Maisha bila korodani (Testes) hayana umuhimu kwa ulimwengu huu wa familia

Maisha bila korodani (Testes) hayana umuhimu kwa ulimwengu huu wa familia

Nihilist

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2022
Posts
226
Reaction score
353
Ni miaka 36 imepita tangu pale mvulana huyu azaliwe kwa furaha ya wazazi iliyoje kupata mtoto wa kiume wakifahamu wameleta mwana wa kuwaongezea ukoo na kuwafanya wajivunie kwa kupata wajukuu na huenda vitukuu na vilembwe, masikini pasina kufahamu kuwa mtoto huyo ana mapungufu makubwa ambayo kama wangeliwahi kushughulikia kijana wao katika umri huu angelikuwa na wajukuu wao na kwa furaha wangelizeeka kwa furaha ya kusumbuliwa na vitukuu vikicheza pembeni yao na kuwasumbua huku na huko, wakijiona sura zao za utotoni kwenye nyuso za wajukuu wao..

Kijana alizaliwa na tatizo linalojulikana kitaalamu kama "Undescended Testes".
Hili ni tatizo linalotokea kwa mtoto wa kiume baada ya kuzaliwa na korodani kutokutokea kwenye eneo lake huenda ni korodani moja au zote mbili (kwa mujibu wa daktari).
-Tatizo hili hufanyiwa matibabu mara tu linapogunduliwa kati ya mwezi mmoja hadi mwaka mmoja tangu mtoto kuzaliwa na siyo zaidi (alisema daktari).
-ikipitiliza katika muda huo huweza kuleta hatari ya kupata kansa na kusababisha kifo.
Tuendelee....
kwa kutokulifahamu hilo wazazi walimwacha mtoto wao kukua wakiamini hakuna tatizo linalomsibu litakalo muhuzunisha maishani milele..

Kasheshe imeanza pale kijana kakua na kujitambua ujanani kakutana na wasichana wa kila aina warefu wafupi weupe weusi bado bila bila hakuna ata mtoto wa kusingizia.....mmmh awapo shuleni akafanya siri maana ni kinyume na maadili na sheria za nchi mwanafunzi kuwa na mahusiano na tena chini ya umri under 18....

Baada ya kuhitimu masomo na kurudi mtaani kupambana akapata kazi nzuri kajenga na ana miradi ya kuweza kumuingizia pesa ya kuweka milo mitatu mezani, anakumbuka kuna jambo haliko sawa wapi mtoto wapi mke..?
itaendelea
 

Attachments

  • undescendedTestA-415x233-esIL-1.png
    undescendedTestA-415x233-esIL-1.png
    13.4 KB · Views: 26
Inaendelea

Baada ya kufahamu kuna kitu kinapungua kijana anaanza kuhesabu wadada aliotembea nao awali na kuhisi kuna tatizo sehemu ila anajifariji huenda ni mipango ya mwenyezi Mungu hajafungua njia,

Miaka inapita miaka 30 bado hakuna mtoto wazazi wanadhani huenda tatizo ni kijana kugoma kuleta mke wanaamua kumshauri kuoa ili wapate mjukuu kijana anawaambia kuwa hatooa ila atatafuta mchumba wa kuishi na wakati wanachunguzana tabia maana wanawake wa siku hizi hawatabiliki,

Mwaka mmoja wa pili na watatu unapita bila bila wakwe wakaanza kudai mali na vishika uchumba vya binti yao ila kijana anaona kama vile atapigwa na kitu kizito maana choo kinajaa na mazao hayaonekani...
Pili vipi kama hilo tatizo litaendelea hadi uzeeni na wameishafunga ndoa,je hiyo ndoa itakuwepo au ni kupotezeana muda tu na kufa kwa misongo ya mawazo ....

