitwa.
Ni mbinu tu imetumika kwa namna Fulani imekua serikali ya Muungano kwa kuweka baadhi ya Viongozi kutoka Zanzibar, ikiwemo pia na Bunge la Tanganyika kuwa na wawakilishi kutoka Zanzibar ili lionekane Bunge la Muungano.

Ila Namba ya Wazanzibar waliopo kwenye hii serikali ya Muungano, plus waliopo Bungeni wanauwezo wa kuiwakilisha Zanzibar sawa sawa kwenye kutetea au kuwakilisha Wazanzibar kwenye maamuzi ya maswala ya Muungano.
Ni wazi hawana uwezo kwasababu serikali yetu Ni ya "kidemokrasia" na maamuzi yanafanyika kidemokrasia ikiwemo Bungeni. Kwa idadi ya wawakilishi waliopo kwenye Bunge hawawezi kuwa na uzito"impact" ya maamuzi hata wakiungana wote.

Hivyo kwa mtazamo huu Maswala yoote ya Muungano yapo chini ya Watanganyika. Maana wao ndio Wana idadi kubwa kwenye maswala ya Kimaamuzi kidemokrasia.

Kwa maana hiyo ni sawa kwa Maalim kuona Serikali ya Zanzibar Haina mamlaka Kamili maana Kuna maswala Mengi yanayo wahusu Wazanzibar yamewekwa Kwenye serikali ya Muungano. Na yakiwa chini ya hiyo serikali hawawezi kuyaamulia.
Maana yake Serikali ya Zanzibar Haina mamlaka juu ya maswala hayo.

Suluhisho Ni Katiba, au mikataba wa Muungano. Ninavyoelewa kwa Kauli hiyo. Maalim Anataka Maswala yanayo wahusu Wazanzibar yawe chini ya mamlaka ya Wazanzibar wenyewe kikamilifu.

Pili maswala ambayo yatakua chini ya Muungano yaridhiwe na Pande zote mbili za Muungano, na yawe na uwakilishi sawa ( hata Kama sio kiidadi) ila kila serikali iwe na Kura yenye uzito sawa .
mfano Kama Watanganyika wapo Mia moja. Na wazanzibari ishirini kwenye uwakilishi wa maamuzi ya maswala ya Muungano. Basi kura ya kila mwakilishi wa tanganyika iwe na uzito wa nusu kura.
Na ya mzazibar iwe na uzito wa Kura mbili na nusu. Ili kuweka uwiano sawa wa uwezo wa kuamua kwa kila upande.

Huo ni mfano tu wa kuweza kuwaoa mamlaka sawa Wazanzibar.
Ukiangalia kwa namna hiyo hapo lazima serikali tatu ziwepo.

Vinginevyo lazima uwe usanii.Au la wazanzibari wenyewe, wananchi. Wakubali serikali yao imezwe chini ya serikali ya Muungano. Maana yake Sasa itabidi kuwe na Serikali kuu moja tu. Ya mapinduzi isiwepo.
Uwepo wq serikali ya Zanzibar inalazimu uwepo wa serikali ya Tanganyika. Kama watataka kuwepo na usawa wa maamuzi kwenye Muungano ambao Sasa utakua na Serikali yake ya tatu.
 
Hivi huyo aliyekwambia kuwa muungano ukivunjika kila mtu atarudi kwao ni nani?

Acha mawazo ya KiCCM hayo ndugu
Kwa hiyo mnataka muvunje muungano halafu mbaki bara kufanya nini, hapa mpo kwa ajili ya muungano ukivunjika mnakuja kwa visa na kibali maalumu maana mnaweza kutuletea ugaidi
 
Kwa hiyo mnataka muvunje muungano halafu mbaki bara kufanya nini, hapa mpo kwa ajili ya muungano ukivunjika mnakuja kwa visa na kibali maalumu maana mnaweza kutuletea ugaidi
Ha ha Mimi naupenda Sana Muungano. Sio wa Zanzibar na Tanganyika tu. Natamani hata Afrika ya Mashariki yoote iwe nchi Moja .

Lakini naomba nikuulize, Hati/ mkataba wa Muungano Ni Jambo la umma au Siri? Msingi wa Muungano ngano huu ulikua au ni nini?

Je unakua Lina Mambo gani au msingi wake Ni nini?

And For the record Mimi sio mzazibar. Ila Wazanzibar nawapenda Sana.

Soma au fuatilia visa vya hili swala la Muungano utajua huu Muungano una walakini.

Na kuendelea nao kwa namna hii utakuja kuvunjika. Jambo ambalo sipendi litokee kabisa.

Naupenda Bado niendelee kujitambulisha kwa Kujivunia Mimi ni mtanzania. Ila Wazanzibar pia wawe na Ari na Hamu hiyo hiyo wajitambulishe Kama watanzania kwa Kujivunia.
 
Ha ha Mimi naupenda Sana Muungano. Sio wa Zanzibar na Tanganyika tu. Natamani hata Afrika ya Mashariki yoote iwe nchi Moja .

