Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Maisha ya machimbo ya dhahabu ni zaidi ya jeshi, nilikimbia

Kimsingi huo wako haukua uchimbaji hata level ya mchimbaji mdogo ulikua hujafika bali ulikua mbangaizaji tu. Watu mnachafua sana sifa za uchimbaji wakati mnaofanya sio uchimbaji.

Ni sawa na mtu awe anauza pair moja ya kiatu Kariakoo akose mteja aseme kkoo pagumu. Huyu hana duka, hata level ya umachinga hajafikia, hajui anything kuhusu ins and outs za Kkoo afu aseme kkoo pagumu, utamchukulia seriously kweli?

Chunya inatoa 300-400Kg of gold yani over 35 Billion TSH monthly. Mnadhani hizi dhahabu zinatoka mbinguni?

Uchimbaji kama biashara zingine unahitaji uwekezaji tena uwekezaji wa maana na maarifa na uchimbaji sio a get rich quick scheme kama wengi mnavyojazana. Wengine tukitoa story zetu hapa mtashangaa. Hizo kona zote nazifahamu na nitakua huko soon.
Hiiii naona likes nyingi mnoo. Bufa anapenda kutufunga kamba nyinyi 😂🙌
 
Nahisi huyo msafwa anaitwa Mwambe kama sijakosea, ndiye mchimbaji wa kwanza kabisa kusambaza vipimo Chunya nzima. Na Hilo swala la vipimo lina habari yake wakati Mboma (Msafwa mwenzake na rafiki yake) akiwa mkuu wa majeshi( Hapa sitagusia[emoji3][emoji119])
Billionaire gani huyu analalia tu [emoji1787][emoji1787][emoji1787]pesa ambayo hata Fred vunjabei anaipiga ndani ya mwaka mmoja tu, kweli pesa Zipo mjini tu
 
They ought to learn from Indians. Wahindi wanawahusisha watoto wao kwenye biashara zote from the very young age sio kufukuza mtoto nyumbani anaondoka hajui dingi unafanya mishe gani. Mambo mengine ya kijinga sana.
Madingi wa kibongo uduanzi mwingi.. nimemaliza chuo namuuliza dingi vipi KONEKSHENI ananiambia nijiajiri. Nikamshangaza na viganja vitatu vya chap chap nikasepa zangu. Aaache ujinga
 
Uchimbaji wa dhahabu ni mgumu sana kuna jamaa mwaka jana kaacha kazi Benki kaingia kwenye hizi mishe kule Kilindi Handeni kapoteza zaidi ya milion 25 na aliambulia 7grms tu. Kazi kapoteza, hela imeisha na familia yake imemdhrau na kumtenga yaani sasa hivi kachanganyikiwa kwa kifupi dishi limeyumba na kapoteza dira kabisa na sasa hivi kaingia kwenye kubet [emoji28]
[emoji1787][emoji23][emoji1787][emoji23]
 
Jamaa ana kibunda sana
Mavi yake, nimeangalia clip nimeona muungaji ungaji tu hana kitu, imagine mtu anaomba benk imkopeshe billion nane tu [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787], kama Tajiri Kwa huo mkpo bado ni kinda tu ebu tembeleeni katoro mtaona vijana waliozaliwa 1992 kila siku wanakusanya mzigo wa kilo tatu mpaka nne wa dhahabu.
 
Mbona story zenu zimeegamia kwenye kutisha tu no hope kabisa unataka kusema sehemu za madini hakuna vitu vizuri vya kujivunia?
Hapa tunaelezea risk zilizopo kwenye machimbo ili kutoa mwanga kwa watu ambao hawajawahi kufanya shughuli kama hizo na wanataka kujaribu.

Unajua wengi wasiojua, wakisikia neno dhahabu wanajua ni kitu simple na kinapatikana kirahisi?

Upande mzuri kuhusu madini pia upo ila upande huo ili uweze kuona neema zake basi hakikisha unakuwa na mtaji mkubwa.

In short ni kwamba kwenda kuchimba dhahabu ukiwa huna hela kwa lengo upate hela ni worse idea.

Kwasababu utalazimika kufanya kazi katika mazingira magumu na ya hatari kwa guarantee ya kipato kidogo.

