DOKEZO Maji ya kuoshea maiti yanayo lalamikiwa kutumika kuhifadhia samaki yanauzwa kwenye maduka ya dawa za asili, Serikali imulike huko

DOKEZO Maji ya kuoshea maiti yanayo lalamikiwa kutumika kuhifadhia samaki yanauzwa kwenye maduka ya dawa za asili, Serikali imulike huko

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Wachawi wako Dunia nzima, hata ktk butchers za nyama hutumia,

Nakushauri kuomba na kutakasa vyakula vyote na VITOWEO kabla hujavitumia.

Ktk butchers asilimia kubwa watu hulishwa NYAMA za watu, ndo Chanzo Cha magonjwa mengi ya WANADAMU.

Kama ndo unajua Leo umeliwa. STUKA.

Ameeeen
Nyama za watu ??? !!
 
Ungesema Dawa za kuhifadhia maiti na siyo maji,mwanza samaki waliohifadhiwa kwenye majokofu hazina wateja,Sababu ni jirani na ziwa hivyo wateja hupenda kununua samaki asubuhi na jioni waliotoka kuvuliwa mida hiyo hiyo.

Hivyo waadhirika wakubwa ni wateja wa mikoani.
Absolutely right! Wanatumia Ile dawa ya kuhifadhia maiti I think inaitwa formaline (sp) huenda ndio alichomaanisha
 
Inawezekana kuna ka- Ukweli ndani yake. Lakini nawasihi wataalamu wetu wa saratani wazidi kufanya utafiti wa chanzo cha saratani kanda ya ziwa. Kuna sababu zaidi ya hiyo. Sababu haingii akilini mtu wa Kyerwa, Muleba, Kanyigo. Murugwanza, ana pata saratani Eti sababu amekulia samaki waliooshewa maji ya maiti. Wakati watu wa Muleba, Kanyigo wanapata samaki flesh toka ziwa I (Victoria). Sababu zipo zaidi ya hiyo fanyeni utafiti wa kina. Please, don't easily jump to the conclusion. Cancer imekuwepo kwa wingi kanda hiyo kabla hizi Zebaki na dawa za kuhifadhi maiti haijawa 'common'.
Migodi kutiririsha zebaki ziwani mf Nyamongo Barrick wametuhumiwa Kwa KASHFA hiyo.

Ni maji zaidi Wala Si samaki. Serikali isitafite pa kujificha MIGODI ya madini ya wazawa na Wawekezaji ni tatizo kubwa.
 
Kwa hiyo ofisi ya Mkuu wa Mkoa wanapotoa pesa ili kuzuia hiyo story isitoke lengo lao watu wazidi kuathirika?

Kama hii story ni kweli, inashangaza kuona tuna pesa za kukuza matatizo, lakini
hatuna pesa za kutatua matatizo yetu.
 
This is a very cheap argument, maji ya kuoshea maiti yana uhusiano gani na kutokea saratani.......do you have any mechanism behind.
Labda tuseme unamaanisha kemikali inayotumika kuhifadhi maiti, mfano formalin......hivi inaingia akilini utumie formalin kwenye samaki na isilete usumbufu kwa watu wanaohusika na wateja kwa kupiga chafya au kuwashwa machoni? Hizo kemikali are very pungent ukiifungua kidogo tu hapawezi kukalika.

Kama swala ni saratani inasabbishwa na hivyo vitu kutumika kuhifadhia samaki, logic inaonyesha kwamba case za saratani zingekuwa nyingi mikoa ya mbali na Mwanza maana ndo watatumia zaidi samaki waliohifadhiwa kuliko Mwanza ambako tutategemea watu wengi wanatumia samaki fresh ambao hawajahifadjiwa na kitu chochote.
Hawa watu wanajaribu kupotosha kiini cha saratani kuwa juu huko Mwanza sijui kwa maslahi ya nani. Wafanye utafiti wenye mashiko, tatizo la saratani kuwa juu kanda ya ziwa ni kutokana na kemikali za migodini zinazoelekezwa kwenye vyanzo vya maji ikiwemo mito na kuishia ziwani. Haya ndo yaleyale ya tume ya Manyere kwamba samaki wa mto Mara walikufa kutokana na kuzidiwa na kinyesi na mikojo ya ng'ombe. Pathetic!!
Wanalenga kuhujumu Uchumi wa Kanda ya ziwa, wakikwepa UKWELI juu ya ZEBAKI inayotumiwa na wachimbaji wadogo na Makampuni hutiririsha maji hayo ktk mito na ziwani.

Sgang wanakomeshwa.
 
Hadi hali ifikie kuwa mbaya kiasi hicho, mabwana na mabibi afya wanakuwa wapi kufuatilia?
Au nchi hii ni kubwa kuliko uwezo wa viongozi na watendaji husika?
Ni aibu!
 