Lakini naomba nikuulize, Hati/ mkataba wa Muungano Ni Jambo la umma au Siri? Msingi wa Muungano ngano huu ulikua au ni nini?

Je unakua Lina Mambo gani au msingi wake Ni nini?

And For the record Mimi sio mzazibar. Ila Wazanzibar nawapenda Sana.

Soma au fuatilia visa vya hili swala la Muungano utajua huu Muungano una walakini.

Na kuendelea nao kwa namna hii utakuja kuvunjika. Jambo ambalo sipendi litokee kabisa.

Naupenda Bado niendelee kujitambulisha kwa Kujivunia Mimi ni mtanzania. Ila Wazanzibar pia wawe na Ari na Hamu hiyo hiyo wajitambulishe Kama watanzania kwa Kujivunia.
Nikikujibu juu ya hati ya muungano nitaongea uongo kwani sijawahi kuiona lakini mkiungana lazima kuna vitu utapoteza sasa kuna wengine hawataki kupoteza ila wanataka kupata tu
 
Nikikujibu juu ya hati ya muungano nitaongea uongo kwani sijawahi kuiona lakini mkiungana lazima kuna vitu utapoteza sasa kuna wengine hawataki kupoteza ila wanataka kupata tu
Unalosema ninkweli. Mnapoungana Lazima kila Mmoja apoteze na kutapa kitu.

Sasa nakushauri hebu Karibu kufuatilia huu Muungano historia yake na Visa vyake. Utagundua tuliungana( prematurely).

Kiukweli sijui kwa nini nchi hizi mbili ziliamua kuungana. Nnalofahamu Ni moja tu inaonekana ilikua Ni matakwa ya Viongozi wawili. Na kwa nini wao wakiungana pia Sina jubu la uhakika.

Lakini ukifuatila historia na Visa vya tangu Muungano huu uwepo Mara nyingi Wazanzibar wamekua na Lawama. Mbaya zaidi kila siku zinavyoenda, nilipo Karibu fuatila Inaonekana Zanzibar inazidi kupokwa Baadhi ya Maswala .

Sasa kwanini serikali hizi mbili zisikae chini Kisha zikubaliane halafu wawaeleweshe wanachi juu ya makubaliano yao, kila upande upigie kura Muafaka. Kama Pande zote mbili zikiridhiwa na wananchi wake tusaini Sasa mkataba wa Muungano wenye mfumo ambao wananchi wa kila.upande wameridhika.


Ila bado nakushauri Fuatilia Visa vya Muungano huu ndipo uweze changanua.
 
Unalosema ninkweli. Mnapoungana Lazima kila Mmoja apoteze na kutapa kitu.

Sasa nakushauri hebu Karibu kufuatilia huu Muungano historia yake na Visa vyake. Utagundua tuliungana( prematurely).

Kiukweli sijui kwa nini nchi hizi mbili ziliamua kuungana. Nnalofahamu Ni moja tu inaonekana ilikua Ni matakwa ya Viongozi wawili. Na kwa nini wao wakiungana pia Sina jubu la uhakika.

Lakini ukifuatila historia na Visa vya tangu Muungano huu uwepo Mara nyingi Wazanzibar wamekua na Lawama. Mbaya zaidi kila siku zinavyoenda, nilipo Karibu fuatila Inaonekana Zanzibar inazidi kupokwa Baadhi ya Maswala .

Sasa kwanini serikali hizi mbili zisikae chini Kisha zikubaliane halafu wawaeleweshe wanachi juu ya makubaliano yao, kila upande upigie kura Muafaka. Kama Pande zote mbili zikiridhiwa na wananchi wake tusaini Sasa mkataba wa Muungano wenye mfumo ambao wananchi wa kila.upande wameridhika.


Ila bado nakushauri Fuatilia Visa vya Muungano huu ndipo uweze changanua.
Tatizo kubwa lipo kwa wanasiasa wanatafuta vidosari vidogodogo ili wapare kura kwa wananchi lakini muungano ukivunjika waathirika wakubwa watakuwa ni wananchi wa kawaida wala sio hao viongozi.
Seif Sharif Hamad ndiye aliyeiba nyaraka toka kwa Jumbe ambaye alitaka kuanzisha serikali tatu na Zanzibar kuwa na mamlaka yake lakini sijasikia wanaounga kauli za Seif hawajamwuliza mbona kipindi kile alimsaliti Jumbe hivyo ukimfatilia utaona ni tamaa ya madaraka inayomsumbua wala sio uchungu kuwa Zanzibar wananyonywa
 
Tatizo kubwa lipo kwa wanasiasa wanatafuta vidosari vidogodogo ili wapare kura kwa wananchi lakini muungano ukivunjika waathirika wakubwa watakuwa ni wananchi wa kawaida wala sio hao viongozi.
Seif Sharif Hamad ndiye aliyeiba nyaraka toka kwa Jumbe ambaye alitaka kuanzisha serikali tatu na Zanzibar kuwa na mamlaka yake lakini sijasikia wanaounga kauli za Seif hawajamwuliza mbona kipindi kile alimsaliti Jumbe hivyo ukimfatilia utaona ni tamaa ya madaraka inayomsumbua wala sio uchungu kuwa Zanzibar wananyonywa
Hilo nalo.
hicho kisa ulichosema Sasa hivi Cha maalim kuiba nyaraka. sijakifuatilia. Siwezi sema lolote juu ya hilo

Swala la Wanasiasa Ni wazi sio mda wote wa kuwaani. Ndio maana mstakabali wa Nchi yoyote unapaswa uachwe kwa wananchi. Wao wenyewe waamue.

