Makonda: Hakuna nilichojifunza, nitawanyoosha. Wasiopaka rangi nyumba zao katikati ya Mji TUTABOMOA

Makonda: Hakuna nilichojifunza, nitawanyoosha. Wasiopaka rangi nyumba zao katikati ya Mji TUTABOMOA

Huyu bwana umtake usimtake utamripot tu habar zake hahaha nikiripoti kutoka jf mimi ni erythrocyte kutoka chadema kwasasa nikiwa mkoa wa arusha kulipoti taarifa za makonda kutoka ccm, ujumbe maendeleo hayana chama
Yaani nimeshangaa sana asee, jamaa kakomaa kabisa na story ya Makonda wakati CDM wana uchaguzi za kanda huko.

Badala atuandikie malengo ya viongozi wa kanda anadinkidinki na PCM 😂!
 
Jamaa kashaona CCM wenzie hawataki hvyo ameamua kujilipua tu kwanza akuandikia mtu barua akaomba kazi alikuwa ametulia zake anajilia maishaa wakamleta wakampa uenezi labda Kwa kujua alivyokaa bench kajifunza kumbe walaaaa Hana habari akawawashia moto uko uenezi hata miezi haijakata wamemtoa Kwa spid ya 5G ,wamempeleka Arusha Ili iwe njia ya kumtoaa ,n muda tu utaongeaa

CCM ya ss sitaki watu wa aina ya makonda ,inatka watu wa kusifia mama anaupigaa mwingi nakuvaa nguo zenye picha ya mama mbeleeView attachment 2958149
Hii ilikua moshi siku ya mwenge moshi wanja ulipendeza sana hongereni wana moshi kwa ujumla
 
Japo mi si timu yake ila kwenye kuboresha usafi wa jiji, kupaka rangi majengo mjini kati na kuleta sijui mabasi ya ghorofa hapo kapatia, alichosahau ni kukamia kuondoa mirungi na bangi zilizojaa mjini maana inaharibu akili za vijana hadi kujifanya hamnazo "wadudu"!!

Mbona hakuzungumzia uwanja mpya wa michezo unaojengwa au sio kipaumbele?

Arusha lazima waombe poo!! Wengine itabidi wahamie Burundi maana saa hizi ni mwendo wa kwata tu huko!

Ukweli usemwe Bimkubwa kapatia sana uteuzi kumpeleka jombaa Arusha akawachangamshe watu wote hasa wadudu!!
 
Hizi ni miongoni mwa kauli zilizotolewa na Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha katika hotuba kabambe ya Utambulisho aliyoitoa Mjini humo alipokuwa anakabidhiwa ofisi .

Hapa akikuwa akiwapa makavu waliokuwa wanamsengenya kwamba hajajifunza pamoja na kuwekwa benchi muda mrefu.
---
Makonda: Hamna nilichojifunza zaidi ya kuwashughulikia wazembe, wavivu na Wala Rushwa

View attachment 2958155
Akitoa hotuba baada ya utambulisho wake Mkuu wa Mkoa mpya wa Arusha Paul Makonda amesisitiza Viongozi wote kuwajibika na kutoa tahadhari kwa Wazembe. Akiongea mbele ya watu waliojitokeza kumpokea Paul Makonda amesema:

Mmenifurahia sana ila tutageukana muda sio mrefu. Sitajali wewe ni nani, baba yako ni nani, ulipataje hicho cheo, aidha ulipata kwa kuhonga, kwa rushwa au kwa uganga nitakula sahani moja na wewe.
Lazima kila mtu awajibike kwenye nafasi yake. Msiseme huyu alikuwa Mwenezi sasa katoka kwenye Uenezi atakuja amepoa. Wengine wanasema eti saivi labla atakuwa amejifunza, hamna nilichojifunza zaidi ya kuwashughulikia wazembe wavivu na Wala rushwa. Sina elimu yoyote mimi hata niwe Mkuu wa Mkoa wa siku moja inatosha lakini awepo mtu mmoja tu ajue kuna mwanaume amepita hapa.
Kwahiyo kila mtu kwenye nafasi yake, kama ni Mkuu wa Wilaya shika Wilaya yako barabara kama ni Mkurugenzi ishike Halmashauri yako kikamilifu.

Makonda: Majengo yaliyopauka yaliyo katikati ya mji lazima yapakwe rangi kama hawataki tutabomoa

View attachment 2958158
Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amewataka wamiliki wa nyumba zilizopo katikati ya jiji hilo kuzipaka rangi ili ziwe na mwonekano mzuri vinginevyo nyumba hizo zitabomolewa.

