Makinda abadili gia angani, asema kuhesabiwa ni siku saba

Makinda abadili gia angani, asema kuhesabiwa ni siku saba

Nimekaa nyumbani mpaka saa 12 jioni na karani hakuja.... Kwa hiyo kesho naendelea na mishe zangu....
 
Tuliambiwa siku ya sensa ni tar.23/8/2022, baada ya hapo watu waendelee na mishe zao. Na Mimi nazingatia hilo, kesho tusitafutane.
 
Kuna mapungufu mengi, leo asubuhi nimefikiwa na karani kuhesabiwa saa 3:53, saa 5:27 nikapokea mgeni aliyetoka safari Kigoma wakati karani ameshaondoka, nikajiuliza, huyu ni mgeni mmoja, je kuna watu wangapi wako safarini na huko waendako watafika wenyeji wao wameshahesabiwa, je ni watu wangapi wameamkia kwenye hotels, lodgings na guest houses wataingiaje kwenye takwimu?
Tatizo mnafuatilia mambo juu juu...Hao wanahesabiwa kwenye dodoso la makundi maalumu Yaani waliolala stendi, lodge, masokoni, watoto wa mitaani etc Kazi ilianza usiku ya kuhesabu makundi hayo

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Kuna mapungufu mengi, leo asubuhi nimefikiwa na karani kuhesabiwa saa 3:53, saa 5:27 nikapokea mgeni aliyetoka safari Kigoma wakati karani ameshaondoka, nikajiuliza, huyu ni mgeni mmoja, je kuna watu wangapi wako safarini na huko waendako watafika wenyeji wao wameshahesabiwa, je ni watu wangapi wameamkia kwenye hotels, lodgings na guest houses wataingiaje kwenye takwimu?
Tatizo mnafuatilia mambo juu juu, hao wanahesabiwa kwenye dodoso la makundi maalumu...Wasiokuwa na makazi maalumu, waliolala stendi, masokoni,lodge, kwenye makambi, watoto wa mtaani. Ambapo kazi ilianza tangu saa 6 usiku kwajili ya makundi hayo

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Kwa walioko safarini ikiwa walilala nyumba za wageni au kituo cha bus, ilipaswa karani apite usiku kuwahesabu na wangepewa beji maalum yakuonesha kuwa wamehesabiwa (dodoso lao ni maalum) Kama alilala nyumbani, basi hapo alipolala wanapaswa kutoa taarifa zake.

Dokezo langu: inasikitisha ikiwa hadi mwanajf hajui kuhusu utaratibu wa wanaotakiwa kuhesabiwa. Je, huko sigimbi?
Mbwembwe zote zile za hamasa zilikuwa na faida gani ikiwa watu hawajui utaratibu?[emoji848]
Kama mtu alikesha kwenye shughuli za ulinzi kuamkia tarehe 23 ya sensa then hakuhesabiwa sehemu alipokesha na hakulala nyumbani, huyo atahesabiwaje kwasababu tunaambiwa ni watu waliolala ndani ya nyumba husika usiku wa kuamkia sensa ndiyo tuwatolee taarifa zao.
 
Uko sahihi, hebu nisaidie hili. Leo niko Mwanza kikazi na sijahesabiwa hapa, narudi alhamisi Dar ambako ndiko makazi yangu yalipo. Je sintokuwa na sifa ya kuhesabiwa huko Dar maana sikuamkia huko tarehe 23/8/22?
Maswali mengine bwana!! Kuna watu hata vyombo vya habari huwa hamsikilizi..Suala hili lishazungumziwa sana hadi mitandaoni humu...Kwamba utaacha taarifa zako ulipolala usiku wa kuamkia tarehe 23. Endapo watahitaji kufahamu zaidi utapigiwa simu

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
 
Wasiokuwa na makazi maalumu, waliolala stendi, masokoni,lodge, kwenye makambi, watoto wa mtaani. Ambapo kazi ilianza tangu saa 6 usiku kwajili ya makundi hayo
Zoezi limeanza leo, kuna watu wamesafiri usiku kucha w barabarani, wao wenyewe wamekiri kutohesabiwa wala kukutana na makarani wewe unalazimisha kuwa wamehesabiwa huko ulikotaja mbona unabishia jambo lililowazi!
 
