Ndugu watanzania wenzangu salamu sana..
Ebu tuweke siasa pembeni dakika chache tu tufikiri kidogo tu.. Naweka UCCM wangu pembeni hapa naomba na UCHADEMA ukae pembeni hapa..!! Let's talk serious issues..!!
Kwa miaka 2 na nusu tu, Mh. Rais Magufuli kafanya haya..
1: Kakomesha
rushwa nchini kwa kiwango kikubwa mno mnoo..!!
2: Mafisadi papa wanashughulikiwa
3: Watumishi wenye vyeti feki wametolewa na kuendelea kuhakikiwa wengine..
4: Wizi wa kutisha Bandarini, Madini, TRA, Uwindaji haramu, etc umedhibitiwa haraka..
5: Ujenzi wa Reli ya Umeme wa kisasa kabisa umeanza..
6: Ujenzi wa Bwawa kubwa la umeme Stigler's Gorge 2,100 MW umeanza..!!
7: Kufufua Shirika letu la Ndege la ATCL, wote tumeona ndege mpya zimewasili tayari na zingine zitakuja very soon..!! Na zinaruka na ni marubani wazawa wanarusha..!!
8: Fly overs, ya TAZARA 98% tayari soon watafungua..!! Ubungo Interchange ujenzi mkubwa unaendelea..
9: Barabara za lami sehemu mbalimbali zinaendelea kujengwa..
10: Jengo la abiria la kisasa kabisa Uwanja wa Julius Nyerere International Airport Dar es Salaam karibia kumalizika...TANROAD wamefanya kazi nzuri mno mnoo.. Na viwanja vingi vya ndege vinaendelea kujengwa.. Runways kadhaa ziko under construction..!!
11: Serikali kuhamia Dodoma, hili ni suala kubwa sana sana, Mh. Rais kafanya kwa vitendo..!!
12: Majambazi wamemalizwa ndani ya muda mfupi tu na polisi waliokuwa sio waaminifu wameondolewa haraka..!! Siku hizi ujambazi umepungua sanaaa..!!
13: Wanyonge wenye haki zao wanazipata siku hizi, mfano hati miliki za ardhi, matajiri hawanyanyasi wanyonge tena, etc
14: Wafanyabiashara, kampuni za simu, banks sasa hulipa kodi halali bila ujanja ujanja wa kukwepa kodi..!!
15: Kufutwa kwa kodi ya Motor Vehicle licence sasa imeingizwa ktk mafuta, yaani utalipia halali kabisa, kama gari lako halitembei hulipi kodi kwa maana hutanunua mafuta, utalipia kodi tu ukinunua mafuta na imeingizwa humo, hii imeondoa sana usumbufu mabarabarani na kuongeza mapato sana kwa serikali..!!
Na mengine mengi mengiiiii mazuri..!!
Swali: Hivi ukitumia akili ya kawaida tu, unapata wapi uzalendo au hata mawazo ya kupinga haya? Sisemi Mh. Rais wetu ni mtakatifu sana, hapana, ni binadamu, ana madhaifu kama mwanadamu yeyote yule, sasa mtu anayeweza fanya haya yoooote ndani ya miaka 2 na nusu tu, unampinga kwa lipi? Utakuwa ww sio mtanzania au mzalendo au wakala wa shetani usiyetakia mema nchi yetu kumpinga Mh. Rais wetu.. Mawakala wa shetani wasioipenda nchi yetu ndio wanaweza pinga maendeleo haya..!!
Mungu mbariki Mh. Rais wetu, Mungu ibariki Tanzania..!!View attachment 828706