Makonda amesisitiza kwamba Arusha lazima iwe na mwonekano na mandhari ya kuvutia watalii kwani mkoa huo ndiyo kitovu cha utalii nchini. Katika kueleza jambo hilo Makonda amesema

Tunataka Arusha iwe salama salimini tunapata watalii wengi sana haitapendeza wakija wakute hapapo salama. Usalama namaanisha wa kila kitu pamoja na kufanya biashara usiku. Hatutaki Arusha iwe mji mkubwa uliolala. Hao Watalii wakija hapa halafu baadaye wanaenda kulala hiyo hela tunaipata lini? Wametoka kwao hawajaja kulala huku wamekuja kushangaa. Lazima tuhakikishe usalama pamoja na usafi wa mji wetu.
Nilikuwa namdokeza RAS siku moja inabidi akae na wale watu wenye hizi daladala za hapa mjini angalau nasisi tuwe na mabasi ya ghorofa katikati ya mji. Na wenye majengo yao katikati ya mji Wapake rangi kama hawawezi tutabomoa, hatuwezi kuwa na mji umejaa uchafu rangi zinachanganyikana tu. Kamji kazuri haka, kana mandhari nzuri ni sisi wenyewe kukapanga

Nakubaliana naye kwenye kupafanya Arusha pavutie kwa watalii.Vitu vinne vikubwa kwa utaliii ni 1) USALAMA 2) USALAMA 3)USALAMA 4)Miundombinu rafiki.

Nashauri makonda afanye study tour hapo kwa Kagame.atapata cha kujifunza cha kumsaidia kufanya mageuzi ya jiji la Arusha.
 
Asubuhi nilikuwa napitapita hapa nawaona mademu( teenage )smarter than usual katika mavazi yao. Nikafikiria labda hii inahusiana na Makonda.
Lakini huyu ni Makonda mpya---- nyumba zipakwe rangi.
 
Watz tuna tatizo IQ !

Hivi unafikiri makonda anafanya haya yote bila backup ya system!!?

Arusha ni jiji la kitalii kivutio Cha wazungu mji was kitalii lazima uendane na hadhi yake!!

Ngojeni muone!!

Makonda 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥!!
Hata ufisadi wa Richmond wajinga kama ninyi mulituaminisha kuna backup ya system
 
Huyu ndio PAULO MAKONDA haniangushi , ni chizi na hii nchi inahitaji machizi.
 
Nakubaliana naye kwenye kupafanya Arusha pavutie kwa watalii.Vitu vinne vikubwa kwa utaliii ni 1) USALAMA 2) USALAMA 3)USALAMA 4)Miundombinu rafiki.

Nashauri makonda afanye study tour hapo kwa Kagame.atapata cha kujifunza cha kumsaidia kufanya mageuzi ya jiji la Arusha.
Swadakta
 
Arusha wamewadharau sana wamewaletea mwehu awe mkuu wa mkoa!!!
 
Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda amezungumza mambo kadhaa wakati wa hafla ya kukadhiwa ofisi, iliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha, Jumatatu Aprili 08.2024

"Naomba sana ushirikiano wenu, mnionyeshe upendo zaidi, bahati niliyonayo mimi ni kwamba naweza kuwa mtu yeyote mnayemtaka, hiyo ndio kitu pekee ambayo huwa namshukuru Mungu, yaani mimi naweza kujifunza nikawa kiongozi wa aina yoyote.

Ukitaka kiongozi anayekaa na Baba Kadinali Pengo tutasoma sala nitakuwa, ukitaka kiongozi anayekaa na 'General' tukaenda kwa kwata nitakuwa, kokote ambako ninyi mtataka na mimi nitakuwa hivyo, kwa hiyo nitabadilika kutokana na mahitaji yenu na speed tutakayokuwanayo.

Kwa hiyo mahitaji yenu yakiwa ni makubwa na mimi nitaenda kwa speed hiyo, mahitaji yenu yakiwa ni kidogo kidogo nitashindwa kwenda kwa speed kubwa kwa sababu nisiende peke yangu.

Kwa hiyo ni speed yenu tu, mkitaka mji upendeze, mkitaka Arusha ibadilike iwe ni mji wenye amani na utulivu ambapo hata mwananchi anaweza akasahau simu yake mahala akaitiwa itakuwa hivyo, mkitaka Arusha uwe mji wa kibiashara ili wafanyabiashara wetu wapate wafanye biashara zao hadi usiku wa manane itakuwa" alisema Paul Makonda.
 
Huyo kijana alitumika kuzima mjadala wa kuuzwa bandari zetu alipoteuliwa,

Hivi sasa pia anazima Ripoti ya CAG haijadiliwi tena.

Huo uchawi una mwisho.

Tusubiri.
 