Anapotimiza miaka 34 ndipo kijana anaamua kumuona daktari ili kupata ushauri wa kitaalam na ikiwezekana matibabu kabisa, masikini hakufahamu kuwa kachelewa, ukweli umekuja ila too late anaenda katika hospitali kubwa kanda ya ziwa kumuona daktari, daktari anamwambia kutoa suruali kuangalia mwanzoni daktari anamfariji kuwa haya matatizo yapo na yanatibika kwa asilimia kubwaila kwa wenye umri chini ya mwaka mmoja ndiyo kwa haraka na uhakika zaidi ila zaidi ya hapo huwa ni hatari kama nilivyoeleza hapo awali.

Kukawa na machaguzi mawili na yote yanahusisha "operation" kisu yaani kuchanwa na baada ya kuchanwa ndipo mbegu zitashushwa eneo lake kama ni nzima au kuondolewa kabisa.

Duuuh moyo ulidunda kwa nguvu niliposikia neno kuondolewa kabisa, nikamuomba daktari vyovyote itakavyokuwa hilo neno lisitokee na huku nikimuomba Mungu sana isiwe hivyo.
Daktari akasema kuna hatua za kufuata na ni gharama sana kufanya upasuaji huo daaaah...!
Itaendelea
 
Pole.
I feel your pain.
Lakini kuna wenye matatizo kukuzidi. Kamwe usichukue uamuzi wa kujidhuru au kujitoa uhai.
Ukihitaji familia kuna wadada wameshazaa na wamefiwa na waume zao. Unaweza jaribu bahati yako. Kila la kheri.
 
Pole.
I feel your pain.
Lakini kuna wenye matatizo kukuzidi. Kamwe usichukue uamuzi wa kujidhuru au kujitoa uhai.
Ukihitaji familia kuna wadada wameshazaa na wamefiwa na waume zao. Unaweza jaribu bahati yako. Kila la kheri.
Ndiyo hilo ni wazo zuri lakini ni vipi unajisikia pale unaposhika mtoto wa mwanaume mwingine na kumuweka kifuani kwako na kujiaminisha hiyo ni mbegu yako....

Ni huzuni kiasi gani unayoipa mwanaume pale unafahamu kabisa unavyovitafuta vyote havitomnufaisha mwanao bali watoto wa wengine..

Ni sonona kiasi gani pale mwanaume unapokaa kijiweni na wanaume wenzako wanajisifia kuhusu watoto wao wanavyofanya darasani na kwamba wamezaa ma- genius na wewe una mtoto hata huzielewi tabia zake..?

Je jamii inayokuzunguka utaiambia ukweli ni mtoto wa kuasil au ni wako na vipi wazazi wako utawapa ukweli.?
au utaleta wa ukoo mwingine kwao na kusema ni mbegu yako
 
Pole mkuu jisikie huru na usijione inferior
Najitahidi ila ninapokuwa pekee yangu haya maswali yanakua magumu kujibu

1:-Nahangaika kutafuta mali namtafutia nani.?
2: -unapokosa korodani kuna homoni zinapungua na utendaji kazi unapungua ....
Sasa namuangaikia nani..?
3:-Je naweza kurudisha korodani hizo?
 

Attachments

  • Johnstone Ouko Mukabi - Mtoto Si Nguo(360P).mp4
    8 MB
Ni miaka 36 imepita tangu pale mvulana huyu azaliwe kwa furaha ya wazazi iliyoje kupata mtoto wa kiume wakifahamu wameleta mwana wa kuwaongezea ukoo na kuwafanya wajivunie kwa kupata wajukuu na huenda vitukuu na vilembwe, masikini pasina kufahamu kuwa mtoto huyo ana mapungufu makubwa ambayo kama wangeliwahi kushughulikia kijana wao katika umri huu angelikuwa na wajukuu wao na kwa furaha wangelizeeka kwa furaha ya kusumbuliwa na vitukuu vikicheza pembeni yao na kuwasumbua huku na huko, wakijiona sura zao za utotoni kwenye nyuso za wajukuu wao..

