Mafanikio ya Rais Magufuli 2015 - 2021
Vyura mitaani walikuwa kero kubwa mtu ilikuwa vigumu kulala hasa ukiwa na nyumba jirani na barabara yenye mashimo ambayo mvua ikinyesha yalikuwepo madimbwi ambayo vyura walikuwa wakiibuka wakipiga miyowe usiku kucha Kama wamelewa gongo au wamevuta bangi hivyo kukosesha usingizi wakazi wa karibu na maeneo hayo.

Baada ya barabara za lami kujengwa mitaani tunalala usingizi mnono .Vyura wametoroka mitaani kukimbia serikali ya awamu ya tano mitaani.

Na Kama mjuavyo chura na barabara ya lami ni vitu viwili tofauti huwezi ona maruhuni chura akiwa juu ya barabara ya lami iwe kukaa au kuvuka barabara ya Lami.Magufuli kawashikisha adabu

Awamu ya tano hoyee
 
Ukipita maeneo mengi uswahilini ya Dar Yana taa za barabarani usiku ni Kama uko new York marekani.Uswahilini Dar mitaa inawaka taa za uhakika , masaki ,mikocheni na mbezi beach hawaoni ndani.Uswahilini Dar kunameremeta Kama London usiku

Magufuli kaamua kuwajali wapiga kura walio wengi.

Maeneo ya wenye nazo Kama mikocheni,masaki,msasani ,mbezi beach nk huwa wengi hawapigi kura .Wapiga kura wako uswahilini .Asante Magufuli kujali
 
Mbona hiyo miradi Ni ya world bank Dar es Salaam Metropolitan Development Project


Miradi yote inayoendelea dar Ni pesa za hao mnaowaita Mabeberu chini ya mradi wa Dar Es Salaam Metropolitan Development Project ambapo pesa zinatoka Benk ya dunia ... Acheni kupotosha.
IMG_20191111_151055.jpeg
 
Cha ajabu ni kwamba kakimbia kelele za vyura kwa kufunga ofisi badala ya kusubiri kutetewa na barabara nzuri alizojenga.
 
Kwani unafikiri hao World Bank wanaweza kuja tu kufanya miradi hapa TZ. Kwanza ni nyinyi mliokuwa mnashangilia kuwa tumenyimwa misaada na WB kwa sababu ya Sheria ya Takwimu?
Sasa hapo umeandika nini , Idiot.
 
Hapo Lumumba mmekula mchana kweli??
Hawajala lakini kusifu awamu hii kumekuwa lazima ili ule maana hiyo ndio hapa kazi tu ingawa wengi wanasifu na kusifu kwa mazoea wanalala njaa. Wengi wamegundua hili ndio maana sifa zimepungua mpaka viongozi wanazunguka na ma-MC wa kuhamasisha wananchi wapige vigelegele kwa viongozi kwenye mikutano ya hadhara. Bila MC mikutano ya viongozi inakuwa kama ya kilio maana yanayosemwa nchi nzima wakati wote SGR, ATCL na Stigler Gorge tu. Wananchi wamechoka kusikia wanataka kupata huduma siyo kusikia mipango, mipango mkakati, michakato au mabilioni yatakayotumika kukamilisha miradi.
 
Kamuulize Mdee na kiburi chake na mwaka kesho anafungasha virago!

Magufuli hawezi siasa za ushindani wala hatakaa aziweze maana hana mvuto wa kisiasa, matumizi ya mabavu pekee kwa kutumia madaraka yake ndio yanaweza kuwapa wanaccm madaraka. Hatutashangaa maagizo yake ya kumpora ushindi Mdee. Hata huu uhuni kwenye uchaguzi huu wa serikali za mitaa ni maagizo yake.
 
Back
Top Bottom