Mahakama yaamuru Eng. Hersi aachie ngazi Yanga!

Mahakama yaamuru Eng. Hersi aachie ngazi Yanga!

So sad.
Hawa wazee wa timu ni mtihani sana.
Timu iko on fire pesa za kuwasajiri akina Chama zipo.
Ni hatari na nusu
 
Simba tutaipiga goli 12 pamoja na hila zenu za kununua magoli ya Saido na kipindi kile cha kiatu cha Mayele akapewa Mpole bado tuzo mnasema mtazitoa kwenye ngao ya jamii

Simba tutaipiga goli 12 pamoja na hila zenu za kununua magoli ya Saido na kipindi kile cha kiatu cha Mayele akapewa Mpole bado tuzo mnasema mtazitoa kwenye ngao ya jamii
Ngoja wazee kakazie hukumu ndio akili iwasogee vzr
 
View attachment 3044226

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuru Uongozi wa Club ya Yanga ukiongozwa na Rais wa Yanga Injinia Hersi Saidi na wenzake, kuachia ngazi na kuondoka kwenye Club hiyo kwakuwa Katiba ya Yanga haitambui uwepo wao.

Imedaiwa kuwa uamuzi huu wa Mahakama umekuja baada ya Kundi la Wazee wachache waliowahi kuwa Wazee wa Yanga kipindi cha nyuma, kushitaki Mahakamani likidai uwepo wa Viongozi wa sasa wa Yanga (Injinia Hersi na wenzake) ni batili na haujafuata Katiba ya Club hiyo.

Kutokana na Wazee hao kushinda kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, inamaana kuwa Rais wa Yanga Injinia Hersi na Viongozi wenzake wanatakiwa kuachia ngazi na kukabidhi Ofisi kuanzia sasa.

Injinia Hersi alianza kuiongoza Yanga kama Rais miaka miwili iliyopita baada ya kushinda nafasi hiyo akiwa ni Mgombea pekee July 2022 na kumfanya kuwa Rais wa kwanza wa Yanga SC toka kuanza kwa mfumo mpya wa mabadiliko ambapo alitangazwa kuwa atakuwa madarakani kwa miaka minne ( hadi 2026 ) kwa mujibu wa Katiba ya Club hiyo.

Source: #MillardAyoUPDATES

====


Source nyingine:
Wanachama wawili wa Yanga SC JUMA MAGOMA na GEOFREY MWAIPOPO walishinda kesi waliyofungua katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar mwaka jana mwezi Agosti. Kesi yao ilikuwa dhidi ya Baraza la wadhamini la klabu hiyo kuikabidhi klabu kwa mtu wasiyemjua wala asiyekuwa Mwanachama wakati kesi inafunguliwa mwezi Mei mwaka 2022 siku moja kabla ya uchaguzi mkuu wa klabu uliomuweka madarakani Rais wa Yanga Eng Hersi Said. Awali walifungua kesi hiyo Mahakama ya Wilaya ya Ilala iliyopo Kinyerezi jijini Dar, kabla ya kushauriwa kuihamishia katika Mahakama ya Kisutu.

Walipinga kutumika kwa katiba ya mwaka 2020 ambayo ilitumika kwenye uchaguzi Mkuu uliouweka uongozi uliopo madarakani wakisema katiba hiyo sio halali. Inasemekana RITA waliitwa kutoa ushahidi na wakasema wanaifahamu katiba ya mwaka 2011 ambayo ipo ofisini kwao na hiyo ya mwaka 2020 hawaitambui.

Baada ya kupata hukumu yao mwezi Agosti mwaka 2023 JUMA MAGOMA NA GEOFREY MWAIPOPO wameona hakuna utekelezaji wa hukumu hiyo hata baada ya kuwasilisha kwa wahusika wakaamua kufungua kesi ya kukazia hukumu ambapo itatolewa maamuzi mwezi Agosti tarehe 5 mwaka 2024, ili hukumu hiyo ianze kufanya kazi. Ambapo inategemewa Mkutano Mkuu wa Yanga kuitwa ambao utajumuisha WANACHAMA WOTE HAI sio wawakilishi wa matawi pekee (kama ilivyo sasa) na kwenda kwenye uchaguzi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa klabu kwa kufuata katiba ya mwaka 2011.

Kama hili litatokea manake Eng Hersi na timu yake watakuwa wameondoshwa madarakani kwakuwa watakuwa wameingia isivyo halali.
View attachment 3044242
Safi xnaaa muanze kua busy na matatizo .waizi wa wachezaji nyie
 
Screenshot_20240716-234347_1.jpg
 
Kuna wakati nilihoji, lakini nikajikuta niko peke yangu Tanzania nzima, kwamba, hivi inakuwaje kuna kampuni yenye uhusiano wa kibiashara na Yanga, that is GSM, halafu Mwenyekiti wa Yanga, Eng. Hersi, ana ajira rasmi, ukurugenzi wa sijui finance, huko GSM ?

Maslahi ya Yanga na GSM yakisigana, huyu Mwajiriwa wa GSM na Mwenyekiti wa Yanga, anasimama wapi ????

Halafu huyu Mwenyekiti wa Yanga, hana maamuzi ya kusema labda kwa nafasi yake huko GSM ataisaidia Yanga, hawezi kwa saab na yeye ana bosi wake huko GSM ambae nae anatafuta maslahi yake ya kibiashara ndo maana akaji associate na Yanga tangia hapo, yani Ghalib na GSM yake. Inakuaje hiiiiii ? Nobody answered me!