Kijana alizaliwa na tatizo linalojulikana kitaalamu kama "Undescended Testes".
Hili ni tatizo linalotokea kwa mtoto wa kiume baada ya kuzaliwa na korodani kutokutokea kwenye eneo lake huenda ni korodani moja au zote mbili (kwa mujibu wa daktari).
-Tatizo hili hufanyiwa matibabu mara tu linapogunduliwa kati ya mwezi mmoja hadi mwaka mmoja tangu mtoto kuzaliwa na siyo zaidi (alisema daktari).
-ikipitiliza katika muda huo huweza kuleta hatari ya kupata kansa na kusababisha kifo.
Tuendelee....
kwa kutokulifahamu hilo wazazi walimwacha mtoto wao kukua wakiamini hakuna tatizo linalomsibu litakalo muhuzunisha maishani milele..

Kasheshe imeanza pale kijana kakua na kujitambua ujanani kakutana na wasichana wa kila aina warefu wafupi weupe weusi bado bila bila hakuna ata mtoto wa kusingizia.....mmmh awapo shuleni akafanya siri maana ni kinyume na maadili na sheria za nchi mwanafunzi kuwa na mahusiano na tena chini ya umri under 18....

Baada ya kuhitimu masomo na kurudi mtaani kupambana akapata kazi nzuri kajenga na ana miradi ya kuweza kumuingizia pesa ya kuweka milo mitatu mezani, anakumbuka kuna jambo haliko sawa wapi mtoto wapi mke..?
itaendelea
Jaribu kuja southafrica hosptali zipo nzuri tena ni kama bure kbsa garama ni kuja tu naamini unaweza kupata matibabu mazuri zaid maana huku wana vifaa vzur sana
 
Inaendelea

Baada yakupata taratibu za upasuaji jumla ya gharama haikuwa kubwa sana kama milioni 4.
Poa ikatolewa na kupangiwa siku ya vipimo kama baada ya wiki moja hivi mbele, siku ya vipimo ultrasound ikaonesha ziko vizuri na ziko kwenye eneo zuri, kupangiwa siku za maandalizi (kukaa hapo hapo hospital ) kufanyiwa vipimo vya karibu na kuandaliwa kwa upasuaji,

Baada ya siku tatu hospital na kuoneshwa daktari atakayefanya upasuaji kutoka Ubelgiji (alikuwa mdogo mdogo kiumri) siku ikawadia alfajiri na mapema kijana kalazwa kitandani kungoja kisu, sindano za ganzi kuupooza mwili mzima zikamuingia taratibu mwili ukawa wa baridi kuashiria kuna mabadiliko ndani ya mwili yametokea, msaidizi mmoja wa daktari akagonga gonga goti kuona kama bado kuna hisia ila hakukuwa na hisia zozote.

Visu na mikasi ikaletwa na shughuli ikaanza ya kuhamisha korodani (maana ndiyo lengo la upasuaji kwa muda huo) maumivu yakawa yanasikika kwa mbali ya nyembe na visu kwa jinsi daktari alivyokuwa anachimba kuingia ndani.

Ghafla daktari akaonesha huzuni na kusogea kwa kijana kumuuliza "kijana kwa hali ilivyo inabidi kuziondoa kabisa"

Kijana kwa sauti ya kuhamaki na kushindwa nini cha kufanya akauliza
"Kwanini.? Mbona vipimo vilionesha ni nzima na zinaweza kurudishwa eneo yaani zinin'ginie"
Mbelgiji akajibu "mimi ni daktari mzoefu na niliishafanya upasuaji kama huu zaidi ya mara 300".

Moyo wakijana ulipatwa na mshtuko na kukosa uvumilivu hadi machozi kuanza kumtoka kulaumu kuwa ugumba unamuijia...

Hakuwa na namna bali kumuachia daktari kazi yake na kumuomba daktari kumuachia walau korodani moja tu.....daktari hakujibu kitu....

Inaendelea
 
Back
Top Bottom