Maduka ya Dawa yaliyo nje ya mageti ya Hospitali za Serikali huwa na dawa muda wote lakini ndani ya Hospitali husika hamna dawa

Maduka ya Dawa yaliyo nje ya mageti ya Hospitali za Serikali huwa na dawa muda wote lakini ndani ya Hospitali husika hamna dawa

Mada ni kuwa inakuweje maduka nje ya hospitali yawe na dawa lakini ndani ya hospitali hakuna dawa wala gloves?

We umeangalia hospitali moja mi nimefanya mzunguko wa hospitali nyingi za serikali.
Isitoshe pia kusema sisi ambao tunakaa na manesi jirani wanavyowauzia dawa majirani wanawazunguka, kila aina ya dawa wanazo na nyingi za watoto,.
Aisee
 
Hebu ileza maduka ya nje yanakuwaje chanzo cha ukozefu wa dawa hospitali. Serikalo inasema mama ni bure Lakini hivyo vitu vya bure huwa serikali yenyewe haivileti sasa kosa la nani kwa mfano

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu..hapa umeongea point nzuri..ambayo inaitaji mjadala mpana..kutolewa dawa bure na upatikanaji usio na mashaka wa hizo dawa za bure kwenye hivi vituo vyetu vya afya..kwa maoni yangu hii ni changamoto kubwa sana kwa vituo vingi vya afya kuweza kuendesha kazi zao za kila siku kwa ufanisi..
 
Hii nchi ina Wapumbavu wengi mtoa mada akiwa mmojawapo

Upatikanaji wa dawa ndani ya Hospitali hauna uhusiano na uwepo wa dawa katika maduka yaliyoko nje ya Hospitali. Dhana hiyo ni moya ya akili fupi alizopata kuwa nazo yeyote aliyefikiria.

Serikali iboreshe mifumo yake ya upatikanaji wa dawa kupitia MSD, Wazabuni binafsi na taratibu zingine ili Vituo vyake viwe na dawa.

Unapoanza kushangaa kwa nini Maduka ya nje ya Hospitali yana dawa na na Zahanati au Hospitali hakuna kwani chanzo chao ni kimoja? Taratibu za manunuzi kwa Hospitali zinafanana na taratibu za manunuzi za mtu binafsi? Famasi Binafsi wanaweza at any time t wakaenda Kariakoo au kwenye Duka lolote la Jumla wakanunua mzigo aidha kwa Cash au Mali kauli wakaweka dukani, je taratibu za manunuzi ya Umma yanaruhusu hilo?

Hii nchi Wapumbavu ni wengi sana kuliko tunavyodhania.
Nchi hii imejaa wapumbavu. Luckily mimi siyo Daktari.

Walahi, mimi ningekuwa Daktari ningekuwa nawaandikia hawa watu fawa yoyote.

Maana inaonekana wanachotaka ni Dawa tu. Nyamabafff
 
Mtoa mada Muongo kichizi hata kipindi cha magufuli hali ni ile ile tuliuguza sana temeke pale...tena usiku ndo kabisa hakuna huduma 2019 hata gloves zilikua dili hospital za serikali
Wakati wa Magufuli Basket Fund haikutoka hata 100 mbovu, hospitali zilipitia kipindi kigumu sana.

Unfortunately hakuna mjuaji yeyote aliyebinua kimdomo kuongea🤣🤣🤣
 
Hii nchi ina Wapumbavu wengi mtoa mada akiwa mmojawapo

Upatikanaji wa dawa ndani ya Hospitali hauna uhusiano na uwepo wa dawa katika maduka yaliyoko nje ya Hospitali. Dhana hiyo ni moya ya akili fupi alizopata kuwa nazo yeyote aliyefikiria.

Serikali iboreshe mifumo yake ya upatikanaji wa dawa kupitia MSD, Wazabuni binafsi na taratibu zingine ili Vituo vyake viwe na dawa.