Ukiwa huna hela itakulazimu tu uchimbe machimbo yasiyohitaji mtaji, labda kuokota mawe au ukasambaze (kubinuka)

Ambapo huko kwenye mawe ili angalau upate pesa ya kueleweka itakubidi upate sehemu yenye mawe yenye dhahabu nyingi.

Mfano kule kuna kipimo cha makadirio kujua kiwango cha dhahabu kilichopo kwenye mawe.

Hicho kipimo kinakadiliwa kupitia idadi ya ujazo wa mawe kwenye kile kiroba cha jumla cha sabuni ya unga. Kule ujazo huo unafahamika kwa neno "dumu"

Sasa ili at least uonekane upo kwenye malengo basi walau kila dumu liwe na possibility ya kutoa point 2.

Ambapo point 1 sawa na 10,000 and this is high maximum approximation. Sio rahisi dhahabu ya kutoka karashani kuuzwa bei hiyo labda ichomwe na chemicals iwe pure.

Na mind you, the more you melting it to get it pure, the more weight decreasing.

So ni msala hakuna nafuu.

Sasa angalia hali ya sasa ilivyo pamoja na kwamba unaona pointi 2 ambayo value yake ni sawa na 20,000 (kwa makadirio ya juu) unaweza kuona kama sio kubwa hiyo pesa ukilinganisha na upatikanaji wake.

Lakini katika hiyo hela kumbuka kila dumu kuna percent utakuwa unakatwa kwa ajili ya kulipia huduma ya kusagiwa mawe kwa mwenye karasha.

Angalia sasa hali ilivyo, ni kwamba ni vigumu sana kupata eneo ambalo utapata mawe yenye sample ya point 2 kwa dumu moja.

Sehemu ambayo utakuta kuna mawe yenye sample yenye kutoa point zaidi ya 2 kupanda juu. Mara nyingi hiyo sio sehemu salama.

Mfano kuna kijiji kimoja kinaitwa "Shoga" huko ziliwahi kufunguka yani dumu moja lilikuwa linatoa hadi Gram kasoro lakini usalama wake ulikuwa mdogo.

Watu walikuwa ni wengi, na penye wengi kuna mengi, watu wako ladhi kukuua ili wakupore gema.

Ndugu yangu kama una ndoto ya kwenda kwenye madini jaribu kuangalia hizi changamoto na uzipime kama unaweza kuzimudu.

Ukiona unaziweza basi unaweza kwenda, ila usije ukaenda ukategemea kitu tofauti na hiki nilichokiandika kwa kudhani mambo ni simple.

Unaweza ukakutana na makubwa mengine ambayo hata hapa mimi sijayaandika.
 
Kuna kuumwa, kupata ajari na kufa ni kawaida tu kwahiyo huyo hata angekuwa dar anauza nguo angekufa tu msikuze vitu hapa, unataka kusema kafa kisa yupo machimhon? Kila hatua ni risk mkuu
Safety is given priority than any bullshit.

Ukikaa karibu na moto unakuwa umechagua kuota au kujiunguza.

Ukikaa kwenye mazingira ya machimbo ambayo usalama wake ni mdogo unakuwa umechagua

1. kupoteza kiungo
2. Kuumwa
3. Kufa.

Bahati mbaya 1 na 3 imekuwa ikijitokeza mara nyingi sana with my experience
 
Hapa tunaelezea risk zilizopo kwenye machimbo ili kutoa mwanga kwa watu ambao hawajawahi kufanya shughuli kama hizo.

Unajua wengi wasiojua, wakisikia neno dhahabu wanajua ni kitu simple na kinapatikana kirahisi?

Upande mzuri kuhusu madini pia upo ila upande huo ili uweze kuona neema zake basi hakikisha unakuwa na mtaji mkubwa.

In short ni kwamba kwenda kuchimba dhahabu ukiwa huna hela kwa lengo upate hela ni worse idea.

Kwasababu utalazimika kufanya kazi katika mazingira magumu na ya hatari kwa guarantee ya kipato kidogo.

Ukiwa huna hela itakulazimu tu uchimbe machimbo yasiyohitaji mtaji, labda kuokota mawe au ukasambaze (kubinuka)

Ambapo huko kwenye mawe ili angalau upate pesa ya kueleweka itakubidi upate sehemu yenye mawe yenye dhahabu nyingi.

Mfano kule kuna kipimo cha makadirio kujua kiwango cha dhahabu kilichopo kwenye mawe.