Hizo ni story mkuu, formalin unaiweka vipi kwenye nyama? na humo ndani ya bucha kuna mtu atakaa humo kwa harufu, kupiga chafya na kuwashwa machoni, au wanatumiaje.....labda watuelimishe.
Kwa hilo makamu alilopoka kama sio msomi, kama Dr PhD angejiuliza kwanza bei ya hiyo chemical na bei ya samaki kwanza, na hizi samaki zinasabazwa Tz nzima hasa dares salama kama ni salatani ingekua dar kwanza sio mwanza, kwa uzoefu wangu watu wa mwanza 70% wanakula sana daga na flu ambazo zinakua fresh, sato na sangara wana uzwa viwandani au Dar.....
 
Swali ni kuwa hayo hao samaki wanaohifadhiwa Kwa maji ya maiti wanauzwa Kanda ya ziwa pekee?

Kwann ihusishwe na kukua Kwa UGONJWA wa saratani Kanda ya ziwa pekee?

Kanda ya ziwa mostly hula samaki fresh Kutoka ziwani ambao hawajahifadhiwa Kwa friji.

Samaki wa Kanda ya ziwa wanasafirishwa Nchi nzima na duniani kote dagaa wakiwemo.

Kwann maji hayo yawe Kwa samaki Kanda ya. Ziwa pekee?

Kwann isiwe Kwa Nchi nzima?

Pwani hawatumii maji hayo Kwa samaki wa baharini?

Nijuavyo mm watu wa gizani huyatumia ktk vyakula vyote ikiwamo NYAMA ktk butchers. Wanaamini biashara itaongezeka.

Makamo wa Rais kama mamlaka haoni kuwa alitakiwa ashughulike tatizo kimya kimya Ili wahalifu wasibadili njia zao?

Maana mataifa ya nje yanayonunua samaki wanaweza sitisha biashara ya kununua samaki!!!!

Naona viongozi wetu wanakosa MAONO, mabadiliko ni lazima Ili Taifa lisiangamie.



S.gang wanakomeshwa[emoji3][emoji3][emoji3]
Ukweli ni kwamba:

1) japo samaki wa kanda ya ziwa wanasafirishwa kwenda mikoa mingine lakini siyo kwa kiasi kikubwa. Na kuna watu katika mikoa mingine hawajawahi hata kuonja samaki wa kanda ya ziwa.

2) Zaidi ya 90% ya samaki wanaouzwa kwenye maeneo mbalimbali ya miji ya kanda ya ziwa huwa wamehifadhiwa kwenye maboksi ya barafu, na huwa kuna taarifa kuwa barafu hizo huwa zinatoka kwenye mashine zilizopo hospitalini (sina uhakika kama ni kweli).

3) si kweli kuwa wakazi wa mikoa hii hawatumii samaki waliohifadhiwa kwenye barafu au kuwekwa dawa nyingine ili samaki wasiharibike. Wafanyabiashara hawawezi kuwauza samaki wote wakamalizika kwa siku moja.

4) nenda hata hapo ferry jirani na posta, Mwanza, kwa wauza samaki. Huwezi kuona nzi yeyote kwenye samaki, ni kwa nini? Wakati samaki ana harufu kali ya kuvuta samaki kuliko nyama ya ng'ombe, mbuzi au kuku.

5) mamlaka za serikali zifanye kazi. Ziharamishe njia zozote za kuhifadhi nyama na vyakula vingine ambazo siyo salama kiafya. Na vyakula vyote vilivyotunzwa kwa njia hatari kiafya, viteketezwe. Ikifanyika mara kadhaa, hakuna atakayetumia njia hizo.
 
Maanina
Kuanzia leo sili Samaki maji baridi hafi kieleweke.

Samami.maji chumvi huwezi kuwahofadhi kwa maji ya maiti i bet
Wamekuset umejaa, tatizo ni kubwa kuliko unavyofikiri.

Mfanya biashara yeyote wa samaki au butcher duniani kote anaenda Kwa mganga hutumia maji hayo,

Si maji tu hata nyama ya binadamu watu hulishwa wanunuapo nyama.

Kanda ya ziwa migodi ndo sababu kubwa ya saratani, ZEBAKI inatiririshwa mitoni na ziwani.
 
Hizo ni story mkuu, formalin unaiweka vipi kwenye nyama? na humo ndani ya bucha kuna mtu atakaa humo kwa harufu, kupiga chafya na kuwashwa machoni, au wanatumiaje.....labda watuelimishe.
Unafahamu mazingira ambayo samaki kanda ya ziwa huwa wanauzwa? Sijaona samaki wakiuzwa sehemu iliyofungwa, labda kwenye viwanda vya samaki. Maeneo yote samaki huuzwa maeneo ya wazi, na mara nyingi ni kwenye fukwe za ziwa.
 
Tafiti nyingi zinahitajika ili kujiridhirisha kama kweli maji yaliyoosha Maiti yanasababisha Kansa! Vinginevyo hali ingekuwa mbaya kote nchini,maana mbali na wakazi wa Kanda ya Ziwa lakini mikoa mingine tunakula samaki wa kutoka huko hasahasa Sangala na Sato lakini hatujaathirika za ulaji wa samaki hao!
Samaki wa kanda ya ziwa, huliwa kwa kiasi kidogo sana katika mikoa mingine, na ni watu wachache wanaowala. Ba wengine hata hawajui hao samaki wa kanda ya ziwa wapoje?
 
Back
Top Bottom