Jamaa kashaona CCM wenzie hawataki hvyo ameamua kujilipua tu kwanza akuandikia mtu barua akaomba kazi alikuwa ametulia zake anajilia maishaa wakamleta wakampa uenezi labda Kwa kujua alivyokaa bench kajifunza kumbe walaaaa Hana habari akawawashia moto uko uenezi hata miezi haijakata wamemtoa Kwa spid ya 5G ,wamempeleka Arusha Ili iwe njia ya kumtoaa ,n muda tu utaongeaa

CCM ya ss sitaki watu wa aina ya makonda ,inatka watu wa kusifia mama anaupigaa mwingi nakuvaa nguo zenye picha ya mama mbeleeView attachment 2958149
Hayo ya Makonda, ngoja Erythrocyte wa CHADEMA aendelee kufanya u MC.

Ila mimi nitoe shukurani. Asante kwa picha, nitahakikisha inatumika kwa haki na wakati muafaka.

Wadada zetu wanapendeza kweli kweli.

Kidumu
 
Arusha wamewadharau sana wamewaletea mwehu awe mkuu wa mkoa!!!
Mapokezi ya kishindo

FB_IMG_17125842510366944.jpg
 
Hizi ni miongoni mwa kauli zilizotolewa na Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha katika hotuba kabambe ya Utambulisho aliyoitoa Mjini humo alipokuwa anakabidhiwa ofisi .

Hapa akikuwa akiwapa makavu waliokuwa wanamsengenya kwamba hajajifunza pamoja na kuwekwa benchi muda mrefu.
---
Makonda: Hamna nilichojifunza zaidi ya kuwashughulikia wazembe, wavivu na Wala Rushwa

View attachment 2958155
Akitoa hotuba baada ya utambulisho wake Mkuu wa Mkoa mpya wa Arusha Paul Makonda amesisitiza Viongozi wote kuwajibika na kutoa tahadhari kwa Wazembe. Akiongea mbele ya watu waliojitokeza kumpokea Paul Makonda amesema:

Mmenifurahia sana ila tutageukana muda sio mrefu. Sitajali wewe ni nani, baba yako ni nani, ulipataje hicho cheo, aidha ulipata kwa kuhonga, kwa rushwa au kwa uganga nitakula sahani moja na wewe.
Lazima kila mtu awajibike kwenye nafasi yake. Msiseme huyu alikuwa Mwenezi sasa katoka kwenye Uenezi atakuja amepoa. Wengine wanasema eti saivi labla atakuwa amejifunza, hamna nilichojifunza zaidi ya kuwashughulikia wazembe wavivu na Wala rushwa. Sina elimu yoyote mimi hata niwe Mkuu wa Mkoa wa siku moja inatosha lakini awepo mtu mmoja tu ajue kuna mwanaume amepita hapa.
Kwahiyo kila mtu kwenye nafasi yake, kama ni Mkuu wa Wilaya shika Wilaya yako barabara kama ni Mkurugenzi ishike Halmashauri yako kikamilifu.

Makonda: Majengo yaliyopauka yaliyo katikati ya mji lazima yapakwe rangi kama hawataki tutabomoa

View attachment 2958158
Mkuu mpya wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amewataka wamiliki wa nyumba zilizopo katikati ya jiji hilo kuzipaka rangi ili ziwe na mwonekano mzuri vinginevyo nyumba hizo zitabomolewa.

Makonda amesisitiza kwamba Arusha lazima iwe na mwonekano na mandhari ya kuvutia watalii kwani mkoa huo ndiyo kitovu cha utalii nchini. Katika kueleza jambo hilo Makonda amesema

Tunataka Arusha iwe salama salimini tunapata watalii wengi sana haitapendeza wakija wakute hapapo salama. Usalama namaanisha wa kila kitu pamoja na kufanya biashara usiku. Hatutaki Arusha iwe mji mkubwa uliolala. Hao Watalii wakija hapa halafu baadaye wanaenda kulala hiyo hela tunaipata lini? Wametoka kwao hawajaja kulala huku wamekuja kushangaa. Lazima tuhakikishe usalama pamoja na usafi wa mji wetu.
Nilikuwa namdokeza RAS siku moja inabidi akae na wale watu wenye hizi daladala za hapa mjini angalau nasisi tuwe na mabasi ya ghorofa katikati ya mji. Na wenye majengo yao katikati ya mji Wapake rangi kama hawawezi tutabomoa, hatuwezi kuwa na mji umejaa uchafu rangi zinachanganyikana tu. Kamji kazuri haka, kana mandhari nzuri ni sisi wenyewe kukapanga
Ndege wanaofanana mbawa huruka pamoja.
Hongera kwa mteuzi na mteule
 
Back
Top Bottom