Mafanikio ya Rais Magufuli 2015 - 2021
Mkuu tunazungumzia ujumla wa mambo, wewe uliyoyataja ni yale madogo madogo
Nimekaa TRA toka saa 3 hadi saa 4:30 pale Samora hawan network nilitaka ku renew leseni yangu ya udereva. Hata sasa nimempigia dogo nilimwacha pale bado hakuna network. So nchi hii bado sana pamoja na pambio zote mnazoimba.
 
Nimepata fursa ya kuzunguka mikoa kadhaa mambo yamebadilika san,kila nilikopita watu wapo bize kweli kweli vijana kwa wazee

Huko shambani ndio usiseme kila kijiji unapita unakuta makundi kwa makundi wanaotesha mazao

Ile tabia ya watu kukaa bar saa moja asubuhi kwa kisingizio cha kutoa hangover hakuna tena, hangover inatolewa baada ya kazi

Toka Magufuli aingie madarakani sioni tena vijana wakikaa vijiweni na kucheza bao Muda wa kupambana

Huyu ndio Rais tuliyemlilia sisi Watanzania amebadilisha mtazamo wa Watanzania wengi mno wamekuwa wabunifu

Kabla ya Magufuli vijana waliokuwa wanaenda chuo walikuwa wakipata pesa za mkopo zinaishia kuzitapanya lkn sasa vijana wanaenda chuo wakipata mkopo hutunza pesa ili wajiajiri baada ya kumaliza chuo
Vijana wengi wasomi wamebadilika sana kimtazamo wabahili kweli kweli wanawaza maendeleo
Kumbe tulikuwa tunahitaji mtu mwenye uthubutu tu kubadilisha mind set za vijana


Ahsante Magufuli umetubadilisha wengi Endelea hivyo hivyo tuwe wachangamfu kwenye fursa kama wanigeria
Hata mimi nakuunga kidole cha kati
 
Kabla Ya Magufuli Pale Hospital Ya Mkoa Wa Ruvuma Nikifika Mapokezi Card Nilikua Nalipia Tsh. 1000. Baada Ya Kuja Serikali Ya Awamu Ya Tano Saizi Card Hiyo Hiyo Nalipia Elfu Tano.

Hongera Sana Serikali Ya Awamu ya Tano Kwa Kutujari Wanyonge.
 
Ni kweli mtoa mada, binafsi ninafanya kazi za ziada ambazo awali sikutaraji kuzisimamia mwenyewe. Muhimu tu ajenge mifumo na taasis imara tukianza na katiba bora, na kusimamia na kuiheshimu.Atakuwa kiongozi bora zaidi katika historia ya taifa letu.
 
Upo sahihi Mkuu
Tuendelee kumuunga mkono mh Rais Kwa uchapa kazi
Ni kweli mtoa mada, binafsi ninafanya kazi za ziada ambazo awali sikutaraji kuzisimamia mwenyewe. Muhimu tu ajenge mifumo na taasis imara tukianza na katiba bora, na kusimamia na kuiheshimu.Atakuwa kiongozi bora zaidi katika historia ya taifa letu.
 
Back
Top Bottom