Unapoanza kushangaa kwa nini Maduka ya nje ya Hospitali yana dawa na na Zahanati au Hospitali hakuna kwani chanzo chao ni kimoja? Taratibu za manunuzi kwa Hospitali zinafanana na taratibu za manunuzi za mtu binafsi? Famasi Binafsi wanaweza at any time t wakaenda Kariakoo au kwenye Duka lolote la Jumla wakanunua mzigo aidha kwa Cash au Mali kauli wakaweka dukani, je taratibu za manunuzi ya Umma yanaruhusu hilo?

Hii nchi Wapumbavu ni wengi sana kuliko tunavyodhania.
Huu ndio ukweli but mchungu
 
Kilimani Pharmacy pale Mawenzi Hospital Moshi. Nilizungushwa sana wakati nauguza. Kila kitu kuanzia mionzi hadi dawa nililazimika kwenda pale sababu hapo hospital wameshatengeneza network ya kupiga pesa. Utasubirishwa pasipo sababu ya msingi huku ukiambiwa kama unaweza nenda kapige hapo kilimani uje doctor akupe huduma. Dawa zote unazoandikiwa hazipo, ila utaambiwa nenda hapo kilimani wanazo
Usiwalaum wanakuambia ukachukue dawa kiliman pharmacy watalum wenye jukum la kuakikisha dawa inapatikan katkka hospital hao wenye pharmacy nje wanatusaidia sana sema kila mmoja anasema kwa utashi wake utakuta pharmacy wana dawa nzur currently lkin hospital za umma wana dawa za kawaida oldest kwa ntumiaj wa bima dawa nzan malalamiko yetu kiini cheke ni wasiotumia bima all in all uzembe wa wakuu wa hospital za umma kuanzia mganga mkuu mpharamacia na uhab wa dawa msd ndio wenye maduka bianfs wanatumia kma fursa big up kwao wanatusadia sana kwenye dharura

Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app
 
Mbona kwenye Hospital binafsi hukuti haya maduka ya dawa yamewekwa nje ya mageti yao?
Huruhusiwi kuandika dawa nje na orodha ya dawa zinazopatikana kwenye hospitali binafsi, ukikaidi mwisho wa mwezi utauona mchungu.
 
Umedanganya , Sheria ilimzuia Magufuli kufunga maduka ya dawa karibu na Hospitali , akaamua kuanzisha maduka ya MSD ili kuyashinda maduka binafsi , huku akisahau kwamba kila wodi ya Wagonjwa kule ndani , sewahaji , Mwaisela nk zinayo maduka humo humo vyumbani , kifupi alichemsha vibaya .

Maduka ya dawa hukaguliwa na Mamlaka ya chakula na dawa , hakuna dawa ya serikali inaweza kuuzwa mle , maana dawa zao zina nembo
Mbowe vip hali yake mkuu?
 
Issue ya upatikanaji wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya ni changamoto ya nchi nzima, ukifuatilia vizuri utaona malalamiko yanafanana.

Nafikiri sera, na miongozo ya upatikanaji wa dawa iliyopo haifai kwa sababu imeshindwa kutatua kero za wananchi,

Wenye dhamana wanapaswa kuangalia suala hili upya kwa macho matatu.
 
Acha kupotosha, hali ilikuwa ile ile hata kwenye hiyo awamu ya tano. Niliuguza sana madogo hospitali ya Wilaya ya Meru, kipindi cha awamu ya tano...dawa nyingi za maana ulikuwa unaenda Tengeru kutafuta pharmacy binafsi ukikosa inabidi uende mpaka USA river
 
Kipindi cha awamu ya tano Mheshimiwa Raisi Magufuli alipiga marufuku sana ya maduka yaliyo nje ya hospitali za serikali, kwani ilionekana kuwa hayo maduka ndo chanzo cha Kukosekana dawa ndani ya hospitali hizi za serikali.

