digba sowey
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 8,926
- 17,880
Ruto ndo rais, jaji mmoja atajitenga dhidi ya maamuzi ya wenzake
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tuwaombee hekima Wajaluo majibu yakija kinyume na matarajio yaoView attachment 2346190
Hukumu ya Mahakama ya Juu iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ya pingamizi la matokeo ya Rais itatolewa Jumatatu, Septemba 5, saa sita mchana.
Kulingana na notisi kutoka kwa msajili wa Mahakama ya Juu ya Kenya, Letizia Wachira, benchi la majaji saba litatarajiwa kutoa uamuzi huo katika mahakama za Milimani Law.
Majaji hao ni pamoja na Jaji Mkuu Martha Koome, Naibu Jaji Mkuu Philomena Mwilu, Isaac Lenaola, Smokin Wanjala, Ibrahim Mohammed, Njoki Ndungu na William Ouko.
"Fahamu kuwa hukumu katika ombi hili itatolewa Jumatatu, Septemba 5, 2022, saa sita mchana katika Mahakama ya Juu ya Kenya Milimani Law Courts," ilisomeka sehemu ya notisi hiyo.
Raila Odinga wa Azimio na Martha Karua waliwasilisha ombi la kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais kumpendelea rais mteule, William Ruto.
Miongoni mwa masuala ambayo Raila aliyataja katika pingamizi lake ni pamoja na; Ruto hakupata asilimia 50 pamoja na mahitaji ya kura moja, akisema kuwa matokeo kutoka maeneo bunge 27 yalikuwa bado hayajahesabiwa na kuthibitishwa kufikia wakati wa tangazo hilo.
Azimio pia alidai kuwa IEBC haiwezi kuhesabu kura 250,000, bila kujumuisha kura zilizopigwa. Raila na mgombea mwenza waliitaka mahakama kuu kuwatangaza rais mteule na naibu rais mteule mtawalia.
Raila pia alitaka ukaguzi wa kina na wa kitaalamu wa vifaa na teknolojia zote zilizotumiwa na tume ya uchaguzi katika uchaguzi wa urais. Raila pia alitaka Chebukati atangazwe kuwa hafai kushikilia wadhifa wa umma.
Elifu tanoWakenya wanaanza safari mpya ya kupata uzoefu mpya wa rais mpya na maisha yaleyale ya zamani
Hivi bei ya unga imefika ngapi sasa