Mabadiliko Baraza la Mawaziri: Doto Biteko ateuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Makamba Mambo ya Nje, Pindi Chana Katiba na Sheria

Mabadiliko Baraza la Mawaziri: Doto Biteko ateuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Makamba Mambo ya Nje, Pindi Chana Katiba na Sheria

Rais Samia Suluhu amefanya mabadiliko na teuzi za sura mpya kwenye baraza la mawaziri. Uapisho utafanyika September 1, Ikulu ndogo Zanzibar saa tano kamili asubuhi.
1. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Doto Biteko kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati. Awali alikuwa Waziri wa Madini.

2. Amemteua January Makamba kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali alikuwa Waziri wa Nishati.

3. Amemhamisha Balozi Pindi Chana kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. Awali alikuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo.

4. Amemhamisha Steven Byabato kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Awali, Byabato alikuwa Naibu Waziri wa Nishati.

5. Amemteua Jerry Silaa kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Silaa ni Mbunge wa Ukonga, Dar es Salaam.

6. Rais amemteua Anthony Mavunde kuwa waziri wa madini, mwanzo alikuwa naibu waziri wa kilimo.

7. Prof Makame Mbarawa aliyekuwa waziri wa ujenzi na uchukuzi amekuwa waziri wa uchukuzi.

8. Innocent Bashungwa amekuwa waziri wa ujenzi, mwanzo alikuwa waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa.


View: https://www.youtube.com/watch?v=7bLEuvgVGG4

======

View attachment 2733279
View attachment 2733280
View attachment 2733281
View attachment 2733282

Hakuna jipya, it's business as usual.Niseme hivi,these changes are very cosmetic and clearly show how Samia is not interested in meeting the basic demands of Tanzanians.Kumuweka Makamba kwenye Wizara kama ya Mambo ya Nje shows how she is out of touch with the needs of Tanzanians.Ni muhimu Samia akasoma alama za nyakati.Matukio ya Mali,Burkina Faso,Niger na sasa Gabon,naomba yamuamshe usingizini.Uonevu waliokuwa wanafanyiwa wananchi wa nchi hizo hauna tofauti sana na uonevu tunaofanyiwa pia Watanzania.

Kwangu mapinduzi yanayokea Africa is a new dawn for Africa.Nadhani tawala zote kandamizi ambazo zimeibia watu wao rasilimali wakae mkao wa kula.

Kwa Tanzania haiwezekani baada ya miaka sitini na tatu ya Uhuru tukiwa na rasilimali nyingi kiasi hiki,bado watu wetu wengi hawana maji,na hata hao wachache wanaopata maji si safi na salama;watu wanakufa kwa sababu hawana huduma za afya;watoto wengine hawasomi kwa kuwa wazazi wao hawawezi kuwapeleka shule kwa kuwa hawana michango,madaftari na kalamu au uniform; Elimu inayotolewa ni chini ya kiwango,shule hazina mazingira mazuri ya kusomea na vitendea kazi;watu wetu hawana nyumba bora za kuishi ;watu wetu wanapata mlo mmoja tu kwa siku na wengine hawapati kabisa nk.nk..

No, lazima kama Watanzania tufike mahali tuseme hapana hii haivumiliki tena inatosha,na tufanye kitu ambacho kitatutoa kwenye uonevu huu
 
Naona hujaielewa dhanna ya Reform and Rebuilding.


Hapo kwa Kassim Majaliwa, kilichositisha asipigwe chini ni mfumo tu, lakini ana "underperform" sana, juzi aliambiwa, usingoje maagizo kutoka juu.
Kassim hakubaliani na Utapeli wa DP, ni kwa vile tu Ccm wote wachumia tumbo, ingekuwa nchi za watu wanaojiheshimu Kassim angejiuzuru uwaziri mkuu na angeheshimika daima.
 
Back
Top Bottom