Mahakama yazuia ombi la kampuni ya NSK kuifilisi Dangote Cement

Mahakama yazuia ombi la kampuni ya NSK kuifilisi Dangote Cement

Tulidanganywa kuwa anafanya service ya week mbili kumbe anakusanya virago vyake aondoke uwekezaji bongo umemshindaView attachment 1640919
Ni mpaka tutakapozinduka kutoka ktk usingi mzito, na kutambua inahitajika taasisi imara ya uongozi ktk nchi hii isiyolazimika kufungamana na chama tawala. Hii itatufanya kama taifa hasa vyombo vya ulinzi na usalama kuondokana na fikra za kimazoea za kubaka demokrasia ili kusaidia kuzidi kubakia na uongozi wa CCM

Sent from my Nokia 2.1 using JamiiForums mobile app
 
Yote hayo ni mabeberu,Nchi yetu ina mazingira rafiki kwa wawekezaji,comeon bebi,mitano tena kwa JPM in voice ya shehe ubwabwa wa Dar
Ha ha ha, uje nimecheka kama mazuri vile.

Am coming babes[emoji23][emoji23]
 
Pamoja na uwepo wa mada inayohusu kufungwa kwa kampuni ya Dangote hapa nchini iliyoletwa na Mkuu Return Of Undertaker, naomba Moderators muuache Uzi huu kwa maslahi ya mjadala na uelewa.

Kichwa pamoja na maudhui ya uzi wa mtajwa hapo juu ni kuleta habari na kutaka kuaminisha umma kuwa Dangote anataka kufunga kampuni yake kule Mtwara na kuondoa uwekezaji wake hapa Tanzania. Katika kuonesha ukweli huo kumeambatishwa habari ya gazeti la the Citizen la leo.

Kwa msomaji makini ataona na kujua kuwa Dangote ndiye anayepinga kufungwa kwa kampuni yake hapa nchini. Hivyobasi, hana nia ya kuifunga na kuondoka. Yeye ndiye aliyepinga na kufanikiwa kuzuia shauri la kufungwa kwa kampuni yake.

Iko hivi kwenye habari hiyo: Kampuni ya Dangote, kama kampuni nyinginezo, iliingia mkataba wa kuletewa fuel na kampuni ya NSK. Katika kufanikisha hilo, kampuni ya NSK ikachukua mkopo kama mtaji kutoka benki ya Standard Chartered wa bilioni 11.1.

Baada ya kushindikana kulipwa kwa mkopo huo, Standard Chartered ikawashtaki NSK na Dangote. Kufuatia shauri hilo, na katika hali ya kujitetea, NSK akapeleka shauri la kufungwa (winding up) kwa kampuni ya Dangote kwa kushindwa kulipa deni lake kwa kampuni hiyo.

Naye Dangote akawasilisha Mahakamani hapohapo Ombi dogo la kusitisha kwa muda shauri la kufungwa kwa kampuni yake. Ombi lake dogo Dangote ndilo lililotolewa uamuzi kwa kusitisha shauri la kufungwa kwa kampuni yake. Ndiyo kusema, Dangote amefanikiwa kwenye maombi yake.

Kwa kifupi, Dangote ndiye anayepinga kufungwa kwa kampuni yake pamoja na deni linalodaiwa kuwepo dhidi ya kampuni ya NSK. Kwenye mashauri hayo yaliyoripotiwa na the Citizen hakuna mahali Dangote na kampuni yake wameonyesha nia ya kufungwa kwa kampuni hiyo na kuondoka nchini.

Ni vyema kusoma habari kwa makini kabla ya kuandika uelewa ambao wakati mwingine waweza kubeba picha ya kupotosha umma. Dangote ndiye aliyepinga kwa nguvu zake zote kufungwa kwa kampuni yake kwenye mashauri matatu yaliyopo Mahakama Kuu yakihusika kampuni yake, kampuni ya NSK na benki ya Standard Chartered.
 
Ndio tuseme yote lakini tusihusishe matatizo ya menejimenti ya makampuni binafsi na sera za uwekezaji. Kushindwa kwao kuendesha hakuhusiani na sera huo ndio ukweli. Kwa mfano kati ya wawekezaji waliokuwa wapendelewa sana ni Dangote hakuna anayepinga hilo.
Whaaat? hii nchi ina sera mbovu za biashara never seen! Dangote anapendelewa,how? Dangote analalamika anapewa incentive kwa mlango wa mbele,lakini jamaa baadaye wanamfata backdoor tena wanahitaji undiluted shares-haipo duniani hii mambo.
 
Mwandishi: "Mheshimiwa unazungumziaje kuhusu kiwanda cha Dangote kufungwa?"

Mheshimiwa: "Ndugu zangu Watanzania Tanzania ni sovereign state, tumeshiriki ukombozi wa nchi za Sub Saharan Africa, tuna historia kubwa sana barani Africa. Hivyo hawa mabeberu wasiturudishe nyuma katika jitihada zetu kuelekea Tanzania ya viwanda "
 
Acha kusambaza uongo wewe, dangote cement wanakamilisha station ya CNG ambayo ni kubwa kuliko hata inazotarajiwa kujengwa hapo udsm, dangote cement inakuwa full CNG powered plant,
 
Ndio tuseme yote lakini tusihusishe matatizo ya menejimenti ya makampuni binafsi na sera za uwekezaji. Kushindwa kwao kuendesha hakuhusiani na sera huo ndio ukweli. Kwa mfano kati ya wawekezaji waliokuwa wapendelewa sana ni Dangote hakuna anayepinga hilo.
Waliopandisha bei ya makaa ya mawe walikuwa ni menejimenti?!

Huyo Dangote hajaanza kulalamika leo, tunachokiona leo ni matokeo tu.
 
Pamoja na uwepo wa mada inayohusu kufungwa kwa kampuni ya Dangote hapa nchini iliyoletwa na Mkuu Return Of Undertaker, naomba Moderators muuache Uzi huu kwa maslahi ya mjadala na uelewa...
👍 Kwanini Serikali ya CCM inawatesa investors?

Mkapa alijitahidi sana kuiamini have dunia kuwa Mambo ya Azimio la Arusha hayatajirudia tena, Kikwete akadumisha mahusiano mema sana na wawekezaji mbalimbali.

Sasa ngwe hii, tunajidanganya sana hatuthamini umuhimu wa uwekezaji. Hala hatujali Ni watu wetu wangapi wanaoathirika kwa kukosa kazi mara tu wawekezaji wanapotimuliwa.

Endeleeni na tabia mbaya tutaona mwisho wake mwema
 
Tulishasema wafanyabiashara wababaishaji lazima waondoke mapema. No way ufisadi awamu hii hauruhusiwi la sivyo lazima kifungo kinamhusu!
mbuta nanga, yani MATAGA hamjui kitu, zilongwa mbali zitendwa mbali!
Subiri polepole atakutafsiria, sadukayo!
 
Ipo shida jana habari ya Rhino cement kufungua mitambo Pwani.
 
Back
Top Bottom