Kumbe bana kuna wenzangu wazee wawili wako nchi hii nao hawamkubali kabisa huyu Eng. Hersi.
 
Kuna wakati nilihoji, lakini nikajikuta niko peke yangu Tanzania nzima, ninaeona hitilafu, kwamba, hivi inakuwaje kuna kampuni yenye uhusiano wa kibiashara na Yanga, that is GSM, halafu Mwenyekiti wa Yanga, Eng. Hersi, ana ajira nyeti huko GSM ?

Maslahi ya Yanga na GSM yakisigana, huyu Mwajiriwa wa GSM na Mwenyekiti wa Yanga, anasimama wapi ????

Halafu huyu Mwenyekiti wa Yanga, hana maamuzi ya kusema labda kwa nafasi hizo mbili atasaidia Yanga kupitia GSM, hawezi kwa saabu na yeye ana bosi wake huko GSM, ndugu Ghalib, ambae nae anatafuta maslahi yake ya kibiashara ndo maana akaji associate na Yanga. Inakuaje hiiiiii ? Nobody answered me!

Kumbe bana kuna wenzangu wazee wawili nchi hii nao hawamkubali kabisa huyu Eng. Hersi.
Baada ya kuanza kushindashinda hii hoja waliizika ila lilikuwa suala la muda tu
 
Tumpe timu yeye akishindwa kuiendesha apigwe mawe 😁, Halafu mbona sio mzee
1721163302648.jpg
 
View attachment 3044226

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam, imeamuru Uongozi wa Club ya Yanga ukiongozwa na Rais wa Yanga Injinia Hersi Saidi na wenzake, kuachia ngazi na kuondoka kwenye Club hiyo kwakuwa Katiba ya Yanga haitambui uwepo wao.

Imedaiwa kuwa uamuzi huu wa Mahakama umekuja baada ya Kundi la Wazee wachache waliowahi kuwa Wazee wa Yanga kipindi cha nyuma, kushitaki Mahakamani likidai uwepo wa Viongozi wa sasa wa Yanga (Injinia Hersi na wenzake) ni batili na haujafuata Katiba ya Club hiyo.

Kutokana na Wazee hao kushinda kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, inamaana kuwa Rais wa Yanga Injinia Hersi na Viongozi wenzake wanatakiwa kuachia ngazi na kukabidhi Ofisi kuanzia sasa.

Injinia Hersi alianza kuiongoza Yanga kama Rais miaka miwili iliyopita baada ya kushinda nafasi hiyo akiwa ni Mgombea pekee July 2022 na kumfanya kuwa Rais wa kwanza wa Yanga SC toka kuanza kwa mfumo mpya wa mabadiliko ambapo alitangazwa kuwa atakuwa madarakani kwa miaka minne ( hadi 2026 ) kwa mujibu wa Katiba ya Club hiyo.

Source: #MillardAyoUPDATES

====


Source nyingine:
Wanachama wawili wa Yanga SC JUMA MAGOMA na GEOFREY MWAIPOPO walishinda kesi waliyofungua katika Mahakama ya Kisutu jijini Dar mwaka jana mwezi Agosti. Kesi yao ilikuwa dhidi ya Baraza la wadhamini la klabu hiyo kuikabidhi klabu kwa mtu wasiyemjua wala asiyekuwa Mwanachama wakati kesi inafunguliwa mwezi Mei mwaka 2022 siku moja kabla ya uchaguzi mkuu wa klabu uliomuweka madarakani Rais wa Yanga Eng Hersi Said. Awali walifungua kesi hiyo Mahakama ya Wilaya ya Ilala iliyopo Kinyerezi jijini Dar, kabla ya kushauriwa kuihamishia katika Mahakama ya Kisutu.

Walipinga kutumika kwa katiba ya mwaka 2020 ambayo ilitumika kwenye uchaguzi Mkuu uliouweka uongozi uliopo madarakani wakisema katiba hiyo sio halali. Inasemekana RITA waliitwa kutoa ushahidi na wakasema wanaifahamu katiba ya mwaka 2011 ambayo ipo ofisini kwao na hiyo ya mwaka 2020 hawaitambui.

Baada ya kupata hukumu yao mwezi Agosti mwaka 2023 JUMA MAGOMA NA GEOFREY MWAIPOPO wameona hakuna utekelezaji wa hukumu hiyo hata baada ya kuwasilisha kwa wahusika wakaamua kufungua kesi ya kukazia hukumu ambapo itatolewa maamuzi mwezi Agosti tarehe 5 mwaka 2024, ili hukumu hiyo ianze kufanya kazi. Ambapo inategemewa Mkutano Mkuu wa Yanga kuitwa ambao utajumuisha WANACHAMA WOTE HAI sio wawakilishi wa matawi pekee (kama ilivyo sasa) na kwenda kwenye uchaguzi mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa klabu kwa kufuata katiba ya mwaka 2011.

Kama hili litatokea manake Eng Hersi na timu yake watakuwa wameondoshwa madarakani kwakuwa watakuwa wameingia isivyo halali.
View attachment 3044242
Hiyo kesi ilikuwa inasikilizwa upande mmoja? Halafu hukumu ya Mahakama inayojiamini isingeamuru waachie ngazi bali ingebatilisha uongozi uliopo, unaamuruje uongozi kuachia ngazi wakati hukumu haijabatilisha?
 
Back
Top Bottom