Maduka ya Dawa yaliyo nje ya mageti ya Hospitali za Serikali huwa na dawa muda wote lakini ndani ya Hospitali husika hamna dawa

Wewe ndio mwongo, unazifahamu taratibu za baraza la famasia? Pia maduka ya MSD yapo na dawa zina bei nafuu sana.
Kama ni hivyo kwamba MSD wanauza rahisi kwanini mnalalamika ? si uzeni rahisi ili hao maduka binafsi washindwe !

Kingine usichokijua ni hiki , Baraza la famasi mara kadhaa limeendesha semina kuwaasa wauza dawa kufungua maduka karibu na Mahospitali ambako ndio wateja wako wengi , kumbuka kwamba hawa ndio wawakilishi wa Wizara .
 
Kwani serikali yenu imekatazwa kuweka dawa mahospitalini , kwanini mnalaumu wengine ? Kwa taarifa yako ni kwamba Nesi au Daktari yoyote hawana uwezo wa kupanga Policy ya Hospitali yoyote , lawama wapelekeeni viongozi wenu , ndio wahusika wakuu
 
Mbona kwenye Hospital binafsi hukuti haya maduka ya dawa yamewekwa nje ya mageti yao?
 
Bila kupoteza muda ama kuumiza kichwa

Jibu ni"hizo ni biashara za watu" tu

Ova
 
RIB Tata JPM
 
Acha uongo ndugu. Watu tumeuguza e

Hapa umedanganya
Tuliouguza enzi za huyo unayemsema tuliendelea kupata dawa katika maduka hayo. Sijui lengo la uongo kama huu unalenga nini.
 
Toka umeacha sigara bwege unajitahidi kuandika, mwendazake aliweka maduka ya dawa ya hospital kwenye kila hospital sasahivi yale maduka nayo yana paracetamol yakijitahidi sana utakuta kuna drip
 
Nilikuwa kwenye kahospital kamoja binafsi nipo kwa dokta tena ndio mmiliki akaingia mtu kumuuzia dawa za serikali mbele yangu, sio waoga wale
 
umezoea kuongea uongo hilo ni tatizo kubwa
 
uhaba wa dawa muhim kwa wagonjwa ktik hospital za umma ndio wanaona wenye mitaji kma fursa madactor wa eneo husika ndio wanamiliki pharmacy kubwa around hospital akikuandikia dawa anakudirect tu nenda pale kama hauna bima na ukienda bima unaandikiwa tu na kupewa maelekezo nenda pharmacy ile utapata hivyo sio tatizo na wanasaidia sana kama dawa nzur inapatikana pharmacy za nje na ndan hamna kuna tatizo gan kama sio kushukru Hakuna jmbo la umma likanyooka kila sehem majanga

Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app
 
Anzia MSD kama wanapeleka madawa kwa wakati ndipo ulete lawama

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Nilikuwa kwenye kahospital kamoja binafsi nipo kwa dokta tena ndio mmiliki akaingia mtu kumuuzia dawa za serikali mbele yangu, sio waoga wale
Ndo maana kila wakati Hospital za umma hakuna dawa, hii ni tofauti na Hospital za binafsi, ukiritimba mwingi
 
Ukosefu huu unatokana na upigaji ndani ya hizo hospitali
 
Yani mentality za kishamba ziliwateka kipindi kile.

Kwanza nani alikuambia kipindi cha Magufuli dawa zote zilipatikana hospitali?

Kingine serikali kwanini isishindane na sekta binafsi katika ushindani huru tu bila kuwafanyia hujuma ya wazi wazi sekta binafsi kwa mizengwe isiyo na akili.

Ila nimeamini kukosa exposure ni jambo baya sana karibuni kwa watu huu muone tofauti sio mnajazwa uongo bila facts mnajaa.

Mwisho niulize hivi serikali ikitaka kufanya kila kitu itaweza?
 
Lile jamaa mtalikumbuka tu..😀
Aliwajengea hofu tu watumishi lakini huduma still zilikuwa mbovu.
Bila pesa hakuna matibabu.
JK unatibiwa kwanza pesa baadae.control number kwanza matibabu baadae.
 
Morogoro referral hosptal. Haina hadhi ya hosptal ya rufaaa utumbo mtupu. Dawa nyingi hawana mpaka mtu ufunge safari kwa msafiri sababu ya bima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…