Mahakama yamwamuru Lissu kufika mahakamani

Mahakama yamwamuru Lissu kufika mahakamani

siasa ni nadharia tu kama mwanasiasa kudhani wapinzani wakichaguliwa watavunja madaraja na kuuza ndege ili kufifisha juhudi.
Ila kiukweli maccm ya hovyo sana hivi kwa kauli kama hizi kweli!!zinatia kinyaa sana kwani hiyo miundombinu ndege na madaraja alinunua kwa hela yake ya mfukoni??
 
Dereva wa Lisu yuko wapi?

Ndiyo mpiga risasi
Kama kuna raia anaweza kupiga risasi 38 mchana kweupe tena kwenye nyumba za viongozi ...zenye ulinzi mkali wa Suma JKT basi kama Taifa tuko hatarini maana IS wako karibu sana
 
Nadhani ni Maagizo kutoka Chamwino! Jamaa hana amani kabisa na Lissu anavyomshushua hadharani.
 
Magufuli kama Magufuli hawezi siasa za ushindani, na kwa muundo wa katiba yetu rais ndio anaagiza mahakama ifanye vipi kazi. Kwa vyovyote vile Magufuli hawezi kukubali ushindani toka kwa Lisu, wakati ana uwezo kabisa wa kuitumia mahakama kumzuia mshindani wake. Kwa sasa hivi hiyo mahakama iko kwenye mbinyo mkubwa ili itumike kumdhibiti Lisu. Na kwa uhakika hata hukumu imeshapangwa iwe vipi.

Pia ni mtihani mkubwa kwa mahakama kiasi kwamba wakiendekeza “maelekezo” wanaweza kutusababishia matatizo nchi yetu na vyombo vya kimataifa na nchi wahisani!

Kwa wenye vichwa vibovu hawajui TL ni gusa unate!
 
Mahakama ndio tuseme hawaoni kuwa anatafuta wadhamini kitendo ambacho kina time limit? Mbona hizo kesi zilizokuwepo hawazisikilizi wanawapiga watuhumiwa tarehe tu na kuwarejesha Segerea.

Upinzani ukichukuwa nchi mwaka wowote, hakuna kuwasamehe wale wote waliotumia madaraka yao vibaya. Wanafanya hivyo kwa utashi wao binafsi na kinyume cha kiapo cha maadili. Piga chini mahakimu na majaji wote watakaonekana wamekiuka kufata sheria ya maadili ya umma.
Nchi isiyofuata sheria huitwa Banana Republic. Lazima kuwe na tofauti baina ya sheria na siasa. Hiyo ni kesi ya miaka minne sasa; haikuanza jana. Angekuwa amebambikwa kesi baada ya kutangaza nia tungesema siyo vizuri, lakini hapa ni kujibu kesi ambayo imekaa mahakamani miaka minne sasa mpaka inafikia wadhamini wake wanataka kujitoa.
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemwamuru kufika mahakamani mbunge wa zamani wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na wenzake watatu, wanaokabiliwa na kesi ya uchochezi, Septemba 14, mwaka huu, baada ya jana kushindwa kufika kusikiliza kesi yake.

Amri hiyo ilitolewa jana na mahakama hiyo iliyoketi chini ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, kesi hiyo ilipopangwa kwa ajili ya kutajwa.

Awali, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, alidai shauri lilipangwa kwa kutajwa na kwamba mshtakiwa Lissu, hakufika kusikiliza kesi yake.

Mdhamini wa Lissu, Robert Katula, alidai mshtakiwa aliwasiliana naye juzi asubuhi na kumueleza kwamba yuko mkoani anatafuta wadhamini kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka huu.

Hakimu Simba, alimtaka mdhamini huyo kuhakikisha mshtakiwa anafika mahakamani na sio kutoa sababu ambazo sio za kisheria.

"Mdhamini hizo sababu hazikubaliki kisheria tusiikosee sheria, sisi ni watekelezaji wa sheria ambapo tunatoa amri. Ukisema unaiachia mahakama tunaweza kusema ulipe dhamana na ukishindwa unakwenda jela hatutaki kufika huko, wewe hakikisha unamleta mshtakiwa tarehe ijayo," alisema.

Hata hivyo, wadhamini wa Lissu waliomba mahakama kujitoa katika udhamini kwasababu wanayemdhamini hana ushirikiano mzuri na wadhamini wake na mahakama iliwaeleza kuwa kisheria mdhamini akitaka kujitoa lazima kwanza anamleta mshtakiwa halafu ndiyo aweze kujitoa.

Kwa upande wa mshtakiwa wa tatu ambaye hakufika mahakamani Mehbooh, ilidaiwa na mdhamini wake kuwa ni mgonjwa na kuwasilisha fomu mahakamani hapo.

Hakimu Simba baada ya kusema hayo, alimtaka mdhamini wa Lissu ahakikishe mshtakiwa huyo anafika mahakamani hapo tarehe ijayo na sio vinginevyo.

Mbali na Lissu washtakiwa wengine ni, Wahariri Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh.

Katika kesi ya msingi kwa pamoja washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka matano ikiwamo kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002.

Ilidaiwa kuwa kati ya Januari 12 hadi 14, 2016 jijini Dar es Salaam, washtakiwa Jabir, Mkina na Lissu, waliandika na kuchapisha taarifa za uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, ‘Machafuko yaja Zanzibar.’

Katika shtaka la pili wanadaiwa kuwa Januari 14, 2016 walichapisha habari hizo ili kuleta chuki kwa wananchi wa Zanzibar.

