Makinda abadili gia angani, asema kuhesabiwa ni siku saba

Makinda abadili gia angani, asema kuhesabiwa ni siku saba

Naona kama zoezi limefail,mtaa ninaoishi hakuna nyumba imehesabiwa...... inawezekana wamepunguza manpower Ili wapige hela,na zoezi linasuasua,wasiponiona leo hawawezi kunipata tena...........labda watoe link tujihesabu wenyewe
 
Aacha utoto, kinachohesabika ni tarehe ya 23/8/2022 hata karani akifika kwako mwezi wa 10 atakuuliza waliolala kwako siku ya 23/08/2022

Uko sahihi, hebu nisaidie hili. Leo niko Mwanza kikazi na sijahesabiwa hapa, narudi alhamisi Dar ambako ndiko makazi yangu yalipo. Je sintokuwa na sifa ya kuhesabiwa huko Dar maana sikuamkia huko tarehe 23/8/22?
 
Maswali kama haya sikuona ulazima wake
  • Una simu janja
  • Una computer
  • Una baiskel, pikipiki
  • Una driving licence, card ya nida, kadi ya mpigakura
  • Nyumba imesakafiwa kwa material gani
  • Una runinga
  • Una paka, mbwa, bata, kuku nk
  • Choo yako ni ya namna gani
  • Umeshawahi kusafiri ndani ya mwezi huu
Jiongeze.... ccm wanataka uhalali wa kutanua wigo wa tozo!
 
Uko sahihi, hebu nisaidie hili. Leo niko Mwanza kikazi na sijahesabiwa hapa, narudi alhamisi Dar ambako ndiko makazi yangu yalipo. Je sintokuwa na sifa ya kuhesabiwa huko Dar maana sikuamkia huko tarehe 23/8/22?
Mzee mgumu sana kuelewa? Wewe kuhesabiwa au kutokuhesabiwa hakuwezi kuzuia zoezi kuendelea na kuisha!
Na hata ukiangalia zoezi zima na maswali yalivyo ni kama unavolunteer kutoa taarifa zako... Usubiri waje sawa. Wakikukosa sawa! Udanganye taarifa sawa... useme ukweli sawa. Ni wewe tu.
Vyovyote vile ni sawa kwao!!
 
Kupika data naina kuna kaugumu sana. Kwanza tablet wanayotumia imeungwa na GPS. Nyumba utakayofika kuhesabu imeshasajiliwa kuwa ni ya nani. Kama ukirekodi kuwa umemhesabu mtu flani kwenye makazi flani na taarifa zikatofautiana na zilizoko kwenye rekodi, waweza kujitengenezea msala.

Hamna umakini huo ndugu, usitake kuonyesha ni zoezi lenye umakini wa kiwango hicho, wakati hata maswali yenyewe yameanza kuonekana jana kwenye mitandao. Inshort ni zoezi linaloendeshwa kijima sana, na hayo ni baadhi ya maeneo unayoweza kupima uwezo wa watendaji wetu ndani ya serikali.
 
Jamani mimi nashindwa kuelewa, hivi hatujawai kuhesabiwa? Hii ni mara ya kwanza?

Karani hata akija kesho kutwa yeye atakua interested na watu waliolala tarehe 23.

Kiuhalisia, ingewezekanaje kuhesabu watu wote kwa siku moja?

Tuwe wavumilivu,tutulie leo siku ya kwanza, tuwape muda, changamoto zitakuwepo lakini ni kazi gani inakosa changamoto.

Wakati nasoma o level, chemistry, ilikua tukiingia lab kufanya test mwalimu alikua anasema " ukiona umepata jibu haraka ujue umekosea" nataka kusema nini?

Zoezi hili ni la kitaifa litachukua walau siku kadhaa kufanikishwa, lingekua rahisi mimi ningemkumbuka mwalimu wangu kuwa " ukiona unapata jibu haraka ujue umekosea"

Tuwe watulivu, tutahesabiwa.
 
Unafahamu kitu inaitwa Recall bias? Nani atakupa taarifa sahihi ya kilichotokea siku 7 zilizopita (ikiwa itaishia siku ya saba?) Bora wangepitisha karatasi zenye kukusanya taarifa katika kaya, ili hii leo raia wangezijaza halafu wakaja kuzikusanya ndani ya siku 7 zao na kuweka marekebisho panapostahili.
Tatizo lako wewe unataka usahahi wa mchakato ili kupata taarifa sahihi.
Wenzako wapo kimkakati wanatumia random sampling kuja kujustify population data na nini kiingie kwenye vision 2025-2035!
Nipo hapa... wangefanya unavohitaji nina imani final population data wangeikuta 80+M people.
Subiria watakavofanya data cleaning na kuondosha ama kuongeza ya kwao ili kufurahisha international community!
 
