Makinda abadili gia angani, asema kuhesabiwa ni siku saba

Makinda abadili gia angani, asema kuhesabiwa ni siku saba

Dokezo langu: inasikitisha ikiwa hadi mwanajf hajui kuhusu utaratibu wa wanaotakiwa kuhesabiwa. Je, huko sigimbi?
Mbwembwe zote zile za hamasa zilikuwa na faida gani ikiwa watu hawajui utaratibu?🤔
Hii si changamoto yangu, nimesema nilichokishuhudia , anyway sijui kosa langu ni lipi
 
Huyu aliyefika kwangu saa 5 hajakutana na karani popote, in other words wamesafiri usiku kucha
Duh, sasa tunawasaidiaje watu wa takwimu- NBS?
Maana hata kama karani angemkuta kwako kesho...bado swali lingehusu waliolala hapo usiki wa kuamkia tarehe 23!

Je, ni wa kiume au wa kike?🤔
Kama ni wa kiume aisee, afanye kila jitihada ahesabiwe. Habari za takwimu kuonesha wanaume ni wachache kuliko wanawake, na kumbe wengine hawajahesabiwa si sawa kabisaa.
Maana wanaume wengi wako huko machimboni, migodini nk wanasaka noti
!
 
Swali la maji nimewajibu tunatumia maji ya bowser yanayouzwa na MORUWASA.
 
Kabisa. Leo siku ya mapumziko makarani wa sensa walipaswa kupita kila kaya na kugawa makaratasi ya madodoso

. Kisha wananchi wayajaze na kuyaancha nyumbani. Ili kuanzia kesho makarani wangekuwa wakipita na kukuta taarifa zote za kaya
Ahaaa huku tandale ingekuwa vurugu wangechafua chafua kisingesomeka kitu
 
Basi wangeongeza vishikwambi na makarani. Au wangepunguza maswali toka 100 ya Sasa na kubakia 3 tu.

Ili ndani ya dakika 10 kaya 5 zihesabiwe.
Maswali ni mengi sana yameharibu zoezi
 
These are going to cook data. hawatampata mtu kuanzia kesho, tumepoteza muda kuwasubiri imetoka hiyo .. rubbish! johnthebaptist
Kupika data naina kuna kaugumu sana. Kwanza tablet wanayotumia imeungwa na GPS. Nyumba utakayofika kuhesabu imeshasajiliwa kuwa ni ya nani. Kama ukirekodi kuwa umemhesabu mtu flani kwenye makazi flani na taarifa zikatofautiana na zilizoko kwenye rekodi, waweza kujitengenezea msala.
 
Nmekaa siku nzima nyumbani, nimeacha mishe zangu ngingi mpaka sasa hola, kesho hawatanikuta home, imetoka hiyo!!

Hili zoezi lilitakiwa wajipange wamalize leo leo!! Mpaka kesho hawatampata mtu tena,,

Worst planning of our resources!! Sijaona sababu ya kufanya sensa kwa siku nzima!!


Lilikuwa suala la kumpangia kila karani angalau kaya 10 mpaka 20 asubuhi mpaka jioni wangemaliza vizuri tu!!

Otherwise its prolonged for their own benefits!!
 
Maswali ni mengi sana yameharibu zoezi
Maswali kama haya sikuona ulazima wake
  • Una simu janja
  • Una computer
  • Una baiskel, pikipiki
  • Una driving licence, card ya nida, kadi ya mpigakura
  • Nyumba imesakafiwa kwa material gani
  • Una runinga
  • Una paka, mbwa, bata, kuku nk
  • Choo yako ni ya namna gani
  • Umeshawahi kusafiri ndani ya mwezi huu
 
Kwa walioko safarini ikiwa walilala nyumba za wageni au kituo cha bus, ilipaswa karani apite usiku kuwahesabu na wangepewa beji maalum yakuonesha kuwa wamehesabiwa (dodoso lao ni maalum) Kama alilala nyumbani, basi hapo alipolala wanapaswa kutoa taarifa zake.