Wengi tulishuhudia huduma nzuri pamoja na upatikanaji wa dawa ndani ya hospitali lakini leo mambo yamejirudia pale pale.

Leo hii Mwananchi wa kawaida anaona ni bora akapate huduma katika Hospitali binafsi kuliko ya serikali kutokana na huduma mbovu zitolewazo katika Hospitali za umma.

Ndani ya hospitali za serikali mara nyingi utapimwa vipimo lakini baada ya majibu kuja utaandikiwa paracetamol na dawa nyingine utaambiwa kanunue duka lililopo nje ya geti.

Kwa upande wa kina mama wanaojifungua tunaambiwa ni bure lakini Hospital nyingi za umma huwa wanalipishwa, huku wajawazito wakiamriwa waje na vifaa vya kujifungulia kama vile pamba. Gloves nk.

Wizara ya afya wafuatilie na pia wawe wakali maana Hospitali za umma zimekuwa changamoto sana kwa wananchi wa kawaida.

Kabla ya malalamiko yoyote twende tukajifunze mfumo wa ununuzi wa dawa na vifaa tiba kwenye hospital zetu na control system yake. Ni nani anahysika na mnyororo mzima. Bajeti ni kiasi gani na inatolewa kiasi gani?

Msisikie hoyahoya huko nje na kusema ilikuwa hali nzuri, bali watu walizimwa kusema. Ulikuwa unawekewa kaa la moto mdomoni lakini unatakiwa useme ni mkate.

Tutafakari pia kwenye:
1: Elimu
2: Afya
3: Ujenzi
4: Sheria
5: Kilimo
6: Biashara ie Bank
7: Mawasiliano ie. Simu

Ni wapi serikali inafanya na kuishinda sekta binafsi kwa ujumla kwenye nchi hii? Haya mambo yanahitaji kushirikiana na kwekeana mazingira mwafaka.

Vitu vya serikali huwa vinaelea hapo kati kutokana na kubeba jukumu la kutoa huduma zaidi kuliko biashara hivyo kuhitaji imput kubwa. Je serikali inaweza kusustain huo mzigo?? Hapo unahitaji mfumo imara na si mtu imara.

Watu walioko kwenye hizo sekta hawajitumi ipasavyo. Kwani hawategemei moja kwa moja malipo toka pale walipo.
Ni wafanyakazi wangapi wa serikali wana objectives na zinakuwa reviewed kila mwisho wa mwaka na kuulizwa utimizaji wake na kuweka mpya au ndo ile theoretical OPRAS.

Je uliwapa vitendea kazi?
BRN ilifia wapi?? Hata utekelezaji wake ulionekana mzigo kwa serikali kutokana na hitaji lake.

Maduka ya dawa nje ya hospitali ni ya kushukuru, kwa kuwa yanasuppliment deficit kwenye institution hizo. Ukitaka ujue umuhimu wake yafunge yote kwa mwezi mmoja tu.

Kuna wakati watoa huduma ya afya wanagawiana gloves na kukaa nazo mifukoni kutokana na uchache wake, si kwa kupenda. Fikiria mama mmoja anaweza kuhitaji kupimwa mara nne kabla ya kujifungua. Nawe umepewa gloves kumi kwa siku???

Tunasema huduma bure kwa watoto chini ya miaka mitano na wazee, uliza hospitali inayopeleka idadi ya hao watu wanaopata huduma bure na kupewa bujeti yake ili kufidia deficit yake kila mwezi na kupewa hela hiyo kama utaipata. Hili ndilo linalofanya ukifika dirishani unaambiwa kanunue hii dawa ya mtoto au mzee.
 
Huruhusiwi kuandika dawa nje na orodha ya dawa zinazopatikana kwenye hospitali binafsi, ukikaidi mwisho wa mwezi utauona mchungu.
Siyo kwamba huruhusiwi kuandika.

