Unaongea nadharia dada yangu unachokitaka hakipo hapa duniani. Na ndio maana wanawake wengi hawaolewi. Kwa sababu wanataka pesa na kunyenyekewa kwa pamoja. Hivyo vitu havipo na havitakaa viwepo. Hakuna mtu atakaekupa pesa na heshima kwa pamoja. Ukiwa na mtazamo huo lazima utakosa mume labda utafute mwanaume ambaye hana hela. Lakini mwanaume mwenye mtazamo huu atasumbuliwa kila siku na wanawake wakililia awaoe. Na mwanamke mwenye mtazamo huu akipata mwnaume mwenye hela anaolewa chap kwa haraka. Unang'ang'ania viapo vya ndoa wakati wachungaji, masheikh na mapadri wanakumbatia matajiri. Unashindana na mumeo una uwezo wa kulipa ada ? Au kuihudumia hiyo nyumba ? Jishushe tu na jifanye mjinga watoto wakishakuwa na Umri ukienda mume atajirudi angalau. Lakini hauwezi kushindana na mtu mwenye hela. Kama unataka Utu tafuta wa size yako. Kuna dada mmoja alikuwa hajatulia akaja kupata mwanaume mwenye nia ya kumuoa. Alikuwa na uwezo mkubwa kifedha akaja kuachana nae kisa alifumania sms za kimapenzi. Hiyo ilikuwa mwaka 2008, mwezi wa saba mwaka huu anatimiza 37. Hana ndoa na bado yupo kwao, yule jamaa ana mke na ameshaoa. Na huyu dada amekuwa kimada kila akihitaji hela anaenda kwa yule ex-wake kubatuliwa. Anamfanyia vituko mke wa jamaa lakini mke anamwambia tu kuwa "wewe ni hawara hauwezi kuwa mke". Dada mpaka leo anajutia maana mke ndio anaitwa Mama Tarimo yeye kabaki kuwa kihawara chenye tamaa ya hela π π π π π π . Huyu mke wa Tarimo ndio anajua nini maana ya kuwa mke.