Dokezo langu: inasikitisha ikiwa hadi mwanajf hajui kuhusu utaratibu wa wanaotakiwa kuhesabiwa. Je, huko sigimbi?
Mbwembwe zote zile za hamasa zilikuwa na faida gani ikiwa watu hawajui utaratibu?🤔
Ndugu Lanlady , huo ulioandika ndio ukweli.
Nimeuona huku Rufiji nilipo kwa sasa.
Watu hawana elimu kabisa ya sensa wala hajui nini kinaulizwa.
 
Kutoka moyoni tumekwazika tumesubiri makarani kutwa nzima kumbe ni zoezi la siku saba.

Kama ni zoezi endelevu kwanini leo ikawe mapumziko,

Sensa ya kuhesabu siku saba itakupa majibu ya uongo maana watu hawatulii sehemu moja kama mawe

Kuna watu hawatahesabiwa au watahesabiwa mara mbili bila kujijua

Mfano leo nipo kwangu Lushoto leo hamjaja. Kesho nitakuwa safarini Ludewa ndio mtakuja kwangu Lushoto, nikifika Ludewa nitakuta mmeshapita, hapo nani kamchenga mwenzake.

Zoezi mmeliharibu wenyewe
nasikia tatizo vishikwambi vichache
 
Watu kweli wagumu kuelewa.

Takwimu zinazochukuliwa ni zile za usiku wa kuamkia tar 23. Hivyo hata wakija kesho bado wataomba taarifa za usiku wa kuamkia tar 23.

Ndio maana wanasema kama unajijua mkuu wa kaya hutikuwepo wakija basi acha taarifa hapo nyumbani zihusuzo usiku wa kuamkia tar 23.
 
Sensa ni ama mahali unaposhinda wakati wote (hii kufanyika nchi zilizoendelea)

Au Sensa ni mahali ulipolala usiku wa kuamkia tarehe 23 Agusti, 2022. Hii ni sensa ya nchi zinazoendelea

Kwahiyo, we chunga tu tarehe 23 Agusti ulipoamkia hata wakija siku ya 7 majibu ni yale yale
Unafahamu kitu inaitwa Recall bias? Nani atakupa taarifa sahihi ya kilichotokea siku 7 zilizopita (ikiwa itaishia siku ya saba?) Bora wangepitisha karatasi zenye kukusanya taarifa katika kaya, ili hii leo raia wangezijaza halafu wakaja kuzikusanya ndani ya siku 7 zao na kuweka marekebisho panapostahili.
 
Watu kweli wagumu kuelewa.

Takwimu zinazochukuliwa ni zile za usiku wa kuamkia tar 23. Hivyo hata wakija kesho bado wataomba taarifa za usiku wa kuamkia tar 23.

Ndio maana wanasema kama unajijua mkuu wa kaya hutikuwepo wakija basi acha taarifa hapo nyumbani zihusuzo usiku wa kuamkia tar 23.
Kaka hilo la kusema watu hawaelewi, watanzania wangapi wanaelewa? Wana elimu hiyo ya kuelewa? Hata maswali tu ya sensa yanazunguka WhatsApp. Kuna mtu hata simu hana. Si bora wangekusanya hizo taarifa manually tu.
 
Kutoka moyoni tumekwazika tumesubiri makarani kutwa nzima kumbe ni zoezi la siku saba.

Kama ni zoezi endelevu kwanini leo ikawe mapumziko,

Sensa ya kuhesabu siku saba itakupa majibu ya uongo maana watu hawatulii sehemu moja kama mawe

Kuna watu hawatahesabiwa au watahesabiwa mara mbili bila kujijua

Mfano leo nipo kwangu Lushoto leo hamjaja. Kesho nitakuwa safarini Ludewa ndio mtakuja kwangu Lushoto, nikifika Ludewa nitakuta mmeshapita, hapo nani kamchenga mwenzake.

Zoezi mmeliharibu wenyewe
Upande wa data usiwaamini sana ccm. Uhesabiwe au laah data zitapatikana tuu!
Jiongeze, hakuna sehemu walisema watahesabu kila mtu kwa lazima!
 
Back
Top Bottom