Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

Magumu yetu Viongozi wa Upinzani mkwepe lawama vipi?

SAMIA& Mwigulu wafanya biashara wengi hawalipo kodi,na Maafisa wa TRA kazi yao Ku under evaluate nankuchukua rushwa huku wakilipwa mishahara minono.
Nashauri VAT iongezeke hadi 30% na corporate tax iwe 45% hii Nchi inachezewa sana na Wafanyabiashara.
 
Wapi analaumiwa mtu? Mbona iko wazi? Uko madarakani huna sera au ufumbuzi toka wachukue wengine.

Hili lina apply kote serikalini na upinzani. Kama kumtoa Mwigulu hatua ya kwanza ni kuanza na wewe uliye hodhi namna yetu ya kulianzisha tatizo liko wapi kuanza na wewe?
Sera zipo nzuri na zinafanya kazi,kama Sera zisingekuwepo Nchi ingekuwa bankrupt.Nampongeza Mama kwa kuupiga mwingi,kama una uchungu hata wewe unaweza organize maandamano hapo ulipo.
 
Acha wakae kimya wameteseka sana awamu iliyopita wakati sisi tulikaa kimya waliteseka pekee yao
Hakuna aliyekaa kimya, walioteseka ni Mbowe na Lissu, na walipata michango ya hali na mali kuanzia matibabu ya Lissu hospitali mpaka michango ha mawakili kwenye kesi ya Mbowe, hakuna aliyekaa kimya.
 
Wapinzani kaeni kimya kabisa waacheni watz wapambane na hali zao. Goli lipo wazi 2025 ni nyie tu mfunge au mbutue ccm hawana kipa.
 
Hakuna aliyekaa kimya, walioteseka ni Mbowe na Lissu, na walipata michango ya hali na mali kuanzia matibabu ya Lissu hospitali mpaka michango ha mawakili kwenye kesi ya Mbowe, hakuna aliyekaa kimya.
Walipotaka watz waandamane nani alitoka?
 
SAMIA& Mwigulu wafanya biashara wengi hawalipo kodi,na Maafisa wa TRA kazi yao Ku under evaluate nankuchukua rushwa huku wakilipwa mishahara minono.
Nashauri VAT iongezeke hadi 30% na corporate tax iwe 45% hii Nchi inachezewa sana na Wafanyabiashara.

Hapana VAT iwe 70% na Cooperate Tax iwe 90%, hamna namna

Kuwe pia na kodi ya kuishi kwa siku!! Kwa siku nashauri kila mtu aliyepo kwenye kaya achangie 5000tsh, Taifa haliendelii bila kodi!! Na ole wako usipotoa labda uhamie Somalia
 
Acha wakae tu kimya na wenyewe ni binadamu wamepiga kelele sana, watanzania wakaishia kuwadharau na kuwaona kama wendawazimu au waliokosa cha kufanya!!

Kwa sababu walichokuwa wanapigania ni kwa ajili ya wote lakini wakaonekana wehu, sasa acha watawala wafanye watakacho mpaka akili ziwakae sawa!!

Siku mkiambiwa bungeni kunahitajika kuwa na wapinzani wengi sana ili sheria za hovyo za kumgandamiza mwananchi zisipitishwe kirahisi muelewe wanaamanisha nini!!

Wakipiga kelele tunahitaji katiba mpya kwa ajili kuweza kuweka dira mpya ya nchi yetu muelewe wanamaanisha nni!!

Watawala kamatieni hapo hapo,, ongezeni kodi zaidi, wakihoji waambieni waende Somalia kabisa,, hamna namna!!
Nakazia ✍️✍️✍️
Ili next time wananchi wakiambiwa ni muhimu wapinzani kuwemo Bungeni waelewe, siyo kuleta zile kauli za kihuni kama:
'...wapinzani walituchelewesha sana...!'
 
Hapana kwa sasa wakae kimya kabisa!! Acha kwanza mtanzania ajitambue!! Hakuna kitu kigumu kama kumpigia mbuzi zeze acheze!! Ni sawa na kupaka upepo rangi!!

Nasema waongeze kodi zaidi na zaidi, mfumuko wa bei uende juu kabisa!!! Hadi mtanzania akili itakapo mkaaa sawa aamke kwenye huo usingizi wa pono!!
Kuna majukwaa ya aina nyingi kwenye kufikisha ujumbe, mwanasiasa anao uwanja mpana zaidi wa kusemea ikiwemo majukwaa, tofauti nasi tunaotegemea mitandao ya kijamii pekee.

