Mabinti wenye umri wa kuolewa na hawajaolewa wafukuzwe nyumbani haraka

Mabinti wenye umri wa kuolewa na hawajaolewa wafukuzwe nyumbani haraka

Hizi mentality ndo zimeharibu wanawake wa sasa
Mwanamke anaenda kuolewa ila ana uhakika akiviruga huko atapokelewa mikono miwili nyumbani kwanin asiwe na kiburi na jeuri kwa mme wake ndo maana ndoa nyingi hazidumu
In short wanaoharibu watoto ni wazazi wenye akili kama hizi
To some extent wazazi ndo wanaharibu watoto,lkn tukumbuke kuwa sehem salama pekee ni kwa wazazi tu.
 
Kuolewa sio lazima,,,nimfukuze aende wapi sasa wakati starehe yangu na Mama yake ndio imemleta yeye,,mbaya zaidi yeye alikuwa hajui na wala hatukuingia makubaliano nae,,ingewezekana angekataa tusimlete dunia,,,kwani kaka ulishawahi kutuletea hata sukari kwa ajili ya malezi???Tuachie watoto wetu wa kike tutawalea hata wakizeekea nyumbani safii tuu kwa kuwa ni wa kwetu!!
Mbona ww uliye letwa na sitarehe ya mama na baba yako hauishi kwa hao wazazi wake?
 
Akili kubwa hii,swali la kujiuliza ni kwamba unamfukuza ili aende wapi??
Aende akaolewe na kujitegemea na awe na uwezo wa kujikwamua kiuchumi, Acheni uoga wafukuzeni msiwalundike lundike majumbani hovyo.. wana changia sana kuharibu mabinti wanaojielewa.

Mzazi ukisha mkingia binti yako kifua hawezi kuolewa ndio atakua anakataa wanaume wanao mposa na kuwajibu hovyo.. pia ikumbukwe mzazi kumkingia binti kifua ni kumwekea security kwamba hata akiolewa atarudi nyumbani na ndio maana hawadumu kwenye ndoa cz wanajua wazazi wapo..
 
Mnaanza kuwalazimisha? Ndo hivyo hawataki...
Fukuza watoto wako, wa kwetu hatutawafukuza na hata wasipoolewa ni sawa. Wanaume wenyewe adimu
 
Furaha ya ndoa kamwe haitakaa kuwa replace na kitu chochote kile
Waliojaribu kureplace ndoa na vitu vingine wamejikuta wanaishi kwenye upweke na kukosa faraja kwa hali ya juu sana na kumepelekea wasifurahie maisha

Navyoongelea ndoa siongelei ndoa ya kanisani au misikitini naongelea maisha ya mahusiano kwa ujumla wake
Unavyoongea ni kama vile ndoa zote ni paradiso ndogo. Huko ndoani kuna watu wametiwa ulemavu wa kudumu, kuna watu wamekatishwa uhai kikatili, kuna watu wapo jela kwa sababu ya matukio ya ndoani, kuna watu wamegeuka mizoga inayotembea kisa mambo wanayokutana nayo huko. Sikatai ndoa ni muhimu lakini hai - guarantee furaha kwa kila anayeingia...ni kama kubeti tu unaweza kula au kuliwa
 
Mnaanza kuwalazimisha? Ndo hivyo hawataki...
Fukuza watoto wako, wa kwetu hatutawafukuza na hata wasipoolewa ni sawa. Wanaume wenyewe adimu
Waoaji wapo wengi.. tatizo mnawafuga mwisho wa siku wanakua wamejazana nyumbani tena kwa dharau wanawaletea na vitoto ambao hawajui hata baba zao ni kina nani.. Acha mara moja hiyo tabia ya kuwa kingia kifua okoa kizazi na Fukuza akafunzwe na ulimwengu...
 
Katika vitu ambavyo siwezi kuvifanya ni kufukuza mtoto wa kike, mwanangu wa kike ataondoka nyumbani pale atakapoolewa tu ata akifikisha miaka 40 hakuna kuondoka nyumbani.
Kha sasa mwanao wa kike mpaka 40 yupo home sii hatari hiyo....humo ndani msinunue matango kabisaa🤣🤣🤣🤣🤣
 
Nyie mnaosema wanawake wanakataa Wanaume Ni uongo mtupu labda mnazungumzia maeneo ya vijijini lakini huku mjini Hakuna waoaji tuache uongo hata sisi tuna dada zetu tunajionea.
Kwa hiyo mzeya wee dada yako anapigwa de liboloz tuu waoaji hamna🤣🤣🤣🤣 dah poleni sana kumbe mnateseka hivyo
 
Mkuu mtoa Mada tafuta chakula uwape watoto wale mkuu kuwafukuza watoto wangu wa kike kwa kuwakataa wanaume uchwara ambao hamjakua kihisia na hamna uchumi mzuri siwezi

Mimi watoto wangu siwez kuwafukuza hata awe kiume au wa kike nyumbani ataishi miaka buku
 
My daughter will always be my daughter, whether she is 15 or 90...and my home is her home forever!

Ataondoka akitaka na atarudi wakati wo wote akitaka. This is her safe place akichoshwa na dunia huko anarudi kwenye usalama wa baba yake.

Aamue kuolewa au kutoolewa huo ni uamuzi wake!
For the moment i thought ur my dad....mwezi mmoja uliopita aliniambia maneno kama haya. Big up mkuu [emoji122][emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom