Maisha bila korodani (Testes) hayana umuhimu kwa ulimwengu huu wa familia

Maisha bila korodani (Testes) hayana umuhimu kwa ulimwengu huu wa familia

Pole.
I feel your pain.
Lakini kuna wenye matatizo kukuzidi. Kamwe usichukue uamuzi wa kujidhuru au kujitoa uhai.
Ukihitaji familia kuna wadada wameshazaa na wamefiwa na waume zao. Unaweza jaribu bahati yako. Kila la kheri.
Tuko wengi mkuu
 
Inaendelea ...

Baada ya kutoka hospital ndipo ugumu wa maisha na majuto ndipo yanaanza.....

-Mwili kuwa na uchovu wa muda mrefu ata pale nikipumzika au kushinda muda mrefu bila kufanya kazi,nachoka bila sababu..

- Kukosa hamu ya kufanya mapenzi kwa muda mrefu ( naweza kukaa ata mwezi mzima bila kumuwazia mwanamke )...mwanamke ndiye anayeniomba kufanya mapenzi kila mara...

-Kuwa na Hasira za ghafla na za mara kwa mara tena zisizoisha kirahisi...mfano unaweza nikosoa kidogo huenda kwa nia njema nikakupandia juu tena kwa lugha mbaya na yenye kejeri ila zikipoa najishangaa kama ni mimi niliongea na kufanya vitendo hivyo...

-Kuwa kwenye wimbi la maswali ya muda mrefu yasiyo na majibu, kuongea mwenyewe barabarani tena kwa sauti bila kujijua nakuja shituka watu wananitizama navunga kama naimba...😟😟😟..

-Kuwa na mshtuko na mfedheheko wa moyo ghafla kwa suala dogo mfano kupata hasara ya pesa kidogo kwa mfano hasara ya shilling mia na hapo nina laki ya matumizi ya siku na siyo kawaida yangu nilikuwa mtoaji wa pesa ila sasa ni tofauti...

-Napenda kujitenga maana nahofia kuchukizana na marafiki zangu nikifahamu kuwa wakiniudhi kidogo tu mimi ni dakika tano mbele urafiki unakufa tena kwa matusi na vitisho vya maisha nikituliza akili najishangaa nilikuwa mimi kweli huyo??......

Ila kuna kifungo cha matibabu kinaitwa therapy haijalishi ni ya vidonge,sindano na mafuta ambayo nahofia nikiingia huko yaani hadi UMAUTI UTAKAPONIKUTA...

MWISHO
Mods muwe mnaweka na kitufe chenye emoji ya kulia....tafadhali I😭
 
Inaendelea

Baada yakupata taratibu za upasuaji jumla ya gharama haikuwa kubwa sana kama milioni 4.
Poa ikatolewa na kupangiwa siku ya vipimo kama baada ya wiki moja hivi mbele, siku ya vipimo ultrasound ikaonesha ziko vizuri na ziko kwenye eneo zuri, kupangiwa siku za maandalizi (kukaa hapo hapo hospital ) kufanyiwa vipimo vya karibu na kuandaliwa kwa upasuaji,

Baada ya siku tatu hospital na kuoneshwa daktari atakayefanya upasuaji kutoka Ubelgiji (alikuwa mdogo mdogo kiumri) siku ikawadia alfajiri na mapema kijana kalazwa kitandani kungoja kisu, sindano za ganzi kuupooza mwili mzima zikamuingia taratibu mwili ukawa wa baridi kuashiria kuna mabadiliko ndani ya mwili yametokea, msaidizi mmoja wa daktari akagonga gonga goti kuona kama bado kuna hisia ila hakukuwa na hisia zozote.

Visu na mikasi ikaletwa na shughuli ikaanza ya kuhamisha korodani (maana ndiyo lengo la upasuaji kwa muda huo) maumivu yakawa yanasikika kwa mbali ya nyembe na visu kwa jinsi daktari alivyokuwa anachimba kuingia ndani.

Ghafla daktari akaonesha huzuni na kusogea kwa kijana kumuuliza "kijana kwa hali ilivyo inabidi kuziondoa kabisa"

Kijana kwa sauti ya kuhamaki na kushindwa nini cha kufanya akauliza
"Kwanini.? Mbona vipimo vilionesha ni nzima na zinaweza kurudishwa eneo yaani zinin'ginie"
Mbelgiji akajibu "mimi ni daktari mzoefu na niliishafanya upasuaji kama huu zaidi ya mara 300".

Moyo wakijana ulipatwa na mshtuko na kukosa uvumilivu hadi machozi kuanza kumtoka kulaumu kuwa ugumba unamuijia...

Hakuwa na namna bali kumuachia daktari kazi yake na kumuomba daktari kumuachia walau korodani moja tu.....daktari hakujibu kitu....

Inaendelea
Dah,sad🥺🥺
 
Kama nakosea basi nakubali kukosolewa. Ila hii ni hadithi tu, maana imeandikwa kiufundi mno na mtu mwenye fani ya uandishi.
 
Nikuulize swali fupi tafadhari...
Kwanini unaishi...?
Hiyo furaha umewahi kuihisi wapi kama si kwa kusikia au kuona vile watu wengine wanavyoielezea

Furaha ya kuona sex ni kila kitu duniani kiasi kwamba ukikosa uwezo wake unajiona huna ulichobakiza duniani

Furaha ya kuona mtoto ni kila kitu

Ina maana wewe ulipozaliwa hadi unafikia umri wa kupata mtoto, uwepo wako duniani ulikuwa useless kwa sababu hukuwa na mtoto???...

Mkuu nakuelewa unavyojihisi na una sababu zote za kujihisi hivyo Ila nachojaribu ni kukuambia usijione kama maisha yako ni worthless

Bado kwa nafasi yako kuna watu unaoweza kujitolea kwao na ukawa ni baba na mkombozi kwao kiasi cha kukupenda na kukuthamini hadi ukajiona una maana kubwa duniani

Cha msingi ni kutengeneza system ya maisha itakayokupa furaha wewe mwenyewe na sio kusubiri kutimiza standards za jamii zetu ili ujihisi na wewe ni binadamu wa kawaida

Ulishawahi kujiuliza walemavu au watu walioodhoofu huwa wanaishi vipi wakati jamii inawachukulia tofauti. Wale matasa wanaishije na wengine hata neema ya pesa wamekosa. Wanawezaje ku_survive kwenye dunia katili namna hii

Jibu ni moja, wamejikubali na kuishi na wanaowakubali na mawazo ya wengineo yasiwaathiri. Sikuambii hakutakuwa na time utawaza lakini ukifanikisha kujikubali bhasi utaihisi furaha zaidi kuliko huzuni
 
Nikuulize swali fupi tafadhari...
Kwanini unaishi...?
Ni swali ambalo nimejiuliza mara nyingi sana japo sijawahi kuyafungulia thread jf 🙏🙏

Ninaishi kwa sababu nina uhai ambayo ni zawadi kubwa kuliko zote maana kama kuna kitu ambacho billion ya watu waliolala kaburini wangepewa nafasi bhasi wangeomba pumzi hata ya dakika tano tu ili wajirekebishe au warekebishe kitu flani maana uhai ni fursa ambayo kila binadamu anapewa ONCE


Ninaishi kwa sababu nimeijua impact yangu kwenye maisha ya watu wengine, sio watoto maana sina japo umri ni sahihi kuwa nao Ila watu ambao nimejitolea kwao. Professionally na kikawaida kiushauri hata kuwasaidia wasiojiweza. Nipo naturally selfless na hakuna kitu nainjoi kama kusaidia watu, kwa kila tumaini na tabasamu nalolisababisha kwao, it means a world to me