Ila ukiandika Dawa ambazo hazipo store ya hospitali maana yake mgonjwa akanunue ndio utapata lawama kama hizi.

Kwahiyo, inadhauriwa Umwandikie mgonjwa Dawa zilizopo store ili kukwepa lawama kama hizi.
 
Acha kupotosha wewe, lini maduka binafsi yaliyoko nje ya hospital yalifungwa?

Yaani alikuja na mbwembwe nyingi eti maduka yote yaliyopo nje ya hospital yafungwe, wakamtazama tu, hakuna aliyefunga , na hakuna kilichofuata!

Suluhisho ni kuweka dawa hospitalini tu, sasa ukiyafunga halafu bado dawa kwenye hizo hospital hakuna, kuna nini?ule ulikuwa ni UKURUPUKAJI TU, na jiwe na diblo waliangukia pua.
Huu msamiati mpya, diblo ndo nani naye huyu!
 
Dunia ya sasa hivi ukipenda vya bure na dezo utaishi maisha magumu mno.
Ni kweli mkuu ila pia dunia ya sasa usipojitambua ukawa na ujinga mwingi unaweza ukalipishwa kiingilio na mkeo kwenye nyumba yako ambayo umeinjenga mwenyewe.

Huwezi kulipa kodi na tozo halafu ulipie na huduma ambazo kimsingi zilitakiwa ziboreshwe na kodi ambazo umelipia.

Serikali haiombwi kuboresha huduma kwa hisani ni wajibu wake kuboresha ila kwa wajinga wajinga wanaweza kuhisi kuwa eti kutoa rushwa ni lazima ili upewe huduma.
 
Chifu Hangaya alipoingia madarakani kwenye zile ziara za kwanza kwanza alikutana na Baraza la Maaskofu katoliki, nakumbuka moja ya changamoto walizomweleza ni kuwa "kutokana na serikali kuboresha huduma za afya sasa hivi hospitali zao hawapati wateja na wamefikia kiwangi cha kushindwa kuwalipa watumishi wao mishahara" wakaomba waondolewe Kodi kwenye huduma za afya nk!

Muda huu Hangaya alikutana nao tena akawaukiza vipi wateja wanapatikana? Nadhani watamwambia "Asante mama kwa kutuongezea wateja!" maana yake ni kwamba huduma za afya kwenye hospitali na vituo vya umma zinaekekea kufa kabisa, ni suala la muda tu!
 
Kipindi cha awamu ya tano Mheshimiwa Raisi Magufuli alipiga marufuku sana ya maduka yaliyo nje ya hospitali za serikali, kwani ilionekana kuwa hayo maduka ndo chanzo cha Kukosekana dawa ndani ya hospitali hizi za serikali.

Wengi tulishuhudia huduma nzuri pamoja na upatikanaji wa dawa ndani ya hospitali lakini leo mambo yamejirudia pale pale.

Leo hii Mwananchi wa kawaida anaona ni bora akapate huduma katika Hospitali binafsi kuliko ya serikali kutokana na huduma mbovu zitolewazo katika Hospitali za umma.

Ndani ya hospitali za serikali mara nyingi utapimwa vipimo lakini baada ya majibu kuja utaandikiwa paracetamol na dawa nyingine utaambiwa kanunue duka lililopo nje ya geti.

Kwa upande wa kina mama wanaojifungua tunaambiwa ni bure lakini Hospital nyingi za umma huwa wanalipishwa, huku wajawazito wakiamriwa waje na vifaa vya kujifungulia kama vile pamba. Gloves nk.

Wizara ya afya wafuatilie na pia wawe wakali maana Hospitali za umma zimekuwa changamoto sana kwa wananchi wa kawaida.
Hata wakati wa jpm mfumo ulikuwa huu huu
Dawa hospital hakuna ila maduka ya dawa nje
Zipo!
Nchi ngumu hii kuanzia juu mpaka chini

Ova
 
Back
Top Bottom