Hizi nguvu mbili zikiunganishwa ni rahisi zaidi kufikia malengo, lakini kusema nguvu moja isitumike ibaki moja pekee huko ni kujichelewesha kuyafikia malengo.

Wao kukaa kimya kuyasemea matatizo yanayoikumba jamii waliyopo basi hata uwepo wao hautakuwa na maana yoyote kama hauisaidii jamii husika, wacheni mihemko kwenye haya mambo.
 
Acheni janja janja nyinyi. Wapinzani mliwaita wasaliti na mkawashawishi waunge mkono juhudi za mwendazake wengi wakahama mkafurahi sasa mnataka nini tena?

Maandamano muanzishe ccm wenyewe huko ndani kwani mkianzisha nyie hayatakuwa maandamano?
 
Acha wakae kimya wameteseka sana awamu iliyopita wakati sisi tulikaa kimya waliteseka pekee yao
Kama kipindi hicho ilikuwa ukiongea unapitia mateso ila wao wakachagua mateso kwa kuongea ni ajabu hivi sasa hakuna mateso kwa kuongea halafu et wao ndio wamechagua kutokuongea.
 
We sio mzima kweli,yani asimie a step down kwa kuwa wewe umandika Uzi,hivi huoni mfano hata huko Sir lanka?.
Asiyekuwa mzima mbona utakuwa wewe?

Unadhani Srilanka hakukuwa na viongozi na hata waratibu?

Usione vimeundwa ..
 
Walipotaka watz waandamane nani alitoka?
Unaonekana ni sehemu ya tatizo, hufanyi chochote hapo ulipo, halafu bado hutaki na wengine wafanye chochote, wewe ni mfano wa fikra dumavu za hili taifa zilizo mtaji wa CCM.
 
Acheni janja janja nyinyi. Wapinzani mliwaita wasaliti na mkawashawishi waunge mkono juhudi za mwendazake wengi wakahama mkafurahi sasa mnataka nini tena?

Maandamano muanzishe ccm wenyewe huko ndani kwani mkianzisha nyie hayatakuwa maandamano?

Ukisema "mliwaita" unakusudia kuwasema kina nani hao waliowaita wenzao? Kwanini usiwe wewe ndiye mwuaji nguli watu hivyo?

Vicious cycle taslimu. Yaani ujinga endelevu si ndiyo huu sasa?

Tufanye waliitwa wasaliti hivyo sasa wamenuna. Basi si wapishe waingie kina Mtikila, Malema, Seif, Nyerere, Tutu na wa namna hiyo wasiokuwa na utoto kama unaoona wewe ni mali mno?

Kwamba:

"Maandamano muanzishe ccm wenyewe huko ndani kwani mkianzisha nyie hayatakuwa maandamano?"

Kama namwona Mwigulu akikushangilia kweli kweli. Kama si nduguyo yumkini wewe ni mfuasi wake nguli kabisa.
 
Unaonekana ni sehemu ya tatizo, hufanyi chochote hapo ulipo, halafu bado hutaki na wengine wafanye chochote, wewe ni mfano wa fikra dumavu za hili taifa zilizo mtaji wa CCM.
Mtu mmoja pekee hawezi leta mabadiliko kama haungwi mkono na wengine.Tozo ziongezwe
 
Wapinzani wasilaumiwe tena naomba waendelee kukaa kimya mambo yanavyozidi kuharibika, maana nasi tulikaa kimya wakati wakiteswa na utawala dhalimu. Lisu, Mbowe, Zitto msiwatetee watz acheni wanyooshwe kisawa sawa na tozo, bei juu nk, maana awakusimama nanyi wakati mkiteswa

Utawala upi huo wa kidhalimu?
 
Mtu mmoja pekee hawezi leta mabadiliko kama haungwi mkono na wengine.Tozo ziongezwe
Hakuna jambo lolote litakaloanzishwa likose viongozi, na kiongozi hawezi kufanya jambo peke yake bila wafuasi, huu ndio muda wa kuungana.
 
Hakuna jambo lolote litakaloanzishwa likose viongozi, na kiongozi hawezi kufanya jambo peke yake bila wafuasi, huu ndio muda wa kuungana.
Sio kwa watz hata viongozi wanajua hili
 

Attachments

  • Screenshot_20220823_095810.jpg
    Screenshot_20220823_095810.jpg
    64.1 KB · Views: 3
Back
Top Bottom