Maswali mengine bwana!! Kuna watu hata vyombo vya habari huwa hamsikilizi..Suala hili lishazungumziwa sana hadi mitandaoni humu...Kwamba utaacha taarifa zako ulipolala usiku wa kuamkia tarehe 23. Endapo watahitaji kufahamu zaidi utapigiwa simu

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app
Kuna watu walidandia fuso jana Kiomboi wamesafiri usiku kucha kwenye gari, mtazungukia magari yote kusaka taarifa zao?
 
Wamekula Bill 900. Wame hujumu idadi ya Makarani. Mm licha ya kushinda nyumbani sija hesabiwa. Hivyo tusimbuane tena!!
 
Kutoka moyoni tumekwazika tumesubiri makarani kutwa nzima kumbe ni zoezi la siku saba.

Kama ni zoezi endelevu kwanini leo ikawe mapumziko,

Sensa ya kuhesabu siku saba itakupa majibu ya uongo maana watu hawatulii sehemu moja kama mawe

Kuna watu hawatahesabiwa au watahesabiwa mara mbili bila kujijua

Mfano leo nipo kwangu Lushoto leo hamjaja. Kesho nitakuwa safarini Ludewa ndio mtakuja kwangu Lushoto, nikifika Ludewa nitakuta mmeshapita, hapo nani kamchenga mwenzake.

Zoezi mmeliharibu wenyewe
Kweli Usilolijua ni sawa na usiku wa giza.Nakuhakikishia hayo unayoyazungumzia yalishatambuliwa na yalishapatiwa ufumbuzi na namna ya kukabiliana nalo. Hata ukiwa safarini wiki nzima au hata ukiwa huko migodini lazima utahesabiwa tu
 
Sasa mbona hawakutuambia tuweke kumbukumbu ya tarehe 23 tu. Tuliambiwa sensa inahesabu watu waliolala nyumbani siku anayopita karani na ikibidi karani anaweza kukagua ili kujiridhisha.

Hawa watu hawakujiandaa na wameshafeli. Anyway wapige hizo hela za walipa tozo na kodi wakapumzike maana ndio kilichobaki kwa serikali hii.
Wacha uzushi. Nani alikwambia hayo maneno? Watu milioni 60 Kwa siku moja?! Imetokea wapi Dunia hii?
 
Kuna mapungufu mengi, leo asubuhi nimefikiwa na karani kuhesabiwa saa 3:53, saa 5:27 nikapokea mgeni aliyetoka safari Kigoma wakati karani ameshaondoka, nikajiuliza, huyu ni mgeni mmoja, je kuna watu wangapi wako safarini na huko waendako watafika wenyeji wao wameshahesabiwa, je ni watu wangapi wameamkia kwenye hotels, lodgings na guest houses wataingiaje kwenye takwimu?
Kuna madodoso ya makundi maalum mfn wasafiri waliolala guest house watoto wa mitaani makahaba wanaojiuza waliolazwa mahospitalini walio kwenye mabweni mahotelini n.k kwa kifupi hakuna atakayeachwa usidhani hilo halikuwekwa katika consideration
 
Maswali mengine bwana!! Kuna watu hata vyombo vya habari huwa hamsikilizi..Suala hili lishazungumziwa sana hadi mitandaoni humu...Kwamba utaacha taarifa zako ulipolala usiku wa kuamkia tarehe 23. Endapo watahitaji kufahamu zaidi utapigiwa simu

Sent from my SM-A217F using JamiiForums mobile app

Kwahiyo niache taarifa zangu guest house niliyolala jana wakati mimi sio mkazi wa huku?
 
Kwahiyo niache taarifa zangu guest house niliyolala jana wakati mimi sio mkazi wa huku?
Ndio, huko kwenye magesti kuliachwa fomu ambapo mtu yoyote aliyeamkia hapo guest au hotelini atajaza na baadae karani atazichukua na kuingiza taarifa zao kwenye mfumo. Japo maswali yataphngua sio kama ya watakao hojiwa kwenye kaya binafsi
 
Faida ya kutofanya maamuzi kiweredi!...wangejiri makarani wengi..kupunguza siku na gharama( waliosoma project planning wataelewa namaanisha nn)
 
Back
Top Bottom