Hicho kipimo kinakadiliwa kupitia idadi ya ujazo wa mawe kwenye kile kiroba cha jumla cha sabuni ya unga. Kule ujazo huo unafahamika kwa neno "dumu"

Sasa ili at least uonekane upo kwenye malengo basi walau kila dumu liwe na possibility ya kutoa point 2.

Ambapo point 1 sawa na 10,000 and this is high maximum approximation. Sio rahisi dhahabu ya kutoka karashani kuuzwa bei hiyo labda ichomwe na chemicals iwe pure.

Na mind you, the more you melting it to get it pure, the more weight decreasing.

So ni msala hakuna nafuu.

Sasa angalia hali ya sasa ilivyo pamoja na kwamba unaona pointi 2 ambayo value yake ni sawa na 20,000 (kwa makadirio ya juu) unaweza kuona kama sio kubwa hiyo pesa ukilinganisha na upatikanaji wake.

Lakini katika hiyo hela kumbuka kila dumu kuna percent utakuwa unakatwa kwa ajili ya kulipia huduma ya kusagiwa mawe kwa mwenye karasha.

Angalia sasa hali ilivyo, ni kwamba ni vigumu sana kupata eneo ambalo utapata mawe yenye sample ya point 2 kwa dumu moja.

Sehemu ambayo utakuta kuna mawe yenye sample yenye kutoa point zaidi ya 2 kupanda juu. Mara nyingi hiyo sio sehemu salama.

Mfano kuna kijiji kimoja kinaitwa "Shoga" huko ziliwahi kufunguka yani dumu moja lilikuwa linatoa hadi Gram kasoro lakini usalama wake ulikuwa mdogo.

Watu walikuwa ni wengi, na penye wengi kuna mengi, watu wako ladhi kukuua ili wakupore gema.

Ndugu yangu kama una ndoto ya kwenda kwenye madini jaribu kuangalia hizi changamoto na uzipime kama unaweza kuzimudu.

Ukiona unaziweza basi unaweza kwenda, ila usije ukaenda ukategemea kitu tofauti na hiki nilichokiandika kwa kudhani mambo ni simple.

Unaweza ukakutana na makubwa mengine ambayo hata hapa mimi sijayaandika.
Dhahabu unayong'ara hupitishwa kwenye tanuru la Moto... Hakuna kitu rahisi kwenye utajiri, high risk high return jinsi unavyosacrifice Roho yako kutafuta utajiri siku ukitoboa unakuwa level nyingine kabisa

Kuna kaka mmoja nilikuwa sehem ya geita huko alikuwa akisimulia kaka ake alivyotoka kwenye umasikin na kuwa Tajiri wa kufa mtu, yeye alienda Kongo huko bila vibali nakumbuka Kongo kila hatua Kuna magaidi hawajawahi nyoa ndevu.

Sasa alienda huko na kuingia kwenye sehemu za madini unaambiwa alipofika alikaa sio chini ya miaka mitano kuchimba dhahabu Kwa jembe na nyundo huku wajeda wakija kukagua wenye vubali anajificha kwenye mashimo hata siku Tatu bila kula Wala Maji

Kufupisha tu story alikuja kupata jiwe la dhahabu maana Kuna Mawe wengine asilimia sabini ni dhahabu tupu, akaweka kwenye begi akaanza kukimbia pori Kwa pori kurudi Tanzania tena Kwa mguu alipofika kwenye misitu minene alikutana na makundi ya kigaidi waanza kumfurumusha Kwa risasi jamaa akawa anakimbia zigizaga akakuta mto akajirusha ndo pona yake akaja kuibukia ng'ambo japo mto ulikuwa na mamba wa kutosha alivuka salama.

Siku ya pili hajapata kitu mdomoni yupo na jiwe tu la dhahabu japo hana uhakika mpaka akaipime, bahati akafika ziwa tanganyika akapanda boti Kuja Tanzania alipofika kigoma akapanda gari la geita akaenda soko la madini, wakaisafisha lile jiwe akapata dhahabu kilo tano mzee mzima akaingiziwa mpunga CRDB

saizi ni Tajiri pale geita changanya Mali za Fred vunjabei na sandaland hawamfikii hata robo.

Hakuna jepesi hii Dunia ukitaka kubaki masikini basi endekeza uoga na usisumbue watu kuomba msaada wa pesa huwa mnakera
 
Back
Top Bottom