Makonda naye ametumwa na Rais Samia?

Makonda naye ametumwa na Rais Samia?

Mkuu Kalamu heshima sana. Hicho kitisho cha ''mpaka Jumatatu'' ni muujiza mwingine ambao hupatikana ndani ya CCM tu. Hakuna mantiki ndani ya hicho kitisho na muda aliotoa. Ila kwa taarifa ambazo hata mimi nimeshindwa kuzithibitisha ni kuwa kuna timbwili la ndani kwa ndani la siku nyingi kati ya Samia vs Kinana + Makamba Jr + Nape and co. Hili nililisikia siku nyingi lakini nikawa nimepuuza baada ya Makamba kupewa uwaziri wa Nje. Ila huyu mwehu Bashite ni mzuri sana kwenye kusoma migongano ndani ya CCM na kujitafutia ''ushujaa''. Inawezekana akawa hajajiropokea tu.
Ahsante sana mkuu 'macho' kwa haya uliyoweka hapa kwa usahihi kabisa.
Kwa maoni yangu, huu ndio ungekuwa mjadala kwenye mada hii; badala ya kupoteza muda na vitisho vya mtu anayepigania maslahi yake mwenyewe.

Kinachonisikitisha mimi ni kuona nchi yetu hii sasa ni viongozi wa aina hii ya Samia na Makonda ndio wanaotupotezea muda kujadili mambo yasiyokuwa na maana kwa nchi yetu
.Hawa ni 'opportunists' tu walio bahatika kufika kwenye nafasi za uongozi ambazo hawana uwezo nazo, na sasa hili linajidhihirisha kila siku mbele ya macho yetu.
 
Kama Gavana Makonda hakutumwa na Samia, basi atakuwa ni mmoja wa ass kissers bora kabisa kuwahi tokea nchi hii!

Halafu Samia wala hakemei hiyo excessive ass kissing tunayoiona.

Atakuwa anaifurahia.

Jana Makonda kamuita Samia kuwa ni ‘mama’ yake.
Kwa yale maneno pale Arusha bado una shaka kwamba ni ass kisser! wala hakuanza leo, hii ya watu kuinuka na kuinama wakitajwa ni yeye alianzisha wakati wa JPM wakati ana kiss . Kuita JJPM majina manne alianzisha katika 'kissing'. Ni bingwa!

Rais SSH haeleleki, huyu bwana hakufaa hata ujumbe wa nyumba 10. Wakati wa JPM alikuwa na uwezo kuliko VP SSH. Kumrudisha katika uongozi licha ya makando kando na uchafu mwingi alioufanya siku za nyuma inafikirisha. Kibaya zaidi kila siku anaboronga Rais anamhamisha tu ! Kuna mengi yanafikirisha! na taswira yake inakuwa 'tainted'
 
Mwezi uliopita, aliyekuwa mkuu wa majeshi ya ulinzi, Jenerali Venance Mabeyo, aliongea na waandishi wa habari wa gazeti la serikali, Daily News, kuhusu siku za mwisho za Rais John Magufuli.

Wajuzi na wajuvi wa mambo wakadai kwamba ametumwa na Samia kuyasema hayo aliyoyasema.

Kwamba hakusema tu kwa bahati mbaya. Alipewa baraka zote na Samia, ili kutuma ujumbe kwa watu flani flani.

Sasa leo/ jana huko Arusha, Gavana wa mkoa huo, Paul Bashite Makonda, katishia kuwataja watu wanaowatuma baadhi ya watu kumtukana Rais Samia kwenye mitandao ya kijamii.

Gavana Makonda kasema anawajua watu hao ambao kati yao wapo na mawaziri wa serikali ya Samia.

Gavana Makonda kawapa watu hao mpaka Jumatatu ya wiki ijayo wawe wameacha mambo wanayoyafanya, la sivyo, atawataja kwa majina!

Sasa swali ibuka ni, je, Gavana Paul Makonda naye ametumwa na Rais Samia awafikishie ujumbe watu hao kama vile ambavyo ilidaiwa Jenerali Mabeyo alivyotumwa?

Wajuzi wa mambo tujuzeni basi na sie tusio na huo ujuzi na ujuvi wenu 🙏.
CCM NI JANGA LA TAIFA
 
Hivi Makonda angesema kuwa kuna Mawaziri wanataka kukuwekea Mh Rais sumu kwenye chakula nako ingepigwa chini hadi sasa.
 
Kwa yale maneno pale Arusha bado una shaka kwamba ni ass kisser! wala hakuanza leo, hii ya watu kuinuka na kuinama wakitajwa ni yeye alianzisha wakati wa JPM wakati ana kiss . Kuita JJPM majina manne alianzisha katika 'kissing'. Ni bingwa!

Rais SSH haeleleki, huyu bwana hakufaa hata ujumbe wa nyumba 10. Wakati wa JPM alikuwa na uwezo kuliko VP SSH. Kumrudisha katika uongozi licha ya makando kando na uchafu mwingi alioufanya siku za nyuma inafikirisha. Kibaya zaidi kila siku anaboronga Rais anamhamisha tu ! Kuna mengi yanafikirisha! na taswira yake inakuwa 'tainted'
Samia hajui afanyalo.

She is just happy to be there!
 
Back
Top Bottom