Majimbo ya Ubunge yaliyosimamisha wagombea wa CCM bila wagombea wa Upinzani
Unaposema "Mholanzi" sio sawa kabisa na huo utakuwa ni ubaguzi.

Baba yake alikuwa ni Mtanzania mwenye asili ya uholanzi na mama yake ni Mzigua wa huko Turiani hivyo Jonas ni Mtanzania, sasa leteni hoja za kuipinga uteuzi wake lakini msilete hoja za kibaguzi kama walivyokuwa makaburu wa Afrika kusini waliowabagua waafrika kwa ajili ya Uafrika na rangi yao.
Na niwe mbaguzi tu,lakini imenikera.Kama angekuwa anafaa nisingejali.Hapa haukuangaliwa weledi ila maslahi na ni mwenzetu.
 
CCM ukisha kuwa na pesa maamuzi ya wana Nchi yapo chini yako ata ukiwaibia pengine ata kuwauwa utamalizana na Dpp!
 
Hii la kupita bila kupingwa haijakaa vizuri tunawanyima haki ya kuchagua viongozi wananchi wao
 
Picha zinakua zimegongwa muhuri na unakua umegusa karatasi..SASA kama alikua mbunge wa viti maalum na alijaziwa kule ofisini na wataalamu ni vigumu kukosea but now kuna pirika kibao kwenye hivyo vyama na kila mmoja anapambana kivyake but we angalia CCM
Sio kweli
 
Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Mvomero Mkoani Morogoro,Hassani Njama amethibitisha kuwa Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Jonas Van Zeland amepita bila kupingwa baada ya kile alichotaja ni kutokana na Wagombea wa Vyama vingine kutokidhi baadhi ya vigezo
Huyu Ni mtanzania mwenye asili ya ulaya?
 
Mkuu,unaweza kutueleza kati ya haya majimbo ni mangapi ambayo wagombea wa CCM walikuwa peke yao 'pure' yahani ambayo wapinzani hawakuenguliwa kwa sababu zozote?.
Mpayukaji kasema atawaingizeni barabarani,vipi mtaingizwa lini barabarani maana Hadi Sasa 20-0.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Huwezi kushiriki uchaguzi Kwa muda mrefu kama CCM walivyoshiriki na ukashindwa kujaza form, nadhani CCM Wana resources na experience kubwa compared to other parties ambazo to be honest vingine ata ofisi ya kujazia hizo forms hawana..
Hakuna resources wala nini

Mfano mtu anarudisha fomu Mkurugenzi hayupo, mtu anaporwa fomu.
 
Nafasi ya kukata rufaa kwa tume ya uchaguzi ipo, hivyo basi dhamana waliobaki nayo ni Tume ya kuamua Kama Wapinzani wanarudishwa au hawarudishwi
 
Picha zinakua zimegongwa muhuri na unakua umegusa karatasi..SASA kama alikua mbunge wa viti maalum na alijaziwa kule ofisini na wataalamu ni vigumu kukosea but now kuna pirika kibao kwenye hivyo vyama na kila mmoja anapambana kivyake but we angalia CCM..wenyeviti,makatibu wa mikoa na wilaya wengi wako maofisini kuwasaidia wagombea wao.. tofauti na vyama vingine unakuta kuanzia Mwenyekiti wa Taifa na safu nzima ya Viongozi wa kitaifa,Mkoa na Jimbo wote wanagombea ubunge,udiwani hata urais...as the result hawana officials ambao wametulia kuwapa miongozo na msaada wa kiofisi...na mbaya zaidi siku ya kurejesha form ni moja tuu na deadline ni saa 10.
Kwani hata kama imegongwa muhuri ndio haiwezi kutolewa? Msimamizi akisema fomu amepokea haina picha utamfanya nini?

Kuhusu viongozi wa chama kugombea ndio useme kuwa hawana muda wa kuwasaidia wagombea wao sidhani kama ina mashiko.

Mfano sidhani kama kuna wilaya yenye majimbo zaidi ya mawili, sasa wakikutana kwa masaa matatu tu kujaza fomu kwa ufasaha kwa pamoja itashindikana?

Mbona hujazungumzia issue za kutekwa, kubambikwa mashitaka, kupewa vitisho, kunyimwa fomu ama kukimbiwa na wasimamizi wa uchaguzi wakati wa kurejesha fomu?

Kwamba haya yote nayo yanatokea kwa bahati mbaya kwa wapinzani pekee? Ukisum up hayo yote utagundua hakuna bahati mbaya hayo yote ni planned na ccm na serikali yake.

Magufuli alisema hadharani kuwa anawapa mshahara, magari nk ole wao wamtangaze mpinzani kashinda, hizi sarakasi zinaonesha wasimamizi wanahaha kulinda ajira zao kwa kuhakikisha ccm inashinda kwa kila mmoja kutengeneza figisu zake kwa kuzingatia kauli ya rais.
 
Back
Top Bottom