Ninaishi kwa sababu nimeijua nafasi yangu na kujiangalia katika uhalisia wangu. Kuzimiliki na kuzikubali kasoro zote nilizonazo,

magumu hote niliyopitia na ninayopitia pamoja na makosa makubwa niliyoyafanya


Yote hayo yamenifanya kuwa mimi na kuna viatu ambavyo navivaa kwa sasa, ninaamini nisingekuwa hivi nilivyo nisingeweza, labda ningekuwa na kazi serikalini, nimeoa nina watoto na maisha yameishia hapo

Ila kwa utofauti wangu ndio umenipa nafasi ya kuyaona maisha katika angle tofauti ambayo wengi hawaioni, maisha yamenipa jukumu ambalo si kila mtu analo and in sha allah, siku moja nitafanikisha

Hiyo ndio core ya maisha yangu, sio watoto , sio mke, sio ndugu, sio familia but MYSELF 🙏🙏🙏
 
Usiishie kuwatupia lawama wazazi mkuu maana hata mimi yalinikuta kama yako japo tofauti kidogo(sitoweza kuelezea hapa) nililalama ila nikaishia kushukuru maaana yameshatokea sasa
Pole,ingekuwa vizuri kama unge-share iwe fundisho kwa wengine

Kumbuka maisha ni fumbo
 
Ni kweri kabisa ss sote hatujui kesho yetu itakuaje cha msingi ni kumshukuru mungu kwa kila jambo na kila kinacho tokea kwenye haya maisha ni mipango yake mungu na kuna kusudio la mungu kufanya hivyo emoji26][emoji26][emoji26][emoji26]
 
Inaendelea

Baada ya kufahamu kuna kitu kinapungua kijana anaanza kuhesabu wadada aliotembea nao awali na kuhisi kuna tatizo sehemu ila anajifariji huenda ni mipango ya mwenyezi Mungu hajafungua njia,

Miaka inapita miaka 30 bado hakuna mtoto wazazi wanadhani huenda tatizo ni kijana kugoma kuleta mke wanaamua kumshauri kuoa ili wapate mjukuu kijana anawaambia kuwa hatooa ila atatafuta mchumba wa kuishi na wakati wanachunguzana tabia maana wanawake wa siku hizi hawatabiliki,

Mwaka mmoja wa pili na watatu unapita bila bila wakwe wakaanza kudai mali na vishika uchumba vya binti yao ila kijana anaona kama vile atapigwa na kitu kizito maana choo kinajaa na mazao hayaonekani...
Pili vipi kama hilo tatizo litaendelea hadi uzeeni na wameishafunga ndoa,je hiyo ndoa itakuwepo au ni kupotezeana muda tu na kufa kwa misongo ya mawazo ....

Anapotimiza miaka 34 ndipo kijana anaamua kumuona daktari ili kupata ushauri wa kitaalam na ikiwezekana matibabu kabisa, masikini hakufahamu kuwa kachelewa, ukweli umekuja ila too late anaenda katika hospitali kubwa kanda ya ziwa kumuona daktari, daktari anamwambia kutoa suruali kuangalia mwanzoni daktari anamfariji kuwa haya matatizo yapo na yanatibika kwa asilimia kubwaila kwa wenye umri chini ya mwaka mmoja ndiyo kwa haraka na uhakika zaidi ila zaidi ya hapo huwa ni hatari kama nilivyoeleza hapo awali.

Kukawa na machaguzi mawili na yote yanahusisha "operation" kisu yaani kuchanwa na baada ya kuchanwa ndipo mbegu zitashushwa eneo lake kama ni nzima au kuondolewa kabisa.

Duuuh moyo ulidunda kwa nguvu niliposikia neno kuondolewa kabisa, nikamuomba daktari vyovyote itakavyokuwa hilo neno lisitokee na huku nikimuomba Mungu sana isiwe hivyo.
Daktari akasema kuna hatua za kufuata na ni gharama sana kufanya upasuaji huo daaaah...!
Itaendelea
I'm wadau naomba Kuliza ivi unaweza simamisha haliyakuwa hauna korodani poumb ata moja...?
 
Back
Top Bottom