Isiwe tu tuwaamini kwa maneno yao ya kusema, wao Ni wazalendo.

Vingine Ni vyeo mfano kumuita mtu mzalendo namba Moja. Ni cheo tu Cha ofisi. Akitoka huyo na Kuingia mwingine, na yeye ataitwa mzalendo namba Moja.

Ila ukweli na Moyoni mwa Muhusika anajua ukweli wa uzalendo wake.

Sisi wananchi tuwahukumu kulingana na matendo yao.
Tusiamini Kauli zao. Tuangalie matendo yao na tuhukumu Kama kweli Ni wazalendo.

Katiba na Sheria ziwape wananchi mamlaka yoote yanayotekelezeka kwa namna na utaratibu wenye tija.

Ila kwa Sasa katiba na Sheria zetu zinabana wanachi kuweza kuamua na maamuzi yao kutoweza kupokwa bila mtu kuingilia kwa kumtumia nguvu au vinginevyo.

Ni vyema wananchi tukadai na kuchukua mamlaka yetu. Wanasiasa waache Hilo liwezekane ili amani na ustawi wetu uendelee.
Waache mamlaka yawe kwa wananchi. Tuwaweke madarakani tunao wataka na wafuate matakwa yetu. Kikatiba na Kisheria
 
Tanzania ya Magufuli bora mgeni kuliko huyo raia , kwani hakuna mgeni aliyebambikiziwa kesi za kijinga

Tanganyika ipo tokea hapo zamani na Zanzibar pia ipo tokea hapo zamani. Watu waliishi na kufanya biashara na hatukusikia hizi fujo mpaka alipokuja Laanatullahi Nyerere akaivamia Zanzibar na kumkamata Waziri Mkuu wake Muhammed Shamte na kumfunga katika jela za Tanganyika kabla huo uvamizi kupewa jina la muungano hapo April 26 1964.

Zawadi yako hii

Asante sana mkuu, hii video nimekua nikiitafuta kwa siku nyingi sana
 
Seif anawahadaa wapambe wake kwani ili kuvunja muungano inabidi ipatikane theruthi mbili ya bara na mbili ya Zanzibar wakati Zanzibar wagombea wake 15 wameshaenguliwa ni wazi hatazipata.

Wapemba wengi wamewekeza bara ikiwamo na yeye mwenyewe ana nyumba bara hivi unafikiri ni wajinga wamruhusu avunje muungano maana kitakachofuata kila mtu arudi kwao
Unamaanisha kawekeza Starlight Hotel? Labda ataihamishia Pemba!
 
Akilazimisha anafunguliwa kesi ya uhaini hata yeye anajua.
Muungano ukivunjika na faida zake zinavunjika bakhresa atabaki kama mwekezaji, wapemba aliowaajili watapunguzwa na wanaobaki itabidi walipiwe work permit na resident permit atakosa faida nyingi sana ndio utambue nani anafaidika na muungano

..Na Bakhresa kidogo-kidogo ataanza kupunguza uwekezaji Tanganyika.

..Ni lazima uelewe kwamba kila upande unamhitaji mwenzake.
 
Bila muungano mzanzibari ataishi Tanganyika kwa vibali sawa na wageni wengine toka mataifa ya nje. Natamani sana hilo litokee.

..na bila muungano Watanganyika hatutalazimika kwenda kuwasaidia CCM-Znz kuiba uchaguzi. Natamani sana hilo litokee.
 
Tatizo kubwa lipo kwa wanasiasa wanatafuta vidosari vidogodogo ili wapare kura kwa wananchi lakini muungano ukivunjika waathirika wakubwa watakuwa ni wananchi wa kawaida wala sio hao viongozi.
Seif Sharif Hamad ndiye aliyeiba nyaraka toka kwa Jumbe ambaye alitaka kuanzisha serikali tatu na Zanzibar kuwa na mamlaka yake lakini sijasikia wanaounga kauli za Seif hawajamwuliza mbona kipindi kile alimsaliti Jumbe hivyo ukimfatilia utaona ni tamaa ya madaraka inayomsumbua wala sio uchungu kuwa Zanzibar wananyonywa

Waliokua hawautaki Muungano ni Wananchi wa Zanzibar usilete kisingizio kwa Seif Sharif

Seif ni muwakilishi tu wa matakwa ya wananchi
 
Back
Top Bottom