Kwa kifupi ni kwamba, taarifa zinazotakiwa kwenye sensa ni zile za kuamkia tarehe 23.08.2022.
Kwa hiyo, hata kama Karani wa Sensa atakuja kwako tarehe 25 au 28.08.2022, wewe utampa taarifa kama ilivyokuwa tarehe 23.08.2022.
Watu waliolala katika Nyumba yako usiku wa kuamkia tarehe hiyo 23.08.2022.
 
Hamna umakini huo ndugu, usitake kuonyesha ni zoezi lenye umakini wa kiwango hicho, wakati hata maswali yenyewe yameanza kuonekana jana kwenye mitandao. Inshort ni zoezi linaloendeshwa kijima sana, na hayo ni baadhi ya maeneo unayoweza kupima uwezo wa watendaji wetu ndani ya serikali.
Mkuu... Maswali kuonekana wala si tatizo ni haki. Kwa kuwa ni zoezi linalotumia fedha za umma lilitakiwa kuwa wazi sana.
Wangekua kweli wapo makini na wanahitaji taatifa sahihi... wangejaribu kuweka hata online links wenye NIDs waingie wajibu maswali kurahisisha mchakato.
Hilo la kutegemea GPS ndo kabisa litaongeza errors.

Nazidi kushikilia msimamo kuwa huu wote ni usanii na mchongo... Statistically tayari wana inferences zao. Wanataka tu kujustify!
 
Sasa mbona hawakutuambia tuweke kumbukumbu ya tarehe 23 tu. Tuliambiwa sensa inahesabu watu waliolala nyumbani siku anayopita karani na ikibidi karani anaweza kukagua ili kujiridhisha.

Hawa watu hawakujiandaa na wameshafeli. Anyway wapige hizo hela za walipa tozo na kodi wakapumzike maana ndio kilichobaki kwa serikali hii.
 
Zoezi lote ni la mchongo wa upigaji... kuna watu baada ya zoezi lazima wanunue viwanja, magari, nyumba n.k kwa mchongo huu wa sensa
Kweli hili zoezi nataka nilifananishe na vitambulisho vya nida 🙂 sarakasi nyingi
 
Kwa kifupi ni kwamba, taarifa zinazotakiwa kwenye sensa ni zile za kuamkia tarehe 23.08.2022.
Kwa hiyo, hata kama Karani wa Sensa atakuja kwako tarehe 25 au 28.08.2022, wewe utampa taarifa kama ilivyokuwa tarehe 23.08.2022.
Watu waliolala katika Nyumba yako usiku wa kuamkia tarehe hiyo 23.08.2022.
Ndo hizo hizo hawatapata za kweli sasa na ni loop hole ya wao kupika data!
 
Sasa mbona hawakutuambia tuweke kumbukumbu ya tarehe 23 tu. Tuliambiwa sensa inahesabu watu waliolala nyumbani siku anayopita karani na ikibidi karani anaweza kukagua ili kujiridhisha...
Mbona taarifa ilitoka kwamba sensa ni siku sita hadi saba, hivyo unapaswa kuweka kumbukumbu za watu waliolala usiku wa kuamkia tarehe 23.
 
Wangeongeza Makarani wafanye kwa siku 2 tu na zote ziwe mapumziko
Basi wangeongeza vishikwambi na makarani. Au wangepunguza maswali toka 100 ya Sasa na kubakia 3 tu.

Ili ndani ya dakika 10 kaya 5 zihesabiwe.
 
Wakati mwingine naona watanzania na serikali yenyewe tuna complicate mambo sana, hata kama mtu asipohesabiwa mwisho wa siku sioni kitakachoongezeka au kupungua kwenye mahitaji ya jamii yetu.

Hizi sensa zimekuwepo 2002, ikaja tena 2012, lakini bado mpaka leo kuna upungufu wa ajira kwa vijana, huduma za afya, matundu ya vyoo kwenye baadhi ya shule na madawati bado ni shida!, hata maji safi na salama sehemu nyingine huku mijini nayo hayapo!

Kama kweli majibu ya hayo matatizo yetu ni sensa, mbona hizo zilizofanyika miaka iliyopita bado hazikuleta majibu ya hayo matatizo yetu? simply, naona hili zoezi limepigiwa debe sana mpaka tumeleweshwa.
 
Back
Top Bottom