Mshtakiwa Mehboob anadaiwa kuwa Januari 13 ,2016 katika jengo la Jamana lililopo Manispaa ya Ilala, alichapisha gazeti la Mawio lililokuwa na taarifa za uchochezi.

Ilidaiwa kuwa mshtakiwa huyo pia alichapisha gazeti hilo bila ya kuwasilisha hati ya sheria ya kiapo kwa Msajili wa Magazeti.
Naona kama vile kumekuwa na mabadiliko kidogo kwa mahakimu wetu, mara nyingi mtu hasipofika mahakamani kinacho fuatia ni amri ya kukamatwa hasa kwa kesi kama hizi, na ukizingatia ameweka wazi kwamba sababu ya kutokuhudhuria kwake si sababu ya kisheria. Lakini hapa hakimu amemtaka mshtakiwa ahudhurie mahakamani septemba 14. Muda ambao itakuwa amesha rudisha fomu.
Hii ina maanisha kwamba hakimu ameamua kumpa nafasi Lissu ili akamilishe utaratibu wakutafuta wadhamini nakurudisha fomu kwa wakati? Ama hakimu amesoma alama za nyakati na kugundua kwamba uchaguzi wa mwaka hautabiriki chochote kinaweza kutokea na pengine Lissu anaweza kuwa bosi wake?
 
Nchi isiyofuata sheria huitwa Banana Republic. Lazima kuwe na tofauti baina ya sheria na siasa. Hiyo ni kesi ya miaka minne sasa; haikuanza jana. Angekuwa amebambikwa kesi baada ya kutangaza nia tungesema siyo vizuri, lakini hapa ni kujibu kesi ambayo imekaa mahakamani miaka minne sasa mpaka inafikia wadhamini wake wanataka kujitoa.

Dhamira ya kesi iko wazi kuwa ni siasa za hujuma.
 
Dhamira ya kesi iko wazi kuwa ni siasa za hujuma.
Sijui facts za kesi na utetezi wake ila ninajua kuwa ni kesi ambayo iko mahakamani kwa miaka minne sasa; kwa hiyo haikuanza eti kwa vile Lissu ametia nia, bali alitia nia wakati akiwa na kesi hiyo. Kutia nia hakuna maana ya sheria kutokufanya kazi zake.
 
Sijui facts za kesi na utetezi wake ila ninajua kuwa ni kesi ambayo iko mahakamani kwa miaka minne sasa; kwa hiyo haikuanza eti kwa vile Lissu ametia nia, bali alitia nia wakati akiwa na kesi hiyo. Kutia nia hakuna maana ya sheria kutokufanya kazi zake.

Sasa kumbe unaongelea jambo usilolijua.
 
Nchi isiyofuata sheria huitwa Banana Republic. Lazima kuwe na tofauti baina ya sheria na siasa. Hiyo ni kesi ya miaka minne sasa; haikuanza jana. Angekuwa amebambikwa kesi baada ya kutangaza nia tungesema siyo vizuri, lakini hapa ni kujibu kesi ambayo imekaa mahakamani miaka minne sasa mpaka inafikia wadhamini wake wanataka kujitoa.

..hapa waTz wapinzani wanabambikiwa makesi kiuonevu.

..itafika mahali tutakuwa miongoni mwa nchi zinazoitwa Banana Republic.
 
Sasa kumbe unaongelea jambo usilolijua.
Kwani wewe unajua facts za kesi hiyo kabla hujasikia ushahidi wa pande zote mbili? Hii ndiyo tabia ya kukurupuka na kutoa baseless conclusions. Lissu hajatoa ushahdi wake amekuwa anakwepa mahakamani, kwanza kwa kutokana na ukweli kuwa alikuwa anaumwa, hilo hawezi kulaumiwa, lakini sasa baada ya kupona ameendelea kuwa anakwepa kwenda mahakamani. Mtu mwenye busara hawezi kutoa conclusion bila kuwa na facts zote. Wewe amini utakacho, mimi nitasubiri taarifa za pande zote mbili.
 
..hapa waTz wapinzani wanabambikiwa makesi kiuonevu.

..itafika mahali tutakuwa miongoni mwa nchi zinazoitwa Banana Republic.
Ukiachia mahakama za msingi ambazo ndizo zenye matatizo sana, kuanzia mahakama za hakimu Mikazi hadi mahakama za rufani ziko vizuri sana kuliko unavyodhani. Mara nyingi sana zimeshaamua dhid ya serikali
 
Ukiachia mahakama za msingi ambazo ndizo zenye matatizo sana, kuanzia mahakama za hakimu Mikazi hadi mahakama za rufani ziko vizuri sana kuliko unavyodhani. Mara nyingi sana zimeshaamua dhid ya serikali

..mahakama ktk ngazi zote imetumika kuumiza wapinzani, hilo halina ubishi.

..jeshi la polisi limetumika vibaya kuumiza wapinzani, huku ccm wakifanya wapendavyo.
 
Najua Tundu hawezi na hana sifa ya kuwa no. 1 wetu. Lkn kwa matendo haya dhidi ya mahakama ni mfano hai wa nchi kusadikika atakayoiongoza bwana huyu. Mbinafsi, mbishi, mwenye dharau na asiye na chembe ya staha kwa wenzake.

Naishangaa mahakama nayo kwa kufumbia macho hii contempt of court anayofanya msomi huyu wa kufikirika tena kwenye kesi ya jinai. Kwa nn hakimu asisikilize mashauri ya Lissu expatre?

Sent from my Infinix X624 using JamiiForums mobile app
Fc mp

Sent from my SM-A605FN using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom