Uchaguzi 2020 Magufuli akiwa Songwe: Msipomchagua Silinde sileti maji Tunduma

Uchaguzi 2020 Magufuli akiwa Songwe: Msipomchagua Silinde sileti maji Tunduma

Wananchi wote walipaswa kumwambia usilete hayo maji, kwani wameishi muda gani bila maji? Hapo kukomesha toka diwani, mbunge na rais unachagua upinzani.hivi maccm wanadhani hivo vimiradi uchwara visipokuwepo wananchi wanaogopa? Jpm kwani atakuwa milele
Labda kwa kuwa Lissu kaidindishia TUME .....!!
Kasoma upepo songwe, na tunduma amehutubia wengi waliosombwa vijijini
 
mwaka huu mkikosea kuchagua mbuge wa upinzani imekula kwenu miaka 5, mtasahauliwa kwa kila kitu,
dawa pekee mwaka huu ni kuchagua Rais wa CCM Wabunge wa CCM na Madiwani wa CCM mkifanya hivyo mtakuwa mmejihakikishia maendeleo.vinginevyo tusije kulaumiana
 
Sasa hivi ni vitisho. Yaani wanyimwe maji kwa kuwa tu watamkataa Silinde? Hii keki ya Taif haiwezi kuwa inagawanywa kwa matakwa ya mtu mmoja
 
Hivi kwa nini huyu mtu hawezi kujifunza kitu hata kidogo.

Kwa fikra zake bado anadhani watu watapigia CCM kura kwa vitisho vya aina hii?

Kama yeye anadhani serikali ijayo itakuwa yake, basi mwache aendelee kulala usingizi wa pono. Kama anategemea kura za maruhani, safari hii hazipo!
 
Hilo ni pingamizi tosha hata kama atachaguliwa. Akumbuke Igunga kipindi kileeee
Bila kumchagua mgombea wa CCM hatutajenga daraja mto Mbutu katika uchaguzi ule alishinda mgombea wa CCM upinzani ukapeleka pingamizi mahakamani mbunge aliyeshinda akatenguliwa ubunge naye alikata rufaa akarudishiwa ubunge wake na Mahakama ya rufani
 
mwaka huu mkikosea kuchagua mbuge wa upinzani imekula kwenu miaka 5, mtasahauliwa kwa kila kitu,
dawa pekee mwaka huu ni kuchagua Rais wa CCM Wabunge wa CCM na Madiwani wa CCM mkifanya hivyo mtakuwa mmejihakikishia maendeleo.vinginevyo tusije kulaumiana
Dawa ni kunyima kura ccm kabisa, kwani magu atakaa milele?
 
Mbona ametoa mapema siri zake za kwamba hatokubali kushindwa Urais. Hii inawasaidi wapinzani kujipanga zaidi.

Anachosema sasa hivi ni sawa sawa na GSM kuwaambia wachezaji wa Yanga kuwa hatatoa zawadi ya pesa kwa wachezaji watakaokosa kwenye kikosi kitakachowafunga Simba tarehe 28.10.
 
'Lakini msinichanganyie, mkiniletea hao, nasema maji hamyapati. Lazima tuambizane ukweli na mimi nazungumzaga ukweli.'

Na anasema maendeleo hayana Chama

Muongo msimuamini!!!
 
Sasa nimeshaelewa, anachosema Lissu kuhusu mamlaka za majimbo.

Ok, asijaribu kwenda tunduma kudai kodi
Aondoe na watoza ushuru wake.

Duu! Huu ni unyanyasaji mkubwa sana, utasema hela anatoa nyumbani kwake!!!
Huyu hatufai kabisa
 
Yeye ni Raisi bado anapokea kero toka kwa wanachi akiwemo Lisu na kuzifanyia kazi

Kuna kero ingine? mwambieni Lisu aendelee kuzitoa ili Raisi aliyeko madarakani azifanyie kazi
Kwahiyo bunge lililovunjwa hasa ccm hawakufanya vyema siyo
 
Back
Top Bottom