DOKEZO Maji ya kuoshea maiti yanayo lalamikiwa kutumika kuhifadhia samaki yanauzwa kwenye maduka ya dawa za asili, Serikali imulike huko

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Nyama za watu ??? !!
 
Absolutely right! Wanatumia Ile dawa ya kuhifadhia maiti I think inaitwa formaline (sp) huenda ndio alichomaanisha
 
Migodi kutiririsha zebaki ziwani mf Nyamongo Barrick wametuhumiwa Kwa KASHFA hiyo.

Ni maji zaidi Wala Si samaki. Serikali isitafite pa kujificha MIGODI ya madini ya wazawa na Wawekezaji ni tatizo kubwa.
 
Kwa hiyo ofisi ya Mkuu wa Mkoa wanapotoa pesa ili kuzuia hiyo story isitoke lengo lao watu wazidi kuathirika?

Kama hii story ni kweli, inashangaza kuona tuna pesa za kukuza matatizo, lakini
hatuna pesa za kutatua matatizo yetu.
 
Wanalenga kuhujumu Uchumi wa Kanda ya ziwa, wakikwepa UKWELI juu ya ZEBAKI inayotumiwa na wachimbaji wadogo na Makampuni hutiririsha maji hayo ktk mito na ziwani.

Sgang wanakomeshwa.
 
Hadi hali ifikie kuwa mbaya kiasi hicho, mabwana na mabibi afya wanakuwa wapi kufuatilia?
Au nchi hii ni kubwa kuliko uwezo wa viongozi na watendaji husika?
Ni aibu!
 
Hizo ni story mkuu, formalin unaiweka vipi kwenye nyama? na humo ndani ya bucha kuna mtu atakaa humo kwa harufu, kupiga chafya na kuwashwa machoni, au wanatumiaje.....labda watuelimishe.
Kwa hilo makamu alilopoka kama sio msomi, kama Dr PhD angejiuliza kwanza bei ya hiyo chemical na bei ya samaki kwanza, na hizi samaki zinasabazwa Tz nzima hasa dares salama kama ni salatani ingekua dar kwanza sio mwanza, kwa uzoefu wangu watu wa mwanza 70% wanakula sana daga na flu ambazo zinakua fresh, sato na sangara wana uzwa viwandani au Dar.....
 
Ukweli ni kwamba:

1) japo samaki wa kanda ya ziwa wanasafirishwa kwenda mikoa mingine lakini siyo kwa kiasi kikubwa. Na kuna watu katika mikoa mingine hawajawahi hata kuonja samaki wa kanda ya ziwa.

2) Zaidi ya 90% ya samaki wanaouzwa kwenye maeneo mbalimbali ya miji ya kanda ya ziwa huwa wamehifadhiwa kwenye maboksi ya barafu, na huwa kuna taarifa kuwa barafu hizo huwa zinatoka kwenye mashine zilizopo hospitalini (sina uhakika kama ni kweli).

3) si kweli kuwa wakazi wa mikoa hii hawatumii samaki waliohifadhiwa kwenye barafu au kuwekwa dawa nyingine ili samaki wasiharibike. Wafanyabiashara hawawezi kuwauza samaki wote wakamalizika kwa siku moja.

4) nenda hata hapo ferry jirani na posta, Mwanza, kwa wauza samaki. Huwezi kuona nzi yeyote kwenye samaki, ni kwa nini? Wakati samaki ana harufu kali ya kuvuta samaki kuliko nyama ya ng'ombe, mbuzi au kuku.

5) mamlaka za serikali zifanye kazi. Ziharamishe njia zozote za kuhifadhi nyama na vyakula vingine ambazo siyo salama kiafya. Na vyakula vyote vilivyotunzwa kwa njia hatari kiafya, viteketezwe. Ikifanyika mara kadhaa, hakuna atakayetumia njia hizo.
 
Rafiki yangu Dinazarde bado nakupenda hama huko Mwanza kwa mustakabali wa maisha yako[emoji2][emoji2]
 
Maanina
Kuanzia leo sili Samaki maji baridi hafi kieleweke.

Samami.maji chumvi huwezi kuwahofadhi kwa maji ya maiti i bet
Wamekuset umejaa, tatizo ni kubwa kuliko unavyofikiri.

Mfanya biashara yeyote wa samaki au butcher duniani kote anaenda Kwa mganga hutumia maji hayo,

Si maji tu hata nyama ya binadamu watu hulishwa wanunuapo nyama.

Kanda ya ziwa migodi ndo sababu kubwa ya saratani, ZEBAKI inatiririshwa mitoni na ziwani.
 
Hizo ni story mkuu, formalin unaiweka vipi kwenye nyama? na humo ndani ya bucha kuna mtu atakaa humo kwa harufu, kupiga chafya na kuwashwa machoni, au wanatumiaje.....labda watuelimishe.
Unafahamu mazingira ambayo samaki kanda ya ziwa huwa wanauzwa? Sijaona samaki wakiuzwa sehemu iliyofungwa, labda kwenye viwanda vya samaki. Maeneo yote samaki huuzwa maeneo ya wazi, na mara nyingi ni kwenye fukwe za ziwa.
 
Samaki wa kanda ya ziwa, huliwa kwa kiasi kidogo sana katika mikoa mingine, na ni watu wachache wanaowala. Ba wengine hata hawajui hao samaki wa kanda